Brn ni mpango wenye mkakati ulengao kuboresha matokeo chanya kuhusu ufaulu kwa wanafunzi. Namna unavyotekelezwa wakuu wa shule walipewa maelekezo ya, mosi, kupanga ratiba ya muda wa jioni ambapo masomo manne yatahusika kufundishwa nayo ni math, geog, kisw na engl. Pili, walimu watashirikiana wote as a team work na kila kipindi kwa shule zenye mkondo mmoja atalipwa sh. Elfu tano hvy kwa mwezi utapaswa uandikiwe cheki ya malipo yako ya sh.elfu ishirini kama utakuwa umefundisha pekeyakona kama mpo wengi basi gawanya kiasi hicho kwa idadi yenu mtakaoshiriki kufundisha.kwa shule zenye mkondo zaidi ya moja watalipwa sh elfu kumi kwa mwezi unaandikiwa cheki yako ya sh. Arobaini elfu . Tatu, wakuu wa shule waliagizwa kusimamia kiukamilifu ratiba hz., ukaguzi wa documenti zote z taaluma na wahakikishe kuwa mada za kila somo zimefundishwa zote kabla ya mwezi wa kumi. Changamoto za mpango huu wa brn. Mosi, waalimu wengi ambao ndiyo watekelezaji wa mpango huu, bado wanamadai mengi ya malimbikizo ya mishahara achilia mbali nyongeza ya mishahara,posho za kufundishia, n.k pili, baadhiya shule zipo mbali na huduma za benki hvy nauli kutoka shule hadi benk kuchukua malipo hayo kwa njia ya cheki itakugharimu utumie si chini ya sh kumi na sita hiyo ni nauli tu ya kufuata malipo hayo ya sh elfu ishirini yaliyo kweye mfumo wa cheki na tayari waalimu wengi wanasagiziana kukwepa kadhia hiyo. Maoni yangu mosi, muda wa kutekeleza mpango huu n mdg sana pili, malipo madogo sn yaongezwe na shule zilizombali na benk waalimu walipwe kwenye vituo vyao. Tatu, madeni na kero zote za walm zitatuliwe. Je mpango huu utafanikiwa? Usiniulize sina jibu la moja kwa moja. Tusubiri tuone matokeo ya mwaka huu yatakuwaje?