Bilioni 50 zinazodaiwa kurudishwa BOT kumbe changa la macho

Zee la shamba

Member
Oct 17, 2007
55
3
Yule mwanasiasa aliyeibua hadharani sakata la ufisadi ndani ya Benki Kuu ya Tanzania, BoT, Dokta Wilbroad Slaa leo ameibuka na mapya kwa kudai kuwa, eti zile Bilioni 50 kati ya 133 zilizoibwa, ambazo Serikali ilidai kuwa zimerejeshwa, ni changa la macho.

Akizungumza na Alasiri leo asubuhi, Dk. Slaa amedai kuwa licha ya Tume iliyoundwa kufuatilia suala hilo kutangaza kuwa Bilioni 50 kati ya bilioni 133 zinazodaiwa kuibwa zimerejeshwa, amepata taarifa nyeti na za uhakika kwamba pesa hizo hazijarudi.


Dk. Slaa ambaye pia ni Mbunge wa Karatu kupitia chama cha upinzani cha Chadema, amedai kuwa kilichofanyika ni kwamba hao wanaodaiwa kukwapua mapesa hayo, walikwenda mbele ya Tume hiyo wakiwa na wanasheria wao na kisha kuingia mkataba wa kurejesha pesa hizo taratibu.


``Nimefuatilia na kubaini kuwa hakuna pesa wanazorejesha kwa sasa, isipokuwa wanakwenda na wanasheria wao na kuingia mkataba wa kurejesha pesa walizochota kidogo kidogo,`` akadai Dk. Slaa.


Ameongeza kuwa suala hilo limemshangaza sana kwani kwa kufanya hivyo ni sawa na wizi kubadilishwa na kuwa deni.


``Mtu wa chini akifanya kosa anahojiwa na kuchukuliwa hatua haraka sana, lakini hawa wameiba mapesa yote hayo na ushahidi upo, lakini wanabadilishiwa kosa la wizi kuwa deni,`` akadai Dk. Slaa


Amesema ingawa hakuna mlango hata mmoja wa BoT uliovunjwa wakati wa wizi wa fedha hizo, lakini ushahidi wa hundi za kuchukua fedha hizo upo na hivyo kitendo hicho hakiwezi kuachwa kuitwa kuwa ni cha jinai.


SOUCE: Gazeti Alasiri
 
Kama ndivyo sheria zetu zilivyo, wale vijana wetu vibaka wa kuku, mayai, karanga nk walioko mahabusu na vifungoni watubu kwa mabwana magereza mbele ya wanasheria wakujitolea na kisha waachiwe huru. maana hawa wliiba kwa ajili ya njaa inayotokana na mifumo mibaya ya kiuchumi, iweje hawa walio husika ukwapuzi wa pesa BOT wawe treated in a special way.
 
Duh! Kweli tuna Siri kali ya wasanii!

Wamedai wameshapokea shilingi 50 bilioni na wanategemea kupata 80% ya shilingi 133 billioni. Tukawaomba majina ya waliokwisharudisha na kiasi walichorudisha, bank account number zilizowekwa pesa hizi na jina la bank hiyo, ili third party yeyote aweze kuhakiki ukweli wa madai ya siri kali kwamba imeshakusanya shilingi 50 bilioni.

Pia tuliwaomba tujue kama zimelipwa kwa cash, money order, cheque au bank to bank transfer. Wakaamua kufanya usanii wao kwa kukaa kimya kama hawaelewi tunachowauliza. Kumbe hawajapokea chochote kutoka kwa mafisadi na bado wako mjini wanapeta na mapesa yao waliokwapua kupitia ufisadi!

Mwe! unatamani kuangusha kilio kwa jinsi mafisadi walivyoiteka nchi
 
Duh! Kweli tuna Siri kali ya wasanii!

Wamedai wameshapokea shilingi 50 bilioni na wanategemea kupata 80% ya shilingi 133 billioni. Tukawaomba majina ya waliokwisharudisha na kiasi walichorudisha, bank account number zilizowekwa pesa hizi na jina la bank hiyo, ili third party yeyote aweze kuhakiki ukweli wa madai ya siri kali kwamba imeshakusanya shilingi 50 bilioni.

Pia tuliwaomba tujue kama zimelipwa kwa cash, money order, cheque au bank to bank transfer. Wakaamua kufanya usanii wao kwa kukaa kimya kama hawaelewi tunachowauliza. Kumbe hawajapokea chochote kutoka kwa mafisadi na bado wako mjini wanapeta na mapesa yao waliokwapua kupitia ufisadi!

Mwe! unatamani kuangusha kilio kwa jinsi mafisadi walivyoiteka nchi

Hapa atakuja mjinga ataanza kudai Oh wapinzani na mabomu sasa kama Nchi haiendi wafanyeje ?Lazima kunyoosha huko then kwenye Nchi yenyewe yaani ku ain kutwaa madaraka ya Nchi . Asante sana Slaa japokuwa Watanzania hawako tayari kuwaunga mkono nyie wapinzai mpate viti kibao Bungeni , nie ninawakubali ni kwamba sina uwezo tu ningaliweza kuzunguka Nchi nzima kuwaombea kura .
 
