Billcanas wanakwepa kodi, TRA tafadhali chukua hatua

Billcanas wanakwepa kodi, TRA tafadhali chukua hatua

mleta mada huna lolote ushakunaku umekujaa tyu! Huwezi kuwa na club katikati ya mji posta kama bilizz ukwepe kodi. Kajipange.

tunachotaka, watoe risiti, sio hao billcanas tu. Kumbi zote zinazotoza viingilio, lazima zitoe risiti, sio ombi. Lazima.

Tusubiri kidogo, tutajua kama wanalipa kodi au la.

Nilichosema hapa, ijumaa hawakutoa risiti, hata pale walipoombwa kufanya hivyo.

Risiti ni haki yetu.sio ombi
 
tutamshika awe ccm,awe act awe ukawa.

Ukwepaji kodi ni uvunjaji wa sheria. Sheria haina chama cha siasa

Ni tatizo la serikali dhaifu inayotakiwa kusimamia sheria na kukusanya mapato yake; hii ni kutokana na kuwa na uongozi unaoingia maradarakani kwa pesa za wakwepa kodi.
 
Ngonjera iko wapi? Nimekueleza kwamba hawatoi risiti. Na risiti ni haki yetu walipaji wa tozo yeyote ile.
Nimeomba pia kumbi zote zichunguzwe, sio Billcanas tu.

Sasa unataka niwaambie nini TRA

Tanzania KWANZA, vikojozi baadaye

Hii kwanza Ni kituko habari za kusimuliwa pili nimeingia kumbi mbali mbali duniani za Burudani kama South Africa, Uingereza, China Dubai sijawahi kupewa Risiti labda kama unatoka na kuwambia narudi tena ndipo watakugonga mhuri au watakupa risiti. Si kuingia ndani hii umetokota kabisa anza upya.
 
tunachotaka, watoe risiti, sio hao billcanas tu. Kumbi zote zinazotoza viingilio, lazima zitoe risiti, sio ombi. Lazima.

Risiti ni haki yetu.sio ombi

Kama ni haki yako tuonyeshe risiti uliyopewa. Kama sivyo wewe ni mhalifu.

Halafu hapa siyo mahali pa hiyo hoja wasaidie TRA kwa taarifa ulizo nazo wazifanyie kazi.

Nikusaidie bure elimu ya uraia ni pamoja na wananchi kupenda kulipa kodi hiyo ndiyo tafsiri sahihi ya UZALENDO; kwetu sisi Elimu hiyo tumenyang'anywa kadri CCM ilivyokuwa inashika hatamu kwa kujitwalia majumu ya serikali. Huku mitaani osisi za CCM hutoa barua au hugongea mihuri kwa tozo. Shughuli zote za CCM wafanyabiashara lazima wachangie tena bila risiti. Polisi nao wanatoa risiti kwa makosa ya traffic wakati makusanyo yanatakiwa yafanywe na TRA tu.

Mifano ni mingi kama ulivyosema tusubiri tuone majipu yanavyotumbuliwa. Na hasa jipu la fadhila za CCM kwa wanaoichangia kwa kulazimishwa na polisi kuwa na risiti unapokamatwa bila kupelekwa mahakamani.

Chini ya CCM kuna madudu watayafunua wenyewe kwa kutekeleza ilani ya upinzani maana hii haikuwa ilani yao.
 
Siku Watz tukiacha hizi chuki za kijinga tutafika mbali sana. Kama mtu ana nia nzuri na hii nchi, swala kama hili alitakiwa aliripotishe TRA na sio kuliripotisha JF. Baadhi ya wachangiaji wa JF watachangia kwa kuonyesha personal attack kwa mmiliki wa Club hiyo ambaye ni Mbowe lakini haitasaidia kupata hiyo kodi inayosemwa inapotea. Tuache chuki, tujenge nchi, tuwe Wazalendo!
 
Inakuwaje mtu mwenye kiduka cha shanga kariakoo aambiwe awe na mashine ya efd halafu danguro kubwa kama hilo lisiwe na mashine za efd kwanini? tena ingewezekana wawe wanawasilisha mahesabu tra kila siku asubuhi kwa mauzo ya jana yake.

Pale kuna viingilio, vinywaji, nyama choma, malipo ya wasanii na madj haya yote hayalipiwi ushuru na kodi halafu huyu mtu tunamchekea tu. Hizi night clubs ziko ngapi nchi nzima? tunapoteza mapato kiasi gani?

kwanza kabla ya kufunguliwa NEMC walikagua kuona kama mazingira yako safi? kuna hewa ya kutosha? maji taka wanatiririsha wapi manake bar kama hiyo mikojo yeke usiombe.

