Bodaboda anaswa akiendesha basi la abiria

Bodaboda anaswa akiendesha basi la abiria

Nchi imefunguka kwelikweli, watu wanateleza tu. Kila kitu kimekuwa kamseleleko.

Kila idara imelegea tepetepe.

Madhara ya afande nilegezee kamba, ili niweze kukupanga afandeee!!!
Kumbe mwamba huwa unamfatilia zu zu zu zuchuuuu
Oky naskia video ya nyimbo ya afande nilegezee kamba ishatoka.... Vipi unayo hapo
 
Kwani ameliangusha.,..mbona mm nayaendeshaga ambayo Sina leseni yake....kwani nayaangushaga😃, watulie muhimu halijaangushwa
 
mkuu,hakuna mtu hata mmoja katika nchi hii anayeweza kuongea na kuandika kiswahili kwa ufasaha.
Hakika mkuu nami ni mhanga wa l na r...mara nyingi naandika erection badala ya election!!!
 
Hata kama angekua na D bado hana sifa ya kua dereva wa gari za Abiria.
Mkuu sijajua umezaliwa mwaka gani,ni kama vile hauna uzoefu wa maisha ya bongo.
Kitu usichokijua madereva wengi wenye hizo leseni unazotaka wewe hawakupitia darasani wamezipata leseni kwa njia za panya na wanaendesha vizuri tu.
Bongo mtu kuwa na cheti au leseni sio guarantee kwamba kweli alifuzu hayo mafunzo labda nchi za watu wa Ulaya huko mtu akiwa na cheti au leseni inakuwa ni ya uhakika kwa asilimia 100.
 
Mkuu sijajua umezaliwa mwaka gani,ni kama vile hauna uzoefu wa maisha ya bongo.
Kitu usichokijua madereva wengi wenye hizo leseni unazotaka wewe hawakupitia darasani wamezipata leseni kwa njia za panya na wanaendesha vizuri tu.
Bongo mtu kuwa na cheti au leseni sio guarantee kwamba kweli alifuzu hayo mafunzo labda nchi za watu wa Ulaya huko mtu akiwa na cheti au leseni inakuwa ni ya uhakika kwa asilimia 100.
Kwa hiyo sheria zifutwe?
 
Nadhani tayari umemaliza,hivi huyo kijana angekuwa ombaomba sii ungesema tafuta kazi ufanye,sasa mwenzio kaamua kujilipua unalia,Kuna Uzi humu wakenya wanatusema tulivyo waoga hebu jiulize,kufanya service ya deni kubwa kama alilokopa mama ni kitu sahihi,ingekuwa UK huyu kizmkazi asingemaliza hata nusu saa vote of no confidence ingekula kichwa,unawekeza mkataba wa Bandari kwa miaka 100 hii ni low key,sasa Mimi namuunga mkono huyo Ponjoro wa bodaboda sababu he is trying his best level to savege his dinner table,ukienda Mexico huko kuna manati kubwa imetengenezwa ili kurusha drugs kuelekea USA watu wanatafuta Mkate kwa kila namna,sisi wananchi tunahangaika wanasiasa wanakopa kupitia Kodi ndio mana nikasema bora huyo Ponjoro bodaboda alieiona fursa.
Kiinglish hatari
 
Polisi mkoani Morogoro wamemnasa dereva mwenye leseni ya kuendesha bodaboda akiendesha basi la abiria!!!
Inafikirisha.
1. Je, Hilo basi alilokuwa akiendesha lilikuwa na abiria ndani? Tusisahau makonda wengi ndo huenda kuosha mabasi baada ya kutoka safarini.
2. Haijaelezwa alikuwa anatokea au anekwenda wapi.
 
Polisi mkoani Morogoro wamemnasa dereva mwenye leseni ya kuendesha bodaboda akiendesha basi la abiria!!!
Boda boda ni kazi ya laana ( Godbless Lema, 2023).
Wengine hawakumwelewa lema
 
Halafu zikitokea ajali za Mabasi wakafa abiria mnalaumu sio?

