Biblia kwa Jicho Jingine

Naomba kwa mwenye kujua jinsi ya kupata post hii "Biblia kwa jicho jingine" umeandikwa na jamaa anayejiita Bilionea ......anisaidie tafadhali
 
Uliyoyaandika yanafikirisha, pia binafsi yanathibitisha msimamo wangu kuwa kuna taarifa nyingi sana na uelewa mpana sana zaidi ya tafsiri nyingi za moja kwa moja za biblia kuhusu Mungu, uumbaji n.k.

Mungu ni mpana sana, Mungu haeleweki, akili za mwanadamu haziwezi kupata maana ya moja kwa moja kuhusu Mungu...

Kama ilivyoongelewa...tunajaribu kumuelezea Mungu kwa hulka za kibinadamu, tunamuweka katika sifa za kibanadamu, tunashindwa kutambua kuwa kuna viumbe vingine vingi (vinavyoonekana na visivyoonekana) ambavyo navyo vinampa Mungu sifa kwa namna vilivyoumbwa...

Itoshe kusema tu....uumbaji wote wa Mungu...hasahasa kwa kiumbe chake (mwanadamu)...amekipa bahati ya kipekee kuishi katika ulimwengu wa aina mbili: Ulimwengu wa nyama, ulimwengu wa kiroho...Mapenzi ya Mungu kwa binadamu ni zaidi ya upendo wa baba kwa mtoto....Mungu anatuwazia mema daima....Hata hofu ya kufa tunajiwekea wanadamu, kufa ni transtion ya kwenda kwenye utakatifu wa kwenda kwenye uwepo wa Mungu....na hata moto haupo, kumbuka roho zetu zina mission moja tu..kurudi zilikotoka...zirudi zinapopaswa kuwa, zirudi kwenye source yake....tumeshare roho (uwezo wa Kimungu) kupitia pumzi ya Mungu..hivyo mateso ya roho kuzuiliwa kurudi sehemu yake kutokana na mapungufu ndo Moto mwenyewe..

Asante mtoa mada...ubarikiwe huko uliko...Mungu yupo
Asante sana ndugu umezidi kunidhibitishia kauli ya kiongozi mmoja wa dini aliwahi kuniambia kwamba hakuna jehanamu wala hakuna pepo au mbingu kama tunavyo aminishwa.
Kwamba kuna mahali ambapo ni motoni au mbingu ni hakuna.

Kama ulivyo sema kwamba roho inapambana kurudi kwenye asili yake, adhabu kubwa kabisa ambayo itapata roho iliyokua ovu ni kutokumuona Mungu milele.
Kwa asili ya roho kutokuonana na Mungu ni adhabu kubwa sana , na hilo ndio litakalowapata watu wote na vyote vilivyo viovu na si kuchomwa moto kama inavyo semekana.

Na huo pepo au mbingu sio sehemu ya kuimba na kusifu wala sehemu ya kula raha na starehe za kibinadamu bali ni ile hali ya roho kukutana na Mungu.

Hivyo vya kupewa pepo ya daraja la kwanza au la mwisho au kuchomwa moto ni imagenetion ya kibinadamu tu.
 
Unachokisema ni kweli kabisa mkuu.

Hata Malaika wanayeishi na Mungu huko juu hawamuelewi huyu Mungu ni nani.
Katika kozi ambazo haziishi mbinguni ni kozi inayoitwa "Kumuelewa Mungu".

Hii ni kozi inayosomwa milele na milele na milele yote na kila kiumbe alichokiumba Mungu, si Malaika wala si wanadamu wala si kiumbe chochote cha kiroo kinaweza ku-graduate katika kozi hii.

Huko mbele nitaelezea concept moja makini sana ambayo kwa kifupi ni kuwa Mungu hujifunua kwa kila kiumbe chake kwa Level ya kiroho waliyo nao hao viumbe wake kwa kuwa yeye ni mkuu mno huwezi kumuelewa akija kama alivyo.

Na ni kweli kuwa Mungu ana mfumo wa utawala kama ulioko huku duniani, lakini yuko accessible kwa kila kiumbe chake, hakuna protocol ngumu ya kumuona kama ilivyo huku duniani, ila angalizo ni moja tu kuwa Mungu huyo unayemuona wewe si Mungu yule anayemuona Serafi au Kerubi, ndio maana wenye uhai wanne wale husihi tu kuimba mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu milele yote.

