fungi06
JF-Expert Member
- Jul 1, 2020
- 632
- 854
Itatokea nini pale ambapo ukiwaeka pamoja mchwa 100 wekundu na wengine 100 mchwa weusi kwenye chupa moja???
Kikawaida hakuna lolote litatokea!!
Lakini balaa litatokea pale Ambapo
Utaitingisha chupa ambayo ndani yake wapo mchwa (wekundu na weusi)
Mchwa wekundu wataamini adui ni mchwa weusi, Vivyo hivyo mchwa weusi wataamini adui yao ni mchwa wekundu
Wataanza kupigana sana bila kujua adui yao ni alie tingisha chupa!.
Vivyo hivyo kwenye jamii zetu, kabla hatujaanza farakana au kugombana na wenzetu kwenye jamii yetu, lazima tujiulize. Je ni nani alie tingisha chupa?
Amani itutawale