Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,199
- 10,932
Hii leo muda mfupi kuanzia sasa malori 20 ya misaada yataanza kuvuka mpaka wa Misri na Gaza kupeleka misaada kwa Wapalestina waliozingirwa Gaza.
Misaada hiyo itakuwa ni ya mwanzo na aliyoitaja raisi Biden juzi kama ni makubaliano yake na Rais Elsisi wa Misri. Jana viongozi wa Hamas waliachia mateka 2 wa Marekani ikionekana kama ndiyo makubaliano hayo ya Biden na Elsisi.
Hata hivyo imeelezwa malori 20 ni kama asilimia moja tu ya mahitaji ya Wapalestina milioni mbili laki tatu kwa kila siku. Kikawaida mpaka huo huwa unapitisha malori 60 kwa siku.
Malori hayo 20 yanakuja baada ya takriban siku 10 za kutoingia chochote nchini humo kutokea popote na wakati mahitaji yameongezeka zaidi kutokana na kuongezeka madhara ya vita.
Misaada hiyo itakuwa ni ya mwanzo na aliyoitaja raisi Biden juzi kama ni makubaliano yake na Rais Elsisi wa Misri. Jana viongozi wa Hamas waliachia mateka 2 wa Marekani ikionekana kama ndiyo makubaliano hayo ya Biden na Elsisi.
Hata hivyo imeelezwa malori 20 ni kama asilimia moja tu ya mahitaji ya Wapalestina milioni mbili laki tatu kwa kila siku. Kikawaida mpaka huo huwa unapitisha malori 60 kwa siku.
Malori hayo 20 yanakuja baada ya takriban siku 10 za kutoingia chochote nchini humo kutokea popote na wakati mahitaji yameongezeka zaidi kutokana na kuongezeka madhara ya vita.