Si kwa sababu wanapenda kumsifu sana ila ni kwa sababu Kila siku wanamuona katika version mpya ambayo walikuwa hawajawahi kuiona, na katika hili kazi yao kuu ni kuitaja sifa kuu waiyoiona kwa wakati huo.
Na kwa kuwa daima anapanda katika viwango kwao kulingana na ufahamu wao, wao huishia tu kusema Mtakatifu Mtakatifu Mtakatifu maana hata wao wanashindwa kumuelewa.

Kwa hiyo ukienda Mbinguni leo ukataka kuonana na Mungu utapelekwa moja kwa moja na utakaa karibu naye kabisa, ila perception yako kwake italingana na uwezo wako wa ku conceive mambo ya Kiroho kwani wakati unadhani unamfahamu kumbe hata bado hujaanza kumfahamu.
zote hizi ni nadharia tu
 
Wewe hujui tofauti ya kudhibitisha na kuthibitisha halafu unaniita mimi si "mwelewa".

Kiswahiki tu kinakupiga chenga. Halafu unanikashifu mimi ninayeona makosa yako kuwa si muelewa. Hata hiyo muelewa yenyewe hujui kuiandika.


Talk about the great unwashed and the tragedy of the commons.

Wapi nilikwambia nataka nithibitishiwe Mungu yupo kwa sababu simuoni (sic) physical?

Unaelewa unaweza kuangalia movie ya Bruce Lee ukumbini kwako, ukamuona Bruce Lee yupo ukumbini mwako anapiga watu, wakati Bruce Lee hayupo alishafariki miaka mingi sana?

Mungu hayupo kwa sababu yenye kina kirefu kuliko kumuona physically.

Mungu wenu mnayesema yupo, mjuzi wa yote, mwwnye uwezo wote na upendo wote, hayupo, kwa sababu, dhana ya kuwepo kwake ina cintradictiin.

At the conceptual level.

Ni kama mtu akwambie "kuna pembwetatu yenye pembe nne katika Euclidian pllanes".

Hiyo ni contradiction. Kitu hicho hakipo. Kinajioinga chenyewe.

Imekuwaje Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote aache kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani, aumbe ulimwengu ambao mabaya yanawezekana?

Hii ni contradiction sawa sawa na ile ya " pembetatu yenye pembe nne".

Sasa nikipinga uwezo wa Mungu jwa sababu ya cintradiction katika dhana ya kuwepo kwake, utasemaje napinga uwepo wa Mungu kwa sababu haonekani?

Wapi ninwpinga uwepo wa Mungu kwa sababu hainekani?

Unaelewa kwamba si kila kionekanacho kipo?

Unajua kusoma kwa ufahamu?
Kiranga nawe matope TU kichwani. Yaani Kwa mawazo Yako unafikiri unaweza mpangia Mungu namna ya kuendesha mambo ?

Nani alikuambia nikiwa na uwezo wa kujua utatenda Nini ndio iwe sababu ya kutokukuazibu ukitenda ? Mbona ujiulizi wewe unayetenda huo uovu wewe ujui kama ulitendalo ni uovu na una uamzi wa kutenda au kutokutenda. Hoja yako ni mfu coz unataka kuondoa uwajibikaji na utashi wa mwanadamu kwa lile alifanyalo. Shupaza shingo Yako na ukifa bila kutubu Chamoto utakiona .

Nani alikuambia coz nina upendo wote why nawachukua wapendwa wako ? This rediculous and pathetic ...toka lini una question upendo wa Mungu kwa kuondoa wapendwa wako. Nani ajuae wafu wanapokwenda wanapofariki? Unazani wana raha sana kuishi Dunia ya watu wabishi na jeuri kama wewe ! Nani ajuae hao wanaoachwa ndo Mungu anawapa fursa ya kulelelewa na watu watakaowasaidia zaidi? Process ya kutambua upendo wa Mungu sio lazima ueleweke kwenye fahamu zako. Njia za Mungu zipo juu ya jinsi unavyotafsiri wewe.

Contradiction ya kiuandishi sio quarantee ya contradiction of the reality. Ni kweli dini ni nyigi na Kuna details zinapishana ila mantic inabaki kuwa ileile . Dini zote zinajaribu kujibu chanzo Cha maisha ya hapa duniani ni kipi, mwanadamu ni nani, Nini kusudio la maisha yake, hatima ya mtu akifa ni nini etc, kufafanua maswali hayo Kuna dhana nyingi zinafafanuliwa ila life dynamics and it's manifestations it tells all...

