Kingsmann
JF-Expert Member
- Oct 4, 2018
- 4,448
- 16,312
Huu ni ushauri tu, tena ambao unatakiwa upewe priority kubwa kuliko chochote kile.
Kwa sasa ukienda hospitali yoyote first impression wanayokujengea ni kwamba una COVID19. Na kwa bahati mbaya sana wale wenye chronic conditions kama kisukari, ugonjwa wa moyo, ugonjwa wa ini, hypertension wanapresent na dalili kuu ya COVID19 ambayo ni kupumua kwa shida.
Sasa ukifika hospitali yoyote na ukaonekana una shida ya kupumua obviously watahitaji kujiridhisha kwanza kama una COVID19 ama laah.
Kwa hali hii Rapid test kits zinatakiwa ziwepo kila hospitali/kituo cha afya/dispensari. Hizi zinaondoa chaos zote zinazoendelea kwa sasa za wagonjwa kuzungushwa huku na huko hasa jiji la Dar.
Jijini Dar malalamiko ya wagonjwa kukataliwa hospitali yamekuwa mengi na mpaka wengine wanafia njiani ama nyumbani. Mbaya zaidi wakifa serikali inazuia mwili wajiridhishe kama ni COVID19 ama sio ndipo mruhusiwe kuendelea na mazishi. Wakikuta ni COVID19 serikali inahusika na mazishi.
Kwa rate ya maambukizi ilivyo sasa haiwezekani kuendelea kutegemea PCR ambayo mchakato wake wa kupata majibu ni mrefu. Kwa wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa haraka wanakufa hata kabla ya hayo majibu kutoka. Na huwezi kuwalaumu wafanyakazi wa afya kwa sababu kwenye milipuko ya magonjwa kama haya wanatakiwa wajiridhishe kwanza ili wajue wanajilinda vipi.
Serikali leteni rapid tests, hizi haziepukiki. Kuweni proactive ili kudhibiti huyu mdudu kuenea. Kwa nini mko nyuma sana kwenye kuchukua hatua stahiki. Sababu mnaweza kujifanya hamnunui hizo kits sasa lakini mwisho wa siku mtakuja kununua tu.
Kwa sasa ukienda hospitali yoyote first impression wanayokujengea ni kwamba una COVID19. Na kwa bahati mbaya sana wale wenye chronic conditions kama kisukari, ugonjwa wa moyo, ugonjwa wa ini, hypertension wanapresent na dalili kuu ya COVID19 ambayo ni kupumua kwa shida.
Sasa ukifika hospitali yoyote na ukaonekana una shida ya kupumua obviously watahitaji kujiridhisha kwanza kama una COVID19 ama laah.
Kwa hali hii Rapid test kits zinatakiwa ziwepo kila hospitali/kituo cha afya/dispensari. Hizi zinaondoa chaos zote zinazoendelea kwa sasa za wagonjwa kuzungushwa huku na huko hasa jiji la Dar.
Jijini Dar malalamiko ya wagonjwa kukataliwa hospitali yamekuwa mengi na mpaka wengine wanafia njiani ama nyumbani. Mbaya zaidi wakifa serikali inazuia mwili wajiridhishe kama ni COVID19 ama sio ndipo mruhusiwe kuendelea na mazishi. Wakikuta ni COVID19 serikali inahusika na mazishi.
Kwa rate ya maambukizi ilivyo sasa haiwezekani kuendelea kutegemea PCR ambayo mchakato wake wa kupata majibu ni mrefu. Kwa wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa haraka wanakufa hata kabla ya hayo majibu kutoka. Na huwezi kuwalaumu wafanyakazi wa afya kwa sababu kwenye milipuko ya magonjwa kama haya wanatakiwa wajiridhishe kwanza ili wajue wanajilinda vipi.
Serikali leteni rapid tests, hizi haziepukiki. Kuweni proactive ili kudhibiti huyu mdudu kuenea. Kwa nini mko nyuma sana kwenye kuchukua hatua stahiki. Sababu mnaweza kujifanya hamnunui hizo kits sasa lakini mwisho wa siku mtakuja kununua tu.