Unamtetea mtu anayebeba roho za watu bila kua na leseni?
Leseni ni karatasi tu, angekuwa hajui kuendesha gari asingekamatwa gari ikiwa barabarani angekamtwa kwa kusabisha ajali. Unakuta mtu ana leseni yake miaka mingi anapoenda kurenew anabadilishiwa madaraja kwa sababu tu hana cheti cha VETA. Huu ni upuuzi kama upuuzi mwengine. Kuna Rubani huko South Afrika alirusha ndege akiwa na leseni fake mpaka amestaafu bila kusababisha ajali yoyote. Mwaka 2016 Inchini Kenya kuna kijana ambaye hakuwa na cheti wala leseni ya udakari alifanya upasuaji kwa waagonjwa 9 mmoja peke yake ndo alipoteza maisha nane wakapona matatizo yao. Lakini wa Mhimbili aliyekuwa na kila kitu akamfanyia mgonjwa operation ya kichwa badala ya mguu.
 
Hukumbuki rubani aliejifungia kwenye cockpit n kubamiza dege mlimani huko German,kifo kipo Islael inwakmua watu bila kosa,huyo mwenye boda license Mimi nmpongeza sababu anajaribu fursa sio kulala wakati nchi inapigwa bei dp world na madeni ya kupikwa kimkakati,angalia nchi ina mashimo road zote wewe unaona Raha msng ww.
Yule rubani alikua ni rubani wa siku zote, sema aliugua depression
 
Leseni ni karatasi tu, angekuwa hajui kuendesha gari asingekamatwa gari ikiwa barabarani angekamtwa kwa kusabisha ajali. Unakuta mtu ana leseni yake miaka mingi anapoenda kurenew anabadilishiwa madaraja kwa sababu tu hana cheti cha VETA. Huu ni upuuzi kama upuuzi mwengine. Kuna Rubani huko South Afrika alirusha ndege akiwa na leseni fake mpaka amestaafu bila kusababisha ajali yoyote. Mwaka 2016 Inchini Kenya kuna kijana ambaye hakuwa na cheti wala leseni ya udakari alifanya upasuaji kwa waagonjwa 9 mmoja peke yake ndo alipoteza maisha nane wakapona matatizo yao. Lakini wa Mhimbili aliyekuwa na kila kitu akamfanyia mgonjwa operation ya kichwa badala ya mguu.
Hapa tunajadili sheria inasemaje,huyo daktari wa huko Kenya kama alikua anajua kila kitu,kwanini hakua na leseni? Huko aliposomea hakupewa leseni yake au documents za kumtambua?

Mimi naongelea sheria inasemaje,hizo sababu ulizoziandika hapo,unaweza kwenda Mahakamani na kumtetea huyo mtuhumiwa kwa kutumia sababu hizo na akashinda kesi?
 
Kwani kinacho endesha basi ni leseni au skills za udereva?
Kwani kinachomtambulisha mbele ya sheria ni skills au leseni ya udereva? Polisi wa Barabarani wakikusimamisha hua wanauliza skills au leseni ya udereva?

Mahakamani utajitetea kwa kusema kua una skills ila huna leseni na utashinda kesi?
 
Hapa tunajadili sheria inasemaje,huyo daktari wa huko Kenya kama alikua anajua kila kitu,kwanini hakua na leseni? Huko aliposomea hakupewa leseni yake au documents za kumtambua?

Mimi naongelea sheria inasemaje,hizo sababu ulizoziandika hapo,unaweza kwenda Mahakamani na kumtetea huyo mtuhumiwa kwa kutumia sababu hizo na akashinda kesi?
Mahakani ndo sehemu pekee ambayo unaweza kujikuta umetuhumiwa kwa jambo ambalo hujafanya na ukweli ukawa nao wewe peke yako na Mungu kwamba hujafanya.
 
Back
Top Bottom