Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 71,270
- 105,468
Mbona nimejibu kirefu katika ulichokinukuu?mbona unakwepa hili swali ambalo hata mimi nilikuuliza? Mungu ninani? ukiweza kujibu hilo tu na hayo mengine yanajijibu yenyewe.
Unajua kusoma?
Soma tena hapa.
Mungu ni wazo lililo katika vichwa vya baadhi ya watu, ambalo halina uhalisi zaidi ya kuwa wazo tu.
Wazo hili halina uhalisia(zaidi ya kuwa wazo tu) kwa sababu lina contradictions zisizotatulika, kuanzia ngazi ya wazo tu, na hivyo haliwezi kuwapo katika uhalisi.
Contradiction kubwa ni ukweli kwamba, Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, kaumbaje ulimwengu unaoruhusu mabaya mengi, wakati alikuwa ana uwezo, ujuzi na upendo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya siyo tu hayawezekani kufanyika, bali pia hayawezekani hata kufikirika kwa sababu hayapo kabisa?
Mungu huyu ni sawa na wazo la "Pembetatu yenye pembe nne" katika Euclidean geometry planes.
Unaweza kuwaza wazo hilo.
Lakini ukweli kwamba unaweza kuwaza "pembetatu yenye pembe nne" haufanyi pembe tatu yenye pembe nne iwepo kwenye uhalisia.