Mungu ni wa kuaminiwa

Mungu ni wa kutumainiwa

Ukimwamini poa usipomwamini yeye anabaki kuwa wa kuaminiwa
 
Kiranga nawe matope TU kichwani. Yaani Kwa mawazo Yako unafikiri unaweza mpangia Mungu namna ya kuendesha mambo ?

Nani alikuambia nikiwa na uwezo wa kujua utatenda Nini ndio iwe sababu ya kutokukuazibu ukitenda ? Mbona ujiulizi wewe unayetenda huo uovu wewe ujui kama ulitendalo ni uovu na una uamzi wa kutenda au kutokutenda. Hoja yako ni mfu coz unataka kuondoa uwajibikaji na utashi wa mwanadamu kwa lile alifanyalo. Shupaza shingo Yako na ukifa bila kutubu Chamoto utakiona .

Nani alikuambia coz nina upendo wote why nawachukua wapendwa wako ? This rediculous and pathetic ...toka lini una question upendo wa Mungu kwa kuondoa wapendwa wako. Nani ajuae wafu wanapokwenda wanapofariki? Unazani wana raha sana kuishi Dunia ya watu wabishi na jeuri kama wewe ! Nani ajuae hao wanaoachwa ndo Mungu anawapa fursa ya kulelelewa na watu watakaowasaidia zaidi? Process ya kutambua upendo wa Mungu sio lazima ueleweke kwenye fahamu zako. Njia za Mungu zipo juu ya jinsi unavyotafsiri wewe.

Contradiction ya kiuandishi sio quarantee ya contradiction of the reality. Ni kweli dini ni nyigi na Kuna details zinapishana ila mantic inabaki kuwa ileile . Dini zote zinajaribu kujibu chanzo Cha maisha ya hapa duniani ni kipi, mwanadamu ni nani, Nini kusudio la maisha yake, hatima ya mtu akifa ni nini etc, kufafanua maswali hayo Kuna dhana nyingi zinafafanuliwa ila life dynamics and it's manifestations it tells all...

Mungu ni wa kuaminiwa

Mungu ni wa kutumainiwa

Ukimwamini poa usipomwamini yeye anabaki kuwa wa kuaminiwa
Hata kama mimi ni matope tu kichwani, hilo linaonesha Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Angekuwepo, asingeumba viumbe kama mimi walio matope tu kichwani.

Pia, huelewi tofauti ya logical consistency na kumpangia Mungu.

Ukisema wewe una urefu wa futi sita, nikataka tuhakiki kama kweli una futi sita, hapo sijakupangia uwe na futi sita, nahakiki kama dai lako lina ukweli. Nikiona hujafika futi sita na kusema wewe una urefu wa futi tano, ukinijibu nisikupangie uwe na futi sita, utakuwa huelewi kwamba mimi sijakupangia uwe na futi sita, nmehakiki maneno yako tu.

Zaidi, mimi siwezi kumpangia kitu Mungu, hilo ni kweli. Kwa sababu Mungu hayupo.

Nitampangiaje kitu Mungu ambaye hayupo?

Kama unabisha, thibitisha Mungu yupo.
 
Hata kama mimi ni matope tu kichwani, hilo linaonesha Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Angekuwepo, asingeumba viumbe kama mimi walio matope tu kichwani.

Pia, huelewi tofauti ya logical consistency na kumpangia Mungu.

Ukisema wewe una urefu wa futi sita, nikataka tuhakiki kama kweli una futi sita, hapo sijakupangia uwe na futi sita, nahakiki kama dai lako lina ukweli. Nikiona hujafika futi sita na kusema wewe una urefu wa futi tano, ukinijibu nisikupangie uwe na futi sita, utakuwa huelewi kwamba mimi sijakupangia uwe na futi sita, nmehakiki maneno yako tu.

Zaidi, mimi siwezi kumpangia kitu Mungu, hilo ni kweli. Kwa sababu Mungu hayupo.

Nitampangiaje kitu Mungu ambaye hayupo?

Kama unabisha, thibitisha Mungu yupo.
Mathayo 11:5
''vipofu wanapata kuona, viwete wanakwenda, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.''

Hatuwezi kuamini kwa kulazimishana ikiwa wewe umehubiriwa juu ya habari njema na wewe ukakataa nitakuwa Mjinga sana kama nikaendelea kukulazimisha,nitaacha Mungu ashughulike na wewe.

