Billcanas wanakwepa kodi, TRA tafadhali chukua hatua

Billcanas wanakwepa kodi, TRA tafadhali chukua hatua

Wasanii wakifanya show wanalipa kodi? Au tamasha lolote? Na kumbi za harusi na harusi zenyewe wanalipa kodi?
Kwa hiyo haya yana halalisha Mbowe kukwepa kodi?
 
Unaweza kushangaa kesho Majaliwa na team yake wanatia team hapo.
 
Ngonjera iko wapi? Nimekueleza kwamba hawatoi risiti. Na risiti ni haki yetu walipaji wa tozo yeyote ile.
Nimeomba pia kumbi zote zichunguzwe, sio Billcanas tu.

Sasa unataka niwaambie nini TRA

Tanzania KWANZA, vikojozi baadaye

Ni taarifa nzuri na itawasaidia TRA kukusanya mapato.

Lakini ainisha na maeneo menguine ambayo umetembelea na pia toa mifano ya kumbi zingine ambazo wanatoa Riceipt kwa kila anayeingia ukumbini ili iwe mfano.
 
Tukiweka mahaba na ushabiki pembeni....na kuuweka uzalendo mbele.....hili suala ni la muhimu mno hasa katika kipindi hiki....
 
"Ijumaa tarehe 26.11.2015" ulimaanisha nini,
wanaolipa kodi kihalali kabisa bila kukwepa wengi ni wafanyakazi kwa sababu mfumo uliowekwa hauwapi chance ya kukwepa
 
Ijumaa tarehe 26.11.2015 rafiki yangu alifika Billcanas Club kwa ajiri ya kujifurahisha ambapo Club hiyo ilikuwa inazinduliwa upya baada ya kufunga mitambo mipya.

Alipofika mlangoni, alilipa kiingilio cha shs 10,000. Akaomba risiti ya malipo lakini hakupatiwa. Akasisitiza na kuambiwa hapa hakuna risiti. Risiti ni haki ya mlipaji. Risiti uonesha serikali inapata kodi kiasi gani kutokana na tozo. Naomba ukumbi huu na kumbi zote zianze kutoa risiti mara moja la sivyo TRA iwafungie.

Ukumbi unaobeba watu 2000. wakilipa 10,000. ni sawa na 20,000,000. Ni pesa nyingi zinapotea, hapo bado vinywaji ninauzwa bei ya juu sana ndani bila risiti yeyote. TRA chunguzeni hizi sekta za burudani, taifa linapoteza mapato humo.

Utaweweseka sana na kwa taarifa yako tu ni kuwa hakuna mtu analipa kodi kama mbowe
 
Asante sana EDDY, umenyoosha maelezo. TRA inpoteza mapato mengi mno mwisho wa wiki kwenye hizi kumbi za usiku. Zikipewa EFD zote, halafu zikadhibitiwa kiuhakika, mapato makubwa sana yatakusanywa

Tanzania KWANZA, vikojozi baadaye

Kumbe wewe ni kikojozi?
 
Billicanas kwanza maeneo mengine baadaye,ww kama mbowe ni anko wako ndo sasa umwambie tunahitaji risiti
 
ule ukumbi una cctv camera police wakamate server wadown load ni ushahidi tosha kabisa then apigiwe hesabu kwa muda wote club hiyo imefanyakazi alipe mara moja na kama mmiliki ni mtumishi wa umma unabidi aondolewe mara moja hatuwezi kulea majizi serikalini hata kama ni mbunge.

eddy ndugu yangu naamini wewe ni mtanzania na unaelewa ukumbi huo unamilikiwa na nani kwa jinsi siasa zetu hapa tanzania hapo kunge kuwa na ukwepaji wa kodi yoyote sasa hivi pangekuwa pameshafungwa
 
Hiv nyie CCM nani kawaloga??? Anzeni kwanza na viongozi wenu ndo mje kwa mbowe, kila siku kwa mwali kwa kungwi lini??? Mbona hatusikii mlivyo na roho mbaya nyie
 
pathetic....eleza vizuri toa na ushaidi sio una leta ngonjera humu. toa maelezo yaliyo nyooka ili kuisaidia TRA!

Sasa maelezo gani ya ziada unayosubiri hapo?
Bilicanas wanatoa huduma bila ya risiti (EFD), ni ukwepaji wa kodi sasa unataka kielezwa nini cha ziada!
 
Back
Top Bottom