Billcanas wanakwepa kodi, TRA tafadhali chukua hatua

Billcanas wanakwepa kodi, TRA tafadhali chukua hatua

Ww ndiye mkwepa kodi namba moja ukijinufaisha na serikali iliyo pita. Mwenzako waliwahi kumzushia bungeni wakashindwa sembuse humu jf.
 
We unaongelea kodi za kumbi za starehe tu. Hujaona kodi za nyumba. Wapangaji wanalipa hela nyingi sana kwaajili ya nyumba walizopanga. Nu shilinhi ngapi Tz inapoteza. Huyohuyo anaelipwa anailalamikia serikali kuwa ni wezi,Mara wanasamehe kodi kitendo kinaipotezea nchi mabilions ya mapene. Yeye hajioni. Piga mahesabu ya chekechea tu. Wilayaoja ya kinondoni ingekusanya Kodi ya pango kwa mwezi wangeiingizia serikali shilingi ngapi??? Nayo waangaliwe kwa jicho lakimakufuli. Watendaji wetu ni mazuzu,wanahangaila na Wamama wenye mtaji wa karaka kilo mbili tsh 4400 na karatasi 1000 mkaa 1500 kopo tena haliishi-- 6900. Wanamdai kodi wakati mwingine anaingiza mafedha kibao halipishwi. Huu ni zaidi ya uchizi. Magufuli waangazie. Jipu lao limekomaa ni lakuchana c lakutumbua
 
Ijumaa tarehe 26.11.2015 rafiki yangu alifika Billcanas Club kwa ajiri ya kujifurahisha ambapo Club hiyo ilikuwa inazinduliwa upya baada ya kufunga mitambo mipya.

Alipofika mlangoni, alilipa kiingilio cha shs 10,000. Akaomba risiti ya malipo lakini hakupatiwa. Akasisitiza na kuambiwa hapa hakuna risiti. Risiti ni haki ya mlipaji. Risiti uonesha serikali inapata kodi kiasi gani kutokana na tozo. Naomba ukumbi huu na kumbi zote zianze kutoa risiti mara moja la sivyo TRA iwafungie.

Ukumbi unaobeba watu 2000. wakilipa 10,000. ni sawa na 20,000,000. Ni pesa nyingi zinapotea, hapo bado vinywaji ninauzwa bei ya juu sana ndani bila risiti yeyote. TRA chunguzeni hizi sekta za burudani, taifa linapoteza mapato humo.

chuki hazina nafasi kwa magufuli,na upeo wako ni mdogo sana na hata bills hupajui.na hata uelewa wa maswala ya kodi wewe ni ziro kabisa
 
chuki hazina nafasi kwa magufuli,na upeo wako ni mdogo sana na hata bills hupajui.na hata uelewa wa maswala ya kodi wewe ni ziro kabisa

mkuu nashukuru, sio sifa kupajua bills, kheri yako mjanja wa mjini. Suala lililopo hapa ni ukwepaji wa kodi za kumbi za burudani ukiongozwa na aliyekuwa mkuu wa kambi ya upinzani.

Tunahitaji risiti,risiti na risiti
 
we unaongelea kodi za kumbi za starehe tu. Hujaona kodi za nyumba. Wapangaji wanalipa hela nyingi sana kwaajili ya nyumba walizopanga. Nu shilinhi ngapi tz inapoteza. Huyohuyo anaelipwa anailalamikia serikali kuwa ni wezi,mara wanasamehe kodi kitendo kinaipotezea nchi mabilions ya mapene. Yeye hajioni. Piga mahesabu ya chekechea tu. Wilayaoja ya kinondoni ingekusanya kodi ya pango kwa mwezi wangeiingizia serikali shilingi ngapi??? Nayo waangaliwe kwa jicho lakimakufuli. Watendaji wetu ni mazuzu,wanahangaila na wamama wenye mtaji wa karaka kilo mbili tsh 4400 na karatasi 1000 mkaa 1500 kopo tena haliishi-- 6900. Wanamdai kodi wakati mwingine anaingiza mafedha kibao halipishwi. Huu ni zaidi ya uchizi. Magufuli waangazie. Jipu lao limekomaa ni lakuchana c lakutumbua

acha kukurupuka.

Uzi huu ni kuhusu ukwepaji wa kodi kwenye kumbi za burudani zikiongozwa na billcanas.
 
ww ndiye mkwepa kodi namba moja ukijinufaisha na serikali iliyo pita. Mwenzako waliwahi kumzushia bungeni wakashindwa sembuse humu jf.

serikali iliyopita...............

Serikali ya jpm tunazuia ukwepaji wote wa kodi.

Rais kasema tutumbue majipu,,mimi natumbua ili la kumbi za burudani, pole kama usaa unatoka sana,,tutaweka chumvi kutuliza maumivu
 
kwa shuluba walizopata ccm kutoka upinzani, wasingemwacha mbowe akwepe kodi kirahisi hivyo.
Mfanyabiashara yeyote tz akiwa upinzani huweza kuzuliwa zengwe hadi kufilisiwa biashara zake, sembuse kukwepa kodi?
Wafanyabiashara wengi wana kadi za fisiem ili kulinda biashara zao.


hakuna ccm wala ukawa

mkwepa kodi ni adui wa watanzania wote,, kama unamfahamu mkwepa kodi,,tafadhari weka humu jf awe ccm au ukawa. Otherwise shut up
 
Ijumaa tarehe 26.11.2015 rafiki yangu alifika Billcanas Club kwa ajiri ya kujifurahisha ambapo Club hiyo ilikuwa inazinduliwa upya baada ya kufunga mitambo mipya.