Tusisumbuane eti tuthibitishe uwepo wa Mungu kisayansi wakati kila siku tunaona matendo Yake.
 
Mathayo 11:5
''vipofu wanapata kuona, viwete wanakwenda, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.''

Hatuwezi kuamini kwa kulazimishana ikiwa wewe umehubiriwa juu ya habari njema na wewe ukakataa nitakuwa Mjinga sana kama nikaendelea kukulazimisha,nitaacha Mungu ashughulike na wewe.

Tusisumbuane eti tuthibitishe uwepo wa Mungu kisayansi wakati kila siku tunaona matendo Yake.
Unaji contradict.

Unanihubiria, halafu hapo hapo unasisitiza hatuwezi kulazimishana.

Mimi sitaki kuhubiriwa, tukianza mahubiri naweza kukushinda wewe kwa mahubiri.

Mimi nataka facts, proofs. Unaweza ku prove Mungu yupo?
 
Unaji contradict.

Unanihubiria, halafu hapo hapo unasisitiza hatuwezi kulazimishana.

Mimi sitaki kuhubiriwa, tukianza mahubiri naweza kukushinda wewe kwa mahubiri.

Mimi nataka facts, proofs. Unaweza ku prove Mungu yupo?
Hata kama utaweza kunizidi kuhubiri kwangu itakuwa furaha zaidi maana sisi hatufanyi hivyo kwa kutafuta utukufu wetu bali ni Kwa Utukufu wa Mungu.
 
Proof nyingne unayotaka ya nini na ikisaidie nini wakati una msimamo wako.Ishi maisha yako, na kama unataka proof msubiri atakuja kukupa yeye mwenyewe
 
Hata kama utaweza kunizidi kuhubiri kwangu itakuwa furaha zaidi maana sisi hatufanyi hivyo kwa kutafuta utukufu wetu bali ni Kwa Utukufu wa Mungu.
Huyo Mungu hayupo.

Habari ya kuwapo kwake ni hadithi tu ilitungwa na watu.

Ukibisha, thibitisha yupo.
 
Proof nyingne unayotaka ya nini na ikisaidie nini wakati una msimamo wako.Ishi maisha yako, na kama unataka proof msubiri atakuja kukupa yeye mwenyewe
Wewe unahubiri hapa. Unahubiri kitu ambacho huwezi kukithibitisha?

Unahubiri uongo siyo?
 
Nimeamua kuandika makala hii kwa heshima ya Jukwaa hili lakini pia kwa ajili ya kuchochea udadisi lengo likiwa kumpa kila asomaye uthubutu wa kutaka kufukiri nje ya Box.

Makala hii ni mjumuisho wa vitabu vingi vya kiroho kikubwa kikiwa Biblia, Simulizi za Kiyahudi, Vitabu vya Mafunuo ambavyo baadhi ya walioishi duniani walibahatika kuyapata kutoka wa Mungu mwenyewe lakini pia baadhi ya mawazo yangu ili kuweka mtoririko mzuri wa kimakala.

Makala hii huenda ikapingana na unachokiamini, lakini chanzo cha fikra mpya hujengwa katika tofauti ya kimitazamo, na hapo ndipo mwanadamu hukua kimawazo, kwa hiyo ukiona yaliyomo humu yanapingana na uelewa wako ni vema uachukulia tu kama masimulizi ya hadithi za kufikirika, maana lengo la uzi huu si kuchafua au kuvuruga imani ya mtu yeyote.


==========

Hapo mwanzo Mungu aliziumba Mbingu na nchi nayo nchi ilikuwa giza tena utupu.

SEHEMU YA KWANZA(UTANGULIZI)

Hapo zamani sana kabla ya mwanzo wa kila kitu alikuwepo Mungu pekee bila kiumbe chochote kile kilicho hai wala kilicho mfu, Mungu huyu kwa utashi wake kabisa na kwa mapenzi yake kabisa bila kushurutishwa na yeyote akaamua kujipanua kwa “kuuwekeza utu(uhai) wake” ndani ya vitu vingine ili tu kutimiza yale ambaye yeye aliyaona yanaifurahisha nafsi yake.

Mungu huyu aliamua kujigawa katika vipande vikubwa vitatu ambavyo vyote vilibeba Uungu wake kwa ukamilifu wa 100%, vipande ambavyo vingemuwezesha yeye kwanza kutekeleza tukio zito lililokuwa mbele yake, lakini pili kurahisisha kile ambacho anataka kwenda kukifanya kwa kuwa kwa vyovyote vile kwa hulka yake alitaka kuugawa uhai wake(kuusambaza) kwa viumbe vyake atakavyoviumba lakini pia kuwa navyo karibu kama familia moja.