Pamoja na kuwa wengi tunapenda majibu juu ya hii saga haraka sana, hatuwezi afford kuloose hope hivyo basi matumaini yangu ni kuwa kama mlango wa kukubali deni ndio unaotumika, basi huo ndio mlango wa wahusika kukubali kilichotokea na kukubali ushirikiano wa kutoa taarifa ZOTE, halafu sasa huko mbeleni ni kufilisi mali ili kurecover PLUS kusekwa jela kwa mujibu wa sheria za nchi.

La ajabu ni kuwa je, akiwa mwizi wa kuku anatuhumiwa na jirani yake, jee vyombo vya dola vingechukua hatua za aina gani?

Kweli kuna viini macho na inagefaa tueleweshwe kama wadau wa nchi yetu.
 
sasa tunaitaka serikali iwatoe ndugu zetu wote walioshikwa kuiba kuku ama makosa madogo yote kwa makubaliano ya wazazi nfugu na viongozi wa mtaa na masheha maana kesi zao hazihitaji waendelee kuhudumiwa na kopdi zetu huko na wakati wezi wakubwa na wahalifu wa uchumi wetu wamebagain hili ndilo liwe agenda ya maandamano tunayopaswa kuyapanga sasa jamani semeni hili safari hii tuoneshe dunia kuwa tumechoka sasa kuandika bila matendo ni bure wanatuchezea tu ndio maana wanafunga forum yetu kwa uoga wetu.
niko tayari kutoa namba za simu ili tuanze rally yetu.
 
Miaka michache iliyopita mwanamuziki Jhiko Manyika alihojiwa na Jenerali Ulimwengu kwenye "Jenerali on Monday" kuhusu muziki wake.Katika albamu yake Safari kulikuwa na wimbo mmoja unaitwa "Mwache aende" alikuwa anaongelea vibaka wanavyouawa kwa kuiba kuku huku vigogo wanaachiwa waibe mabilioni.

Ndiyo haya sasa.Kwani hela zilichukuliwa katika mazingira gani na kwa nini mkondo wa sheria usifuatwe?
 
Mhhh, Hali hii kwa kweli inakatisha tamaa kabisa.

Maana kwanza kabisa it's been established kwamba hawa watu waliiba au walijichukulia pesa hizo kinyume na sheria. Sasa BoT na/au serikali kuingia kwenye "payment plan" na hawa wezi maana yake ni nini? Kwamba walichokifanya hawa wezi ni kusahau kwamba hizi pesa ni za watanzania, au walikopeshwa or what? Na kama hizo pesa hazirudishwi au hazijarudishwa ndiyo serikali inafanya nini sasa?

Credibility ya serikali yetu inazidi kushuka chini na inatia hata kichefuchefu kusikia mambo kama haya kwa kweli. Hivi hii serikali inadhani sisi watanzania ni vipofu, au ni mabubu? Madhambi mengi yanafichuliwa waziwazi lakini hii serikali aidha inayaachia, inayafunika/kuyaficha au kuyapuuza! Inatia uchungu sana. Mimi naona tuishitaki serikali kwa mambo yanayofanyika!
 
Mhhh, Hali hii kwa kweli inakatisha tamaa kabisa.

Maana kwanza kabisa it's been established kwamba hawa watu waliiba au walijichukulia pesa hizo kinyume na sheria. Sasa BoT na/au serikali kuingia kwenye "payment plan" na hawa wezi maana yake ni nini? Kwamba walichokifanya hawa wezi ni kusahau kwamba hizi pesa ni za watanzania, au walikopeshwa or what? Na kama hizo pesa hazirudishwi au hazijarudishwa ndiyo serikali inafanya nini sasa?

Credibility ya serikali yetu inazidi kushuka chini na inatia hata kichefuchefu kusikia mambo kama haya kwa kweli. Hivi hii serikali inadhani sisi watanzania ni vipofu, au ni mabubu? Madhambi mengi yanafichuliwa waziwazi lakini hii serikali aidha inayaachia, inayafunika/kuyaficha au kuyapuuza! Inatia uchungu sana. Mimi naona tuishitaki serikali kwa mambo yanayofanyika!


Jamani JK anachapa kazi au hujawahi kumsikia KadaMpinzani na ndugu yake Dar salaam ?Ndiyo kasi na utendaji .Pesa zile wamegawana hawa hawa sasa wanaweza kumtaja nani ?
 
Some of these things can only happen in Bongo, but why then??????????? Hii ni laana nini??
 
Miaka mingi nyuma tulikuwa tunashangaa kwa nini majeshi yalikuwa yanaondoa utawala wa kiraia kwa nguvu. Sasa hivi nimekwisha kuelewa ni kwa nini hali hiyo ilikuwa inajitokeza kwa baadhi ya nchi.Hata hivyo niishie hapo,maana kuna watu watanitafsiri kuwa nina mawazo ya kihaini.
 