Alipofika mlangoni, alilipa kiingilio cha shs 10,000. Akaomba risiti ya malipo lakini hakupatiwa. Akasisitiza na kuambiwa hapa hakuna risiti. Risiti ni haki ya mlipaji. Risiti uonesha serikali inapata kodi kiasi gani kutokana na tozo. Naomba ukumbi huu na kumbi zote zianze kutoa risiti mara moja la sivyo TRA iwafungie.

Ukumbi unaobeba watu 2000. wakilipa 10,000. ni sawa na 20,000,000. Ni pesa nyingi zinapotea, hapo bado vinywaji ninauzwa bei ya juu sana ndani bila risiti yeyote. TRA chunguzeni hizi sekta za burudani, taifa linapoteza mapato humo.

Nzuri sana
Ila fanya hiana upate data za kutosha peleka TRA upate 3% ya hiyo kodi iliyopotea
 
mbona umenyonya mziki kwenye flash lakini hukugagania kupewa risti hujui kuwa umekwepa kodi au maandaz uliyokula leo umelipia kodi ?

nalipa kodi yangu kwenye mshahara wangu, nalipa kodi yangu kwa kila nunuzi nalolifanya kwa kudai risiti,,hata ninunue luku ya 1000, lazima nidai risiti, huu ni wajibu wangu kwa nchi yangu
 
Nina wasiwasi na Mtoa Mada kama Yeye ama huyo ndg yake aliwahi kuingia bills, bills haina mahala pa kuweka hata watu 1000,

Pale bills risiti zilianza kutolewa hata kabla ya machine za EFD, sasa kama kodi inafika TRA ni swala lingine, sehemu ya strarehe niliyoona wanatoa risit za EFD dsm ni samakisamaki mlimani city
 
nitajie club zinazolipa kodi hapa nchini na kutoa risiti we mwana hizaya..!

kwa kuwa club nyingine hazitoi risiti ina maana ndo hatuna haki ya kudai risiti.

Nimesema billcanas ninao ushahidi wa hili la kutotoa risiti, tra wachunguze kumbi zote za starehe,,wakianza na hii club billcanas
 
hakuna club inayotoa risiti mlangoni bongo, tunaojua ni sisi tunaoenda club sio nyie wapuuzi

nashukuru sana kwa kuwa mpuuzi,,hongera mwerevu mwenda viwanja. Nachokuahidi,,soon utaanza kupewa risiti...nachokuomba,,,dai risiti club yeyote uendayo
 
Ninatumaini watu wa tra mnaona huu upotevu wa mapato
 
Mimi mwenyewe niliingia hapo jana yani sikuelewa kabisa ule utaratibu. Mtu unalipa kiingilio alafu upewi ticket wanakupa kikaratasi kama cha kwenye daladala then wanakulazimisha kukupiga muhuri kama tupo disco vumbi. Pale kuna uhuni mkubwa sana wa kukwwpa kodi.

Ata hivyo ile club naona kama imeishiwa pumzi maana ukikaa mule zaid ya lisaa we mwanaume kweli sound mbovu inakatakata full mabumashi.

Ilo la kodi TRA mkatumbue jipu la bills au ifungwe kwanza ile ni open space ikibidi lipelekwe bulldozer.
 
Ijumaa tarehe 26.11.2015 rafiki yangu alifika Billcanas Club kwa ajiri ya kujifurahisha ambapo Club hiyo ilikuwa inazinduliwa upya baada ya kufunga mitambo mipya.

Alipofika mlangoni, alilipa kiingilio cha shs 10,000. Akaomba risiti ya malipo lakini hakupatiwa. Akasisitiza na kuambiwa hapa hakuna risiti. Risiti ni haki ya mlipaji. Risiti uonesha serikali inapata kodi kiasi gani kutokana na tozo. Naomba ukumbi huu na kumbi zote zianze kutoa risiti mara moja la sivyo TRA iwafungie.

Ukumbi unaobeba watu 2000. wakilipa 10,000. ni sawa na 20,000,000. Ni pesa nyingi zinapotea, hapo bado vinywaji ninauzwa bei ya juu sana ndani bila risiti yeyote. TRA chunguzeni hizi sekta za burudani, taifa linapoteza mapato humo.

Wewe jamaa ni mshamba sana kama kitu haujui ni vema ungekaa kimya na kuficha ujinga wako.
1. Huo ni ukumbi na ni wazi kuwa umesajiliwa na mapato yanalipwa kwa biashara ya ukumbi sasa wewe unataka malipo yepi zaidi? ni wazi katika kumbi za burudani kinachotolewa huwa ni tiketi na sio lisiti kwa ujinga huu wa mawazo yako inamaanisha hata kwenye uwanja wa Taifa watu wakienda kuangalia mpira eti wapewe Lisiti na sio Tiketi acha ushamba ndugu.

2. Kuhusu vinywaji ni wazi kuna leseni ya vileo ambayo ulipiwa pia mapato yake TRA na leseni ya biashara hiyo
 
Huyo rafiki yako wakati analipa, wewe hakukulipia nini?
 
Back
Top Bottom