Viumbe hivi kwa vyovyote vile visingeweza kumuelewa na wala haviwezi kumuelewa milele yeye ni nani, kifupi vinaelewa kile tu ambacho ameruhusu kieleweke kwao kwa wakati huo, pamoja na hilo bado hivyo alivyoviruhusu vieleweke vimekuwa “hekima nzito kweli kweli” , hekima ambayo imeviharibu viumbe hivyo vilivyoamua kuitumia vibaya uelewa mdogo waliopewa kuibeba si wa malaika wala wanadamu wala kwa viumbe vyote vya rohoni alivyoamua kuviumba.

Kwa msingi huu Mungu huyu akaamua kufanya kazi katika nafsi tatu, ya kwanza akaiita Mungu Baba(Mungu Mwenyezi), ya pili akaiita Neno(baadaye alivaa mwili ili aje duniani kama mwanadamu) na ya tatu Roho baadaye alikuja kufahamika kama Roho Mtakatifu huku duniani.

Kimsingi nafsi hizi tatu zina nguvu kubwa sana na imekuwa vigumu sana kwa viumbe vyote vya rohoni na vya mwilini kujua hasa tofauti yao ni ipi na nani ni nani , lakini majukumu yao yamegawanyika kiutendaji zaidi, huku nafsi hizi tatu zikibaki kubeba Uungu wao kwa 100%.

Kifupi unayedhani ni Mungu Baba saa nyingine unakuta siye yeye ila ni Neno, na unayedhani ni Neno sometimes siye yeye ila Roho na unayedhani ni Roho saa nyingine siye ila ni Mungu Mwenyezi mwenyewe kwa kuwa kila mmoja ni tofauti na mwenzake na wakati huo kila mmoja yumo ndani ya mwezake, wote hawa ni nafsi tatu tofauti kabisa zinazojitegemea lakini pia nafsi hizi tatu ni moja.

Mungu Mwenyezi huyu yeye akaamua kuchukua jukumu kama la msimamizi mkuu na Master Planner wa kila kitu kinachoendelea huko kwenye mbingu za juu sana, mbingu tunazozijua sisi na hapa duniani, ni kama Senior Planner na administrator wa kila kitu. Yeye ndiye mpangaji au designer, muandaa maono na senior Founder.

Neno yeye akachukua jukumu la kutekeleza maono yote yanayotoka kwa Mungu Mweyezi, yeye ndiye hasa fundi wa kutafsiri maono na mipango kutoka kwa kwa Mungu Mwenyezi na kuuingiza katika utekelezaji ili vyote vilivyopangwa kugeuka kuwa vitu tangible, lakini pia kunapotokea failure kama iliyotokea kwa Adam na mkewe bustanini Edeni, failure ambayo inatokana na design nzuri kabisa ya kukipa kila kiumbe chake uhuru wa kuishi maisha ya kuwa na utashi akichagua anachotaka na asichotaka bila kushurutishwa na yeyote basi Neno huja na kurekebisha kasoro hio kwa kufuata design kutoka kwa Mungu Mwenyezi.

Kifupi Neno huyu ndiye mwenye jukumu la kurekebisha kasoro hio na ndio maana maandiko yanasema “alichinjwa kabla ya kuwekwa misingi ya nchi kwa kosa la Adam na mkewe Hawa” Roho yeye akabeba jukumu la uwezeshaji, yeye ndiye supplier wa nguvu na uwezo na materials za kiroho kuhakikisha kuwa plan zote kutoka kwa Mungu Mwenyezi, na utekelezaji wake kutoka kwa Neno unafanya kazi kama ilivyopangwa.

Yeye ndiye mwenye jukumu hasa la kuhakikisha kila kitu kinakuwa maintained katika viwango vyake kama ambavyo Master Plan inavyosema, lakini yeye pia ndiye msimamizi mkuu wa Uungu katika viumbe vyote vilivyoumbwa na vitakavyoumbwa.

Kabla ya Neno kuja kuanza kazi yake, Roho huyu hutangulia kwanza na kuyaaandaa mazingira, na mara baada ya Neno kumaliza kazi zake kama mtekelezaji, Roho hukabidhiwa jukumu pia la kuiendeleza kazi iliyofanywa na Neno lakini pia kuhakikisha kuwa quality na standards zake zinafikia Master Plan kama ilivyopangwa na Mungu Mwenyezi.

