Kweli wanawake wanajua kushikilia akili za wanaume mshkaji wangu an girlfrind wake wa miaka miwili kaambiwa ukweli na mchumba wake bila kununua gari a kutembelea ndoa hakua harusi kikao cha pili. mshkaji anahaha kukichangisha hadi m9 ifike. wadada mbona mnatuanyia hivo lakini?
Jamaa ndio anatemwa kiana. Lazima kuna mtu mwingine kampa hiyo ahadi ya gari. Jamaa atulize kichwa aachane na huyo mwenye masharti magumu. Hivi huyo binti baba yake ana gari? Tu assume analo, je wakati baba yake anaoa alikuwa na gari?
Raha ya mali mchume wote!
Kashikiwa bunduki?
huyo rafiki ako ni boya, amwambie basi hana uwezo aone binti atakavohaha hapo
nanyie wanaume wa siku hizi sijui mkoje ndo maana mnapelekeshwa
Nimekupendaje Evelyn Salt!!
Sasa hapo ni uchumba tu fikiria atakapomuoa atapelekeshwa kama mbio za mwenge
Nakupenda pia....ila we ni me au ke?
hili jibu langu lisijeleta madhara
eve hawa watu bila kuwa bandidu mambo hayaendi bana, so big up mdada kaza buti tena akinunua mwambie bila kujenga nyumba mtoto hazaliwi.
Meeeee
:hug:
Eeeeh haya tena nimejiingiza mkenge, okay poa...Meeeee
:hug:
ahaaa ukinipa condition kama hii katika ndoa, utajikomoa mwenyewe sijengi mpaka ufikishe 40, tuone nani ataingia menopause
mawazo kama haya hapo red ndio yanayofanya watu wa afrika tuwe masikini tu. tunaweka investments si kwa ajili yetu tu, bali na kwa vizazi vyetu vijavyo, angalia kina bush wananua uranium wanajua vijukuu vyao vitakuja kutumia....Ingekuwa hivyo ndoa zisingefungwa na watoto wasingezaliwa,tulikuja watupu na tutaondoka watupu,mali ni matokeo kuna jamii nyingi na familia hazina mali(magari ,majumba ) na maisha yanaenda tena vizuri kwa amani
Kwanni vitu vya kupita visivyo na guarantee viwe attached na life commitment? Haya suppose hilo gari la 9m limenunuliwa na kwa kuwa bwana harusi pesa yote imeishi kwenye gari na gharama za harusi hivyo bima aliyokata ni third part. Wakiwa honey moon Bagamoyo gari limeungua completely vipi shosti atadai talaka?
Bobby hivi unaamini kwamba bibi harusi anaweza kuleta condition kama hiyo wakati harusi ipo katika kikao cha pili? mi siamini bana
Mijinaume mingine inatuzalilisha tu