Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,920
- 30,263
MBALI NA PAKA WAKE NA MWENYE PAKA MBALI NA NYUMBANI
Wingu limetanda na vua linadondoka ile mvua Mwingereza atasema, "It is raining cats and dogs."
Mvua na wingu jeusi huleta kitu kinaitwa, "melancholy."
Ikiwa kwa bahati mbaya hujui neno hilo muulize Prof. Google.
Always at your service.
Hii ni kwa kawaida.
Sasa kwangu mimi changanya na uzee.
Nasikiliza ''rhythm of the falling rain...''
Si ile nyimbo bali nasikiliza sauti ya mvua yenyewe inavyonyesha.
Wakati mzuri wa kuomba dua.
Majonzi yapo sababu ni hali ya wingu jeusi na kiza cha mchana wa saa saba.
Lakini hakuna "thunder and lightning," ile ya "Three Weird Sisters," katika Mcbeth kana alivyoeleza William Shakespeare.
Hawa ''Weird Sisters'' ni Wanga Watatu.
Naam Wazungu walikuwa washirikina wakiamini uchawi.
Mvua na ''melancholy,'' nishaondoka Magomeni Mapipa sasa niko Edinburgh, Scotland milimani kwenye Edinburgh Castle na hali ya kiza na mawingu ndiyo hii naiona hapa Mapipa.
Allah fundi.
Dakika moja ''split second'' nishafika Scotland naiangalia nchi na milima yake na nawaona wale wanga walimtabiria Macbeth ufalme.
Mara nisharudi Dar es Salaam kijana mdogo wa miaka 15 St. Joseph' Convent School mbele yangu kasimama Miss Menez mwalimu wangu wa Literature ananisomesha fasihi ya Kiingereza mkononi kashika Mcbeth.
Haya yote ''effortlessly.''
Bila shida wala kichwa si kizito kuwa kimeelemewa na taarifa zote nilizohifadhi kichwani.
Hakika neema za Allah hazihesabiki.
Nakwenda mbele narudi nyuma.
Bila tabu wala kutumia nguvu yoyote.
Hivi Hard Disc ya kichwa ni GB ngapi?
Vua tu linadondoka kimya kimya sauti ninayoisikia ni sauti ya matone yakigonga sakafu.
Nje ya dirisha la jikoni ukuta wa ua juu kakaa paka wa binti yangu.
Yeye anapenda paka lakini yu mbali na nyumbani angekuwepo angeniambia paka huyu wake ni kizazi cha ngapi.
Paka wake alipokuwapo mwenyewe huwa wakizaliwa anawapa majina.
Kwangu mimi wote nawaona sura moja.
Yeye anawajua kwa sura na majina na huwa anazungumzanao na wakimuudhi huwatishia kuwaadabisha kwa mikwaju.
Paka wanatii amri.
Wakiumwa anawatia kwenye kikapu anawapeleka hospitali kutibiwa tena kikapu kakibeba ndani ya mwendokasi au daladala.
Nimemwangalia paka anajificha mvua.
Paka kanikumbusha mwanangu mbali na nyumbani.
''Mbali na Nyumbani,'' ni kitabu cha mwandishi maarufu wa fasihi Adam Shafi.
Ashiki kitabu hiki.
''Ashiki Kitabu Hiki,'' hicho ni kitabu cha Shaban Robert.
Mvua hii inanishawishi niingie Maktaba nikitafute ''Mbali na Nyumbani,'' nipate kukitalii.
Huwezi kuchoka kumsoma Adam Shafi.
Kanihadithia Adam Shafi.
Anasema alikuwa Ulaya kwa binti yake anaandika kitabu.
Toka asubuhi mwanae ni kuleta kahawa kikombe baada ya kikombe.
Jioni mtoto kapata hamu ya kujua baba yake kaandika nini kutwa nzima.
Adam Shafi akamuonyesha.
''Ba, siku nzima hata ukurasa mmoja hujamaliza!
Chao!
melancholy
noun
a feeling of pensive sadness, typically with no obvious cause.