Kumbuka hawa watatu ni wamoja na ni tofauti pia, wakati unadhani sasa yuko Neno anafanya kazi, kumbe siye ila ni Roho na wakati unadhani ni Roho anafanya kazi unakuta ni Mwenyezi mwenyewe na wakati unadhani ni Mwenyezi yuko kazini kumbe ni Roho au ni Neno yuko kazini. Biblia inasema Mungu[Jehova] kwa Neno lake[Neno] aliziumba mbingu na nchi na kwa Hekima yake[Roho] akazithibitisha(zikawa maintained).

Kazi ya uumbaji ilipoanza, Mungu Baba akaandaa Master Plan master, Plan hii ikaanza utekelezaji wake awamu kwa awamu kwa kadri alivyoona yeye kuwa inafaa kwa nyakati atakazoziweka yeye na kwa namna atakavyoamua yeye.

Umbaji huu uligawanyika katika vipande viwili (Spheres Mbili)
Uumbaji wa kwanza ulikuwa uumbaji wa viumbe vya Kiroho na uumbaji wa Pili ulikuwa uumbaji wa viumbe vya kimwili, pia Mungu akaamua kuweka baadhi ya viumbe vya kiroho na kimwili kusimamia kazi zake za uumbaji, kusimamia mifumo yake ya Kiuungu, kusimamia tabia na makuzi ya viumbe vya kiroho lakini pia akatoa wasaidizi chini ya kila aliyepewa jukumu la kusimamia.

Sphere za Kiroho
Katika uumbaji wa Sphere za Kiroho kuna spheres ndogo ndogo nyingi sana huenda zikawa mabilioni kwa sasa kwa uwa kazi ya uumbaji inaendelea na ni ya milele na milele.
Spheres hizi zina vipande vitatu,
• Kipande cha ndani kabisa
• Kipande cha katikati
• Kipande cha Nje

Kipande cha ndani kabisa ambacho wengi tunakifahamu kama Mbingu ya Mwenyezi Mungu, Mbingu hii ndipo mahali ambapo kiti cha enzi cha Mungu kipo na ndio hasa headquarter ya uumbaji wote maana ndiko ambako Mungu yupo.

Muundo wa kipande hiki au Mbingu hii umegawanyika pia katika sehemu kuu tatu.
1) Ya Kwanza ni sehemu ya Uungu inayoanza kwa Kiti cha Enzi cha Mungu kilicho upande wa Kaskazini wa Mbingu, kiti hiki kiko juu ya kila kitu kwa maana ya height na hakuna kitu kinachoruhusiwa kukaa nyuma yake, kiti hiki kimezungukwa na viumbe vinne vyenye uhai ambavyo vimejaa hekima na ukuu na utiisho wa ajabu kwa sababu ya kuwa karibu na Mungu muda wote na viumbe hivi vina act kama waangalizi wa kiti hiki lakini pia Uungu wa Mungu.

Mara baada ya kiti hiki cha Enzi kuna Sehemu ya Roho ambazo zinasimamia tabia kuu za Mungu ambazo ni 1) Amani , 2) Upendo, 3) Utukufu mkuu, 4)Nguvu , 5)Uzima, 6 )Hekima ,7) rehema. Baada ya hapo kuna uwazi mkubwa sana kama bahari ya kioo na mbele yake kuna wazee 24 ambao nao wako katika sehemu ya Uungu wa Mungu, hawa ni kama “baraza” la Umungu, kumi na wawili wakiwa mkono wa kuume wa Mungu na Kumi na wawili wakiwa mkono wa Kushoto wa Mungu.

2) Sehemu ya Pili ni sehemu ya ibada ya Uungu ambapo kuna madhabahu ya dhahabu ya kutoa uvumba, madhabahu hii iko pembei kidogo mara baada ya kutoka kwenye viti vya wazee 24. Hapa ndipo ambapo sala zote na dua zote na shukrani zote za wanadamu na viumbe vyote aivyoviumba Mungu hupelekwa na kufukizwa kama harufu ya manukato kwa Mungu, harufu hii kupelekwa moja kwa moja kwa Mungu mwenyewe kwenye kiti che enzi bila kiumbe yeyote kugusa maana hii ni haki ya Mungu pekee.

