hekimatele
JF-Expert Member
- May 31, 2011
- 9,884
- 2,781
Habari zenu wanajamii?
Kwa muda sasa miaka nenda miaka rudi kumekua na hii reality show inayoitwa Big Brother inayofanyika karibu kila mwaka katika nchi ya South Africa.
Swali ambalo limekua likinitatiza ni je, hii reality show ina manufaa gani hasa kwa mtu binafsi na hata jamii ya waafrika ituzungukayo? Kwa zaidi ya miaka mingi Afrika imekua na maadili yake yenyewe na tukiiangalia hii show kwa jinsi ilivyo hai reflect hata chembe ya maadili yetu wenyewe. Hii inaonesha jinsi itikadi na tamaduni yetu ilivyomezwa na tamaduni za kimagharibi.
Ni kweli show hii ina manufaa yoyote katika bara hili la Morikwa?
faida zipo tena nyingi,na moja moja ni hile hali ya kuitangaza nchi,hakuna anaelazimishwa kuonesha tamadun za magharib na ilimradi kuna nchi za africa tupu,ile ndo life ya hao watu katika hali halisi na kuwepo kwa globalization kamwe mwingiliano wa tamaduni hauepukiki,apart from that si lazima kila kitu kifundishe inabaki kuwa entertaiment kwa anaetaka,kwa hali ya kawaida nivipindi vingapi vya umuhim watu wanaskip?