Binti mmoja katia doa ndoa yangu

Binti mmoja katia doa ndoa yangu

WA KISHUA

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
365
Reaction score
130
Habari za asubuhi waungwana,

Poleni sana na uchovu wa weekend ndefu na sikukuu za Pasaka, hasa kwa wale wapenda bata kama mimi. Vitabu vitakatifu vinakwambia msema kweli mpenzi wa Mungu, sio siri nimejitaidi kuuchuna lakini roho inanituma niseme.

Imepita kama miezi mitatu tangu nifahamiane na huyu binti, tulifahamiana kwenye mgahawa mmoja upo pale Makumbusho barabarani unaotazama na geti la kwenda kwenye kota za usalama.

Mimi ni mteja wao mkubwa sana pale hasa nyakati napokuwa natoka kazini mida ya jioni huwa napitia pale kupasha tumbo. Huyu binti ni accountant kwenye Microfinance moja hapa mjini. Kiukweli huyu mtoto ameumbika, mrembo, mweupe, mrefu na msafi kweli kweli.

Amepanga nyumba nzima maeneo ya Mikocheni kwa Nyerere ana usafiri mzuri i mean anatembelea Harrier Lexus pia ana ist pale nyumbani kwake anaishi na mdogo wake wa kike na housegirl pamoja na mlinzi wa kaka secirity.

Kwa ufupi yupo vizuri, ila kwa alichonifanyia siku ya Pasaka ndicho kimenifanya hasa nilete uzi huu kwenye meza ya MMU. Binti alinipigia cmu mida ya asubuhi akanikaribisha Pasaka niende nikapige msosi kwake. Nikamwambia siyo kesi nitaenda.

Kufika mida ya saa 8 ikabidi nimtie sound wife kuwa natoka mara moja, basi bhana baada ya my baby mama kunipa greenlight breki ya kwanza getini kwa huyu binti sio siri huyu mwanamke ni mtundu na anamapenzi hata jini mahaba sidhani kama anaweza kuwa nayo.

Baada ya kufika tuu nikapokelewa kwa bashasha za kufa mtu, mabusu na mashamsham kibao, ikabidi nihoji mdogo wake na housegirl wako wapi? Akasema wameenda kula Pasaka kwa mama yake anaishi Msasani. Basi libeneke likaendelea pale, sio siri sikutaka kabisa ku-sex na huyu mwanamke ila nilishindwa kujizuia na kujikuta maji yakizidi unga.

Nakiri kusema sijawahi pewa mapenzi kama haya jamani, huyu mwanamke ana mapenzi mpaka shetani anamuogopa. Najuta kusaliti ndoa yngu. Nafikiria kumuomba radhi wife japokuwa mpaka sasa hajagundua chochote kinachoendelea ila huyu mwanamke ametokea kunichanganya kwa kweli.

Nashindwa niamue lipi, maana nikimueleza wife ukweli hakutakalika ndani kabis. Nahitaji ushauri wenu, naipenda ndoa yangu na wife pia.

Angalizo: Wenye matusi uzi huu hauwahusu kabisa.
 
Binadamu pote pake apatapo pakushika kaka.
 
Huyu binti ni accountant kwny Microfinance moja hapa mjini. Kiukweli huyu mtoto ameumbika, mrembo, mweupe, mrf na msafi kweli kweli.

Amepanga nyumba nzima maeneo ya Mikocheni kwa Nyerere ana usafiri mzuri i mean anatembelea Harrier Lexus pia ana ist pale nyumbani kwake anaishi na mdg wake wa kike na housegirl pmj na mlinzi wa Kk secirity.
 
Pole sana mkuu...lakini nahofia unaweza kuchonga mzinga kabisaa. Swali ni je, ulimtongoza hapo awali? kama ulimtongoza yote uliyatak wewe kama hukumtongoza mwambie ukweli huyo Binti kuwa una mke na unaipenda familia yako ili ajue hilo pia. Ukimwambia mkeo utakuwa umekoroga sumu kwenye maji ukidhani ni sukari unywe. Angalia usije telekeza familia mkuu utadhani umerogwa kumbee...pole sana
 
Kwanza pole sana na pili hongera sana kwa kufaidi utamu for time being..! Potezea tuu usimwambie ishi maisha ya kutopenda kufanya nae open relation uwe unakula kuku kwa mrija i mean silently silently
 
Ahahahahah duuh wacha nicheke kwanza,nakuelewa unayoyasema kua umepewa vitu adimu sasabasi chakufanya usimwambie mkeo ila mnunulie japo zawadi nzuri sana ya thamani kama uwezo upo kama huna japo pete au hata pesa mpe mwambie akanunue anachotaka,nanikulize sasa huyo wa Kibondei ndio basi au ndio ukishindwa kujizuwia unaenda kusukutua moyo?
 
Hongera kupata tam ya dam za Tanga hz,kufanya kosa sio kosa ukirudia ndo kosa mpotezee ikibid kata mguu
 
Umeshatenda dhambi teyari,ili kunusuru ndoa yako kata mawasiliano na bint huyu kabisa. Usifikiri wewe ni wa kwanza wapo wengi wameshapita kwenye mikono ya huyo bint,hivyo kuendelea naye ni hatari sana kwa ndoa yako
 
Oa wake wawili kama mzee Mengi,ya nini kupata shida
 
So unataka kumwambia mkeo kuwa umepata mchepuko wenye mautundu kuliko yeye??? Acha ujinga ndugu yangu. Uchepukaji huleta adha si tu kwa mkeo bali familia nzima unaiathiri kwa kushindwa kufikiria mambo yenye tija kwa family unashinda siku nzima ukiwaza limchepuko la kibondei!!?
 
Ni kawaida upatapo kitu kipya akili huwa ina stuck hapo, ila baada ya muda kama utaendelea kujilia vinono utamkinai na kumuona wa kawaida sana.
 
Kwa mbondei!!!!!!!!!!!!!??????????????? Pole kwa kuwa ulichonga mzinga kabla ya kulamba asali.... Ulichoandika zaidi ni taarifa za mchepuko wako ulivyoumbika na bila kusahau penzi la kichawi linalohatarisha uwepo wa ndoa yako.... Nadhani sijaandika matusi kama ulivyotaadharisha ila nimejaribu kukuhabarishe ukweli japo kama usipotafakari vya kutosha utahisi ni matusi.
 
Hayo mautundu uliyopewa na mbondei ungemfundisha mkeo itakuwa pouwah utafunguza kuchepuka kidizaini fulani
 
Hapo unaomba ushauri gn mkuu mbona unatufanya kama watoot wadogo umemcfia weeeee na mzigo umepiga mi nakuomba uweke picha hapa yake na ya mke wako pia namba zao
 
hapo ndo ujue cheatng is nt a mistake its a choice
 
Hii story inasound kama ki2 cha kufirika...
 
Back
Top Bottom