Kwa wale wanaochukulia mambo juujuu bila kuchambua kwa kina hawawezi kunielewa. Ni ukweli kwamba CCM ina wafuasi sana katika mikoa fulani hasa ya tambarare na Pwani na pia Unguja. Mikoa kama Lindi, Mtwara, dodoma vijijini, tanga, unguja nk ni vigumu sana chadema kushinda huko. Lakini pia maeneo haya ndio CUF ina wafuasi. Sasa ili chadema ishinde lazima CUF iwe na nguvu ili katika maeneo hayo wagawane na CCM angalao CUF 40% CCM 60%. Kupanuka kwa CUF si tishio kwa Chadema bali CCM hivyo kwa maoni yangu ni vizuri tuisaidie CUF irudishe hadhi yake ili wapambane na CCM katika maeneo ambayo ni no fly zone kwa chadema. Nimebahatika kutembelea baadhi ya maeneo haya na nilikuwa Tanga last week baadhi ya watu wanaiona Chadema kama chama cha wakristo na ni ngumu kuwabadili mawazo. CUF wanaweza kuwabadili tukapunguza mtaji wa ccm! Tutafakari