Katika sehemu hii ya pili pia mbele ya kiti cha enzi husimama malaika wakuu 7 wa Mungu ambao huutazama uso wa Mungu daima wakipokea amri za kutekeleza kulingana na jukumu la kila mmoja alilopangiwa, majukumu haya yanahusisha control ya galaxies zote ambazo zinakadiriwa kuwa zaidi ya Bilions, usimamizi wa Mifumo ya Uungu na utawala na majukumu mengineo kulingana na nyakati na ratiba ya Mungu. Sehemu hii ya pili pia ni sehemu ya kila kiumbe ambacho kinataka kuwa na audience na Mungu awe ni malaika au viumbe vya rohoni au Adam enzi hajaanguka au yeyote anayetaka kujihudhurisha mbele za Mungu hapa anaruhusiwa kusimama na kuonana na Mungu moja kwa moja bila urasimu wowote.

3) Sehemu ya tatu ni sehemu kama ”mji” au city center ambapo kuna shuguli mbali mbali zinaendelea za kiofisi lakini pia za kimakazi kwa baadhi ya viumbe ambavyo vimepata nafasi ya kuishi mbinguni moja kwa moja kulingana na level yao ya ukuaji wa kiroho. Hii ni sehemu iliyo busy sana na iliyo na “kelele nyingi” kila “mtu” akiwa na lake, ikiwa ni sehemu ya kuingia na kutoa na pilika pilika za kutosha kila mmoja akifanya lililompeleka makao makuu. Kuna idara nyingi sana katika eneo hili ikwemo idara ya sifa, idara ya uumbaji, idara ya vita, idara inayohusika na wanadamu, idara za hukumu na mipangilio mingine mingi.

Kama nilivyosema kuna makazi huko mbinguni ya viumbe alivyoviumba Mungu, haya si makazi ambayo Yesu aliyaahidi kwa wafuasi wake, na ni wenye Uungu tu waio na makazi mbinguni lakini kila kiumbe kingine kina makazi yake, Mungu tu ndiye anayeishi na kukaa kwenye kiti chake cha enzi. Hili Nitalielezea kwa mapana nikifika kwenye kipengele cha malaika na maisha ya malaika.

Katika spheres za kiroho kitu kinachitukuzwa sana ni Nuru au mwangaza wa utukufu, kwa maana kuwa ukuu wa kitu unaakisiwa na kiwango cha Nuru uliyo nayo, kuna viumbe vina nuru kubwa sana vingine vinayo ndogo, ukuu wa nuru unategemeana na ukaribu wako na Mungu lakini pia dimension ya ukomavu wako wa kiroho na viwango vyako vya rohoni.

Mara baada ya kipande cha Ndani kuna kipande cha kati kati ambacho ni kipande kilichotengwa maalumu kwa ajili ya makuzi ya kiroho, makuzi haya hutegemea na kusudi ambalo Mungu amemuumba kiumbe wake, wapo walioumbwa kuwa wakuu wa usimizi wa vitengo mbali mbali, wapo walioumbwa kuwa wakuu wasaidizi, wapo walioumbwa kuwa “raia wa kawaida” na kadhalika. Sphere hizi za kati kazi ni nyingi sana na hupokea viumbe vinavyokuwa na kukuwa kiroho kila siku, makuzi ya kiroho hayadhihiriki katika umri ila katika kiwango cha nuru uliyo nayo katika ulimwengu wa roho.

Nje kabisa ya spheres hizi za kiroho kuna sphere yenye maisha ya kawaida ya viumbe vya Mungu ambavyo aliviumba, hapa ndipo mwanzo wa kila kitu alichokiumba, hapa ndipo akila kilichoumbwa kwa dimension yake kinakaa, wanadamu kwa dimension yao na spheres zao, malaika kwa dimension yao na spheres zao, viumbe vingine pia vya rohoni vina dimension yao na spheres zao vile vile na kila kimoja kikiwa kinaishi bila kukiingilia kingine wala kukibugudhi kingine kwa mipaka aliyioweka Mungu kwa hekima yake.

Katika sphere hizi ikitokea mfano malaika akataka kuingia katika sphere ya wanadamu itambidi ajibadilishe awe kama wao kwa kuvaa umbo lao vinginevyo hataonekana nao. Vile vile ikitokea mwanadamu akataka kuingia kwenye dimension ya malaika inabidi avue mwili avae roho vinginevyo malaika hawana uwezo wa kui nterract nao na kuna portal maalumu za kuingilia si kuvamia vamia tu. Ikitokea umechakachua na ukaingia kwenye sphere isiyokuhusu kwako ni kosa na unatakiwa kuhukumiwa, na Hiki ndicho kisa hasa cha wale malaika 200 waliovaa miili wakaja kuishi na wanadmu wakasababisha dunia kuchafuka kwa maasi yaliyopelekea gharika.

