Bima ya afya

nard

Member
Nov 10, 2011
28
28
Naomba kufahamishwa na yeyote mwenye taarifa sahihi kuhusu mapato ya mfuko wa taifa wa bima ya afya. Swali langu la msingi "Ni kiasi gani mfuko wa taifa wa bima ya afya hupata kutoka katika mishahara ya wafanyakazi wa serikali kwa mwaka?" hata hivyo kiu yangu ya kufahamu hilo haitaishia hapo kwani nilihitaji kufahamu zaidi "fedha hizo zinazidi au zinapungua kwa kiasi gani ukilinganisha na bajeti ya serikali kwenye wizara ya afya?"
 
Mimi namshauri mkurugenzi wa shirika la bima ya afya kuangalia uwezekano wa kuwakopesha wanachama wa mfuko huo.

sidhani kama ni sahihi maana nafahamu hata wakisema ni mikopo nafuu lazima kuna riba ni kwa nini wasitoe matibabu kwa watanzania wote bure maana hayo ndiyo malengo yao na siyo biashara!
 
Ajabu ni kuwa makato ya bima ya afya huanza mara tu mtu aajiriwapo na gov.t kabla ya mwajiriwa kujaza form za kuhitaji huduma za mfuko huu. Hata mwajiriwa anapojaza form zao, huchukua miezi miwili au mitatu kabla ya kupewa kitambulisho. Wakati wote huo hela hukatwa ktk mshahara pasipo huduma kwa mwajiriwa mpya... WIZI MTUPU
 
Back
Top Bottom