Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,192
- 1,976
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
UKUMBI mpya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, unaotumika kwa shughuli za Bunge utavunjwa na kusukwa upya ili kuruhusu utengenezaji wa viti vya kisasa vitakavyofungwa vifaa maalumu vya mawasiliano ya teknolojia ya kisasa.
Hatua hiyo pia itaongeza idadi ya viti kutoka 340 vya sasa hadi viti 360 ili kumudu idadi ya wabunge wanaotarajiwa kuongezeka katika Bunge lijalo.
Itakumbukwa jengo hilo ambalo ni la kwanza Afrika Mashariki na la tatu kwa Bara la Afrika, hadi kukamilika kwake liligharimu zaidi ya sh bilioni 30.9.
Hatua hiyo ilitangazwa jana na Spika wa Bunge, Samuel Sitta, wakati akitoa mwongozo wa kiti cha Spika, kutokana na hoja iliyoibuliwa na Mbunge wa Ukerewe, Gertrude Mongela, aliyehoji sababu za Bunge kutumia teknolojia ya zamani kuhesabu kura za ndiyo na hapana zilizopigwa kwa wabunge ili kuunga mkono au kupinga hotuba ya Bajeti ya Serikali ya mwaka 2010/2011.
Akifafanua muundo mpya wa Bunge, Spika Sitta alisema kila kiti cha mbunge kitakuwa na runinga pamoja na mawasilino ya kisasa ya kompyuta, ambayo yatamwezesha kuuliza swali na kupata majibu kutoka kwa waziri anayehusika bila kusimama wala kutumia vikaratasi.
"Kwanini tunatumia teknolojia ya zamani, jibu lake ni dogo tu, ni kwamba hili jengo viti vyake vitafumuliwa vyote na kusukwa upya na kazi hiyo itafanyika mara baada ya kuvujwa Bunge. Michoro ya kazi hiyo imeshakamilika na kazi hiyo imefanywa na Mbunge wa Hai, Fuya Kimbita (CCM), yeye na ujumbe wake wamekwenda kwenye mabunge ya Scotland na mabunge mengine kuangalia jinsi ya kulirekebisha Bunge letu liwe la kisasa zaidi," alisema Spika Sitta.
Kwa Habari Zaidi Soma Tanzania Daima
UKUMBI mpya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, unaotumika kwa shughuli za Bunge utavunjwa na kusukwa upya ili kuruhusu utengenezaji wa viti vya kisasa vitakavyofungwa vifaa maalumu vya mawasiliano ya teknolojia ya kisasa.
Hatua hiyo pia itaongeza idadi ya viti kutoka 340 vya sasa hadi viti 360 ili kumudu idadi ya wabunge wanaotarajiwa kuongezeka katika Bunge lijalo.
Itakumbukwa jengo hilo ambalo ni la kwanza Afrika Mashariki na la tatu kwa Bara la Afrika, hadi kukamilika kwake liligharimu zaidi ya sh bilioni 30.9.
Hatua hiyo ilitangazwa jana na Spika wa Bunge, Samuel Sitta, wakati akitoa mwongozo wa kiti cha Spika, kutokana na hoja iliyoibuliwa na Mbunge wa Ukerewe, Gertrude Mongela, aliyehoji sababu za Bunge kutumia teknolojia ya zamani kuhesabu kura za ndiyo na hapana zilizopigwa kwa wabunge ili kuunga mkono au kupinga hotuba ya Bajeti ya Serikali ya mwaka 2010/2011.
Akifafanua muundo mpya wa Bunge, Spika Sitta alisema kila kiti cha mbunge kitakuwa na runinga pamoja na mawasilino ya kisasa ya kompyuta, ambayo yatamwezesha kuuliza swali na kupata majibu kutoka kwa waziri anayehusika bila kusimama wala kutumia vikaratasi.
"Kwanini tunatumia teknolojia ya zamani, jibu lake ni dogo tu, ni kwamba hili jengo viti vyake vitafumuliwa vyote na kusukwa upya na kazi hiyo itafanyika mara baada ya kuvujwa Bunge. Michoro ya kazi hiyo imeshakamilika na kazi hiyo imefanywa na Mbunge wa Hai, Fuya Kimbita (CCM), yeye na ujumbe wake wamekwenda kwenye mabunge ya Scotland na mabunge mengine kuangalia jinsi ya kulirekebisha Bunge letu liwe la kisasa zaidi," alisema Spika Sitta.
Kwa Habari Zaidi Soma Tanzania Daima