Spheres za Kimwili
Mara baada ya spheres za kiroho kuna spehere za kimwili ambazo nazo zimegawanyika katika vipengele saba, vyote hivi ni kwa ajili ya makuzi ya kiroho na kimwili ya viumbe vya mwilini. Adamu alipopewa kuishi kwenye Bustani ya Edeni alipewa jukumu la yeye na viumbe vyake alivyokabidhiwa kukua katika sphere hizi zote saba akianzia katika sphere ya kwanza kabisa ambayo tunaiita bustani ya Edeni, bahati mbaya sana jamaa akajichanganya mapema kabisa.

Mara baada ya anguko la Lucifer iliundwa sphere nyingine inayojulikana kama sphere ya tatu au sphere ya giza au war sphere , ilichukua kama theluthi moja ya spheres zote za uumbaji wa Mungu kwa wakati huo.
Sphere hii ya giza kwa makosa ya Adam ikajitanua mpaka kwenye dunia yetu hii na kupelekea mwanadamu kuwa kiumbe mwenye Umungu na Ushetani ndani yake.

Nuru na giza vikawa ndani yake matokeao yake maisha yake yakawa ni mapambano na mahangaiko ya wema na ubaya vikiishi kwa pamoja ndani ya mtu mmoja kila kimoja kikishindaba kuvutia upande wake.
Juu ya dunia tunayoishi kwa sasa kuna sphere za nuru nne ambazo wengi wa wanadamu wanaokaribia kufa huziona na huona kama vile wanapita katika tunnel ya mwanga au njia Fulani ndefu sana ya mwanga tupu na kuelekea huko kwenye spheres za juu.

Wengi waliopata nafasi ya kufika kwenye sphere hizo za juu ya dunia walidhani wameishaingia mbinguni, na mara nyingi spheres hizo za nuru za juu ya dunia huwa zina ufanano na dunia hii isipokuwa zinakuwa ziko perfect sana na hazijachakachuka na giza kama tulilonalo huku, wengi wanaoingia hapo hupaita paradiso, lakini kimsingi hata paradiso yenyewe bado.

Chini pia ya dunia kuna spheres mbili za giza moja ikiwa ni giza tupu lililosheheni ushetani wa hali ya juu ambapo waovu wa dunia hii huenda kuchukua nguvu za giza kuja kuiharibu dunia, ni shemeu ambapo mapepo mengi sana yanapatikana na roho za wandamu waliokufa katika giza hugeuzwa kuwa maajenti wa kuzimu kuja kuvuruga maisha huku duniani, na hapa ndipo kuna kitu kinaziliwa kinaitwa majeshi ya wafu, vibwengo, vinyamkera , aliens na mengineyo.

Chini kabisa kuna sphere moja iliyo na giza kuu ambalo ndipo Lucifer mwenyewe yupo anaishi, huko ndiko kuzimu hasa ambapo ni makao makuu ya uovu wote kukisheheni hekima yote ya kishetani na viwanda vikubwa vya uharibifu na ubunifu wa kila namna lengo likiwa ni moja tu kumkomoa Mungu na viumbe vyake.
Nitaizungumzia Kuzimu kwa mapana yake baadaye mara baada ya kuwachambua malaika na maisha yao kwa upana wake.

Kabla ya hapo tuyazungumzie maisha ya ulimwengu wa kiroho kabla ya kuumbwa kwa dunia yetu, maisha yanayojumusiha pia uasi na anguko la Lucifer.

Sehemu ya Pili itafuata soon…
Labda ungeonyesha kwanza chanzo cha habari ya makala yako - mfano wapi imeandikwa Mungu akisema yeye ni "Mungu Baba" etc. Lengo la uandishi ni kutoa habari inayosimama yenyewe, lakini makala yako haya yana habari za kupika na hayatokani na utafiti ulioufanya kwa sababu kama ingekuwa hivyo angalau ungeonyesha marejeo ya vyanzo vyako au hata utafiti wa watu wengine wenye 'conclusion' kama ya kwako. Katika yote haya jambo muhimu likiwa 'intellectual humility'.
 
Back
Top Bottom