Mnakurupuka sana watu Wa CCM. Sheria ya kumbi za Disco Ni tofauti na vitu vingine tafiti kwanza.
 
hayo yote ni makosa inabidi kurekebsisha mazoea hayahalalishi haramu, .

asante sana ndugu zekidon, sababu watu hawajazoea kupewa au kudai risiti.

SIJUI KITENGO CHA TRA ELIMU KINAFANYA NINI, WANACHOPASWA KUFANYA, NI KUWAELIMISHA WATANZANIA WOTE ULAZIMA WA KUPEWA RISITI, WAWEKE NAMBA AMBAYO TUTAPIGA PALE TUNAPONYIMWA RISITI.

RISITI NI HAKI YA MLIPAJI KISHERIA, RISITI NI HAKI YA SERIKALI KISHERIA.

TUMSAIDIE RAIS WETU KUKUSANYA MAPATO ILI NCHII IPIGE HATUA KWELI KWELI.

LAZIMA TUAMKE NA KUTAMBUA HAKI ZETU.

PIPI MOJA YA EURO 0.50 HUTOLEWA RISITI HUKO SCANDNAVIA, NDO MAANA WANAPIGA HATUA, KILA MTU ANALIPA KODI KWA NAFASI YAKE, BAADAYE WATANZANIA WOTE WANAFAIDIKA KWA UJUMLA.

NIMESEMA KUMBI ZA STAREHE HAQZILIPI KODI, HAZIFUATILIWI.
TANZANIA KWANZA,VIKOJOZI BAADAYE

ZIFUATILIWE, ZIWEKEWE UTARATIBU WA KULIPA KODI NA KUTOA RISITI
 
kama ni haki yako tuonyeshe risiti uliyopewa. Kama sivyo wewe ni mhalifu. Halafu hapa siyo mahali pake wasaidie tra kwa taarifa ulizo nzo wazifanyie kazi.

mpumbavu sana wewe, hapa sio mahali pake, hapa ni mahali pa kufanya nini,?

Hapa ndo mahali pekee watanzania tunafunguka bila uoga.

Juzi mtu kaleta uzi wa madawa ya kulevya uko mwenge, jana lijamaa limeshikwa.

Hapa ndo mahali pake.tunasema openly, wenye kumbi zote za starehe, walipe kodi na watoe risiti, tutasema mpaka jpm atasikia

risiti.risiti.risiti

tanzania kwanza,vikojozi baadaye
 
siku watz tukiacha hizi chuki za kijinga tutafika mbali sana. Kama mtu ana nia nzuri na hii nchi, swala kama hili alitakiwa aliripotishe tra na sio kuliripotisha jf. Baadhi ya wachangiaji wa jf watachangia kwa kuonyesha personal attack kwa mmiliki wa club hiyo ambaye ni mbowe lakini haitasaidia kupata hiyo kodi inayosemwa inapotea. Tuache chuki, tujenge nchi, tuwe wazalendo!

hao tra ni wazembe, wamejaa rushwa, hata ukisema hawasikilizi. Tunasema hapa hapa, imani yetu jpm atasikia.

Jana wamemshika muuza unga uko mwenge, uzi ulianza hapa hapa jf.

Hao vigogo wote wanapitia jf. Huyo kamishna wa elimu tra atolewe kabisa, hatoi elimu yeyote.
 
Huyo Makengeza afilisiwe mali zote za urithi...mshenzi mkubwa huyo...yani wananchi tunaangaika hatupati huduma kumbe halipi kodi ya biashara zake!?!😠
Ni jambo jema kama pro ccm mnaanza kuwa conscious na kodi
 
siku watz tukiacha hizi chuki za kijinga tutafika mbali sana. Kama mtu ana nia nzuri na hii nchi, swala kama hili alitakiwa aliripotishe tra na sio kuliripotisha jf. Baadhi ya wachangiaji wa jf watachangia kwa kuonyesha personal attack kwa mmiliki wa club hiyo ambaye ni mbowe lakini haitasaidia kupata hiyo kodi inayosemwa inapotea. Tuache chuki, tujenge nchi, tuwe wazalendo!

tumesema kumbi zote za starehe, billcanas nimeitaja sababu nimejirizisha hawatoi risiti
 
pathetic....eleza vizuri toa na ushaidi sio una leta ngonjera humu. toa maelezo yaliyo nyooka ili kuisaidia TRA!
Wewe mkibosho mbona una kichwa kigumu hivyo? Umeambiwa kabisa kuwa watu wanatozwa pesa mlangoni bila kupewa risiti na maana yake hapo kuwa serikali haipati mapato!

Nilishakwenda Maisha club mtwara pale mlangoni wana EFD machine walinifurahisha sana na nilidhani hawa ndio walitakiwa kuwa mfano wa kuigwa!
Yani mtu hatoi hata risiti atawezaje kulipa kodi inayo stahili?
 
Back
Top Bottom