Miaka mingi nyuma tulikuwa tunashangaa kwa nini majeshi yalikuwa yanaondoa utawala wa kiraia kwa nguvu. Sasa hivi nimekwisha kuelewa ni kwa nini hali hiyo ilikuwa inajitokeza kwa baadhi ya nchi.Hata hivyo niishie hapo,maana kuna watu watanitafsiri kuwa nina mawazo ya kihaini.

Siku hizi wanawamegea, kwa hiyo hawana tena mawazo hayo na wazalendo jeshini hawako tena
 
changa la macho kama hili linaweza kutokea TZ kwa sababu SERIKALI= WEZI WA BOT kwa namna 1 au ingine!
Uuwii!Nasikia kulia!
Hivi TZ hamna "Civil Action"? Yaani kesi ya wananchi vs So & So?
Mungu ibariki Tanzania
 
Siku hizi wanawamegea, kwa hiyo hawana tena mawazo hayo na wazalendo jeshini hawako tena

Ungejua jinsi wanavyoteseka wala usingesema!!! Hawana uwezo kwa vile kule ndo kwenye ufisadi zaidi. Wale wazalendo na wanajeshi wenye akili wote wamecha jeshi na nani unaona siku hizi anajiunga zaidi ya wale wanaokosa ajira sehemu nyingine. Waliopo anaona wapo kwa favour tu ndo maana wamekaa hawaongei. wanasubiri wakatiwe maji wakapige utafikiri jeshi la 1907 linaloamini kila kitu ni nguvu na vitisho.
 
Ni kweli tuna Wanasiasa wanao vaa nguo za jeshi, hatuna jeshi. Kama jeshi litatwaa madaraka kwa nguvu watwaaji watakuwa ni Masajenti na makoplo hawa wengine hawawezi dhubutu.
 
these things r possible because Mafisadi= Serikali! Hivi TZ kesi ya wananchi dhidi ya so & so haiwezekani? Yaani CIVIL ACTION?
Tuliombee Taifa letu!
 
Huko Jeshini wanaogopana kupita kiasi maana usalama wa taifa wamewaingilia kwenye kila kona. Ndio maana ma-Sajent wameamua kuwa majambazi wa kutumia silaha na hawana mpango na mapinduzi kama wale waliomtishia Nyerere.

Kama Lowassa alikuwa hana hata nyumba mwaka 1990 alipopewa ukurugenzi wa AICC, lakini leo 2008 anauwezo wa kukodisha ndege hadi Monduli, ingawa muda wote huo alikuwa ni civil servant tu mshahara na marupurupu yake yote yanajulikana, kwa nini masajenti nao wasivunje mabenki na bunduki zao? Kwani wao hawataki watoto wao wakasoma ulaya au wao angalau kuendesha mtumba?

Tunakoelekea sio pazuri unless mabadiliko makubwa ndani ya CCM yatokee. Inatakiwa aingie mtu asiyejuana kabisaa na wanamtandao na wapambe wao ili aanze upya na hata ikibidi kuwaadhibu baadhi yao. Lakini hii sio rahisi kwa 2010 au hata 2015 maana sidhani kama umaarufu na nguvu za JK vitakuwa vimesinyaa ndani ya CCM. Lakini nikiiangalia nchi yangu baada ya 2010, inabidi nitumie taulo kufutia machozi maana handikachifu yangu itakuwa imeloa chapa. Nyerere alisema, mapinduzi ya kweli yatatokea ndani ya CCM na kwa kiasi fulani naamini huu msemo wake, tatizo ni kuwa ni lini yatatokea au mpaka tutakapochinjana?

Kama wapinzani wangefanikiwa kutwaa nchi ingekuwa bora zaidi maana nafikiri bunge pia nalo lingekuwa na mgawanyiko mzuri zaidi. Lakini bado zijaona dalili za wao kuchukua nchi hasa baada ya kushindwa uchaguzi hivi karibuni. Kwa kweli inatubidi tumuombe mwenyezi Mungu kwa sana ili kikombe hiki kitupite.

Ibarikiwe Tanzania........ Inshalah.
 
Miaka mingi nyuma tulikuwa tunashangaa kwa nini majeshi yalikuwa yanaondoa utawala wa kiraia kwa nguvu. Sasa hivi nimekwisha kuelewa ni kwa nini hali hiyo ilikuwa inajitokeza kwa baadhi ya nchi.Hata hivyo niishie hapo,maana kuna watu watanitafsiri kuwa nina mawazo ya kihaini.

Uko sahihi mkuu!
Hao wanaopindua sirikali zao wala si wa kuwalaumu sana sometimes.
Huenda walikuwa washachoka na upumbavu kama huu unaoendelea sasa katika sakata zima hili, kiasi kwamba wakaamua kwamba sasa liwalo na liwe, hawana cha kupoteza.
 
Back
Top Bottom