"an air of melancholy surrounded him"
Wingu limetanda na vua linadondoka ile mvua Mwingereza atasema, "It is raining cats and dogs."
Mvua na wingu jeusi huleta kitu kinaitwa, "melancholy."
Ikiwa kwa bahati mbaya hujui neno hilo muulize Prof. Google.
Always at your service.
Hii ni kwa kawaida.
Sasa kwangu mimi changanya na uzee.
Nasikiliza ''rhythm of the falling rain...''
Si ile nyimbo bali nasikiliza sauti ya mvua yenyewe inavyonyesha.
Wakati mzuri wa kuomba dua.
Majonzi yapo sababu ni hali ya wingu jeusi na kiza cha mchana wa saa saba.
Lakini hakuna "thunder and lightning," ile ya "Three Weird Sisters," katika Mcbeth kana alivyoeleza William Shakespeare.
Hawa ''Weird Sisters'' ni Wanga Watatu.
Naam Wazungu walikuwa washirikina wakiamini uchawi.
Mvua na ''melancholy,'' nishaondoka Magomeni Mapipa sasa niko Edinburgh, Scotland milimani kwenye Edinburgh Castle na hali ya kiza na mawingu ndiyo hii naiona hapa Mapipa.
Allah fundi.
Dakika moja ''split second'' nishafika Scotland naiangalia nchi na milima yake na nawaona wale wanga walimtabiria Macbeth ufalme.
Mara nisharudi Dar es Salaam kijana mdogo wa miaka 15 St. Joseph' Convent School mbele yangu kasimama Miss Menez mwalimu wangu wa Literature ananisomesha fasihi ya Kiingereza mkononi kashika Mcbeth.
Haya yote ''effortlessly.''
Bila shida wala kichwa si kizito kuwa kimeelemewa na taarifa zote nilizohifadhi kichwani.
Hakika neema za Allah hazihesabiki.
Nakwenda mbele narudi nyuma.
Bila tabu wala kutumia nguvu yoyote.
Hivi Hard Disc ya kichwa ni GB ngapi?
Vua tu linadondoka kimya kimya sauti ninayoisikia ni sauti ya matone yakigonga sakafu.
Nje ya dirisha la jikoni ukuta wa ua juu kakaa paka wa binti yangu.
Yeye anapenda paka lakini yu mbali na nyumbani angekuwepo angeniambia paka huyu wake ni kizazi cha ngapi.
Paka wake alipokuwapo mwenyewe huwa wakizaliwa anawapa majina.
Kwangu mimi wote nawaona sura moja.
Yeye anawajua kwa sura na majina na huwa anazungumzanao na wakimuudhi huwatishia kuwaadabisha kwa mikwaju.
Paka wanatii amri.
Wakiumwa anawatia kwenye kikapu anawapeleka hospitali kutibiwa tena kikapu kakibeba ndani ya mwendokasi au daladala.
Nimemwangalia paka anajificha mvua.
Paka kanikumbusha mwanangu mbali na nyumbani.
''Mbali na Nyumbani,'' ni kitabu cha mwandishi maarufu wa fasihi Adam Shafi.
Ashiki kitabu hiki.
''Ashiki Kitabu Hiki,'' hicho ni kitabu cha Shaban Robert.
Mvua hii inanishawishi niingie Maktaba nikitafute ''Mbali na Nyumbani,'' nipate kukitalii.
Huwezi kuchoka kumsoma Adam Shafi.
Kanihadithia Adam Shafi.
Anasema alikuwa Ulaya kwa binti yake anaandika kitabu.
Toka asubuhi mwanae ni kuleta kahawa kikombe baada ya kikombe.
Jioni mtoto kapata hamu ya kujua baba yake kaandika nini kutwa nzima.
Adam Shafi akamuonyesha.
''Ba, siku nzima hata ukurasa mmoja hujamaliza!
Chao!
melancholy
noun
a feeling of pensive sadness, typically with no obvious cause.
"an air of melancholy surrounded him"