john achila mukumwa
Senior Member
- Jan 4, 2024
- 135
- 273
Biblia inavyosema kuhusu kiburi
Kiburi siyo dhambi unayofanya kwa njia sawa na kuiba au kusema uwongo. Ni mtazamo wa moyo na njia ya kufikiria. Huwezi kuona upepo, lakini unaweza kuona athari za upepo, na ni sawa na kiburi. Huwezi kuona kiburi, lakini unaweza kuona matokeo yake. Kimsingi, kiburi ni kufikiria wewe ni bora kuliko vile ulivyo (Warumi 12:3).
Kwa kawaida katika matukio ambayo Biblia inataja majivuno, fahari, au kiburi, ni tabia au nia iliyochukiwa na Mungu. Biblia inatuambia wale wenye kiburi na wenye moyo wenye kiburi ni chukizo kwake: "Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa Bwana; Hakika, hatakosa adhabu" (Methali 16:5).
Kuna vitu sita anavyochukia Mwenyezi-Mungu; naam, vitu saba ambavyo ni chukizo kwake: (1) macho ya kiburi, (2) ulimi mdanganyifu, (3) mikono inayoua wasio na hatia, (4) moyo unaopanga mipango miovu, (5) miguu iliyo mbioni kutenda maovu, (6) shahidi wa uongo abubujikaye uongo, na (7) mtu achocheaye fitina kati ya ndugu (Methali 6:16-19).
Kati ya mambo saba Biblia inatuambia kwamba Mungu huchukia, "macho ya kiburi" ndiyo ya kwanza iliyoorodheshwa (Methali 6: 16-19).
Kwa nini kiburi ni dhambi hivyo?
1. Kiburi ni kujitukuza wenyewe na kujinutukia sifa kwa ajili ya kitu ambacho Mungu amekamilisha.
2. Kiburi ni kuchukua utukufu wa Mungu pekee na kuweka kwa wenyewe.
3. Kiburi, kimsingi ni ibada nafsia. Kitu cho chote sisi tunachokamilisha katika dunia hii hakingewezekana isingekuwa ni Mungu anatuwezesha na kututunza. "Maana ni nini anayekupambanua na mwingine? Nawe una nini usichokipokea? Lakini iwapo ulipokea, wajisifia nini kana kwamba hukupokea?" (1Wakorintho 4:7).
Hiyo ndiyo sababu sisi humpa Mungu utukufu anaostahili peke yake.
Kiburi, pia kinajulikana kama ubatili, kinachukuliwa kuwa dhambi ya asili, na mbaya zaidi, ni kati ya dhambi saba kuu za kishetani zaidi. Pia inafikiriwa kuwa chanzo cha dhambi nyingine kuu.
Kiburi ni kinyume cha unyenyekevu. Kiburi ni hali ya "mpinga-Mungu", nafasi ambayo nafsi na nafsi inapingana moja kwa moja na Mungu: "uchafu, hasira, uchoyo, ulevi na yote hayo, si kitu kwa kulinganisha: ilikuwa ni kwa kiburi kwamba Lusifa akawa mwovu: kiburi kinaongoza kwa kila hali nyingine".
Kumbuka kwamba kiburi ni nyoka mbaya zaidi aliye moyoni, msumbufu mkuu zaidi wa amani ya roho na ushirika mtamu na Kristo.
Kiburi ni dhambi ya kwanza kuwahi kuwako na iko chini kabisa katika msingi wa jengo zima la Lusifa, na ndiyo iliyong'olewa kwa shida zaidi, na ndiyo iliyofichwa zaidi ya siri na ulaghai katika kila aina ya siri na udanganyifu.
Matumizi ya kisasa ya kiburi yanaweza kujumlishwa katika methali ya kibiblia: "kiburi hutangulia uharibifu; roho yenye majivuno hutangulia anguko". Kwa kifupi, "kiburi hutangulia anguko" (Mithali 16:18).
"Kiburi kinachopofusha", husababisha vitendo vya kipumbavu dhidi ya akili ya kawaida. Kwa mfao, katika uchanganuzi wa kisiasa, "kiburi" mara nyingi hutumiwa kuelezea jinsi viongozi walio na mamlaka makubwa kwa miaka mingi wanavyozidi kujiamini na kudharau ushauri, na kuwaongoza kutenda kwa msukumo.
Badala ya majivuno, Biblia inatufundisha kinyume chake. 1Wakorintho 13:4 inasema, "Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni".
Wakristo wanaitwa ili kuonyesha upendo; kiburi ni kinyume na upendo huo. Warumi 12:3 inasema, "Kwa hiyo nawaarifu ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu." Hatuwezi kuwa na majivuno huku tukiwa na unyenyekevu wa kiungu.
Kuwa na mtazamo wa majivuno kuwa "Mimi ni bora zaidi kukuliko" huwa unatishia na kuharibu mahusiano yetu na wengine. Hata hivyo, Yesu alitufundisha kuweka wengine mbele ya nafsi zao: "Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu anayetaka kuwa mkubwa kwenu, atakuwa mtumishi wenu, na mtu anayetaka kuwa wa kwanza wenu, atakuwa mtumwa wa wote. Kwa maana Mwana wa Adamu naye hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi" (Marko 10:43-45).
Ikiwa mtazamo wetu ni wa kiburi, hatuwezi kutumikia wengine vizuri
Mtume Paulo alielezea mawazo hayo katika barua yake kwa kanisa la Filipi: "Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake" (Wafilipi 2:3).
Hii ni tofauti sana kutokana na hali ya ushindani ya dunia yetu hii leo, na kutuacha bila nafasi yo yote sisi kuwa na kiburi. Ambapo dunia inatusukuma kujitahidi kufikia ngazi ya juu bila kujali gharama, na kuwa wenye kiburi.
Wakati sisi hufanya hivyo, Yesu ametuagiza kuwa tofauti: "Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa" (Luka 14:11; Yakobo 4:6).
Kuhusu mtazamo wetu kwa Mungu na wanadamu wenzetu, Mungu anatupa ahadi mbili: Kwanza, wapumbavu wataadhibiwa (Methali 16:5; Isaya 13:11).
Pili, "Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao" (Mathayo 5:3).
Methali 21:24 inasema “Mwenye kiburi na kutakabari, jina lake ni mbishi; Hutenda mambo katika majivuno ya kiburi chake”. Na, Methali 16:5 inasema “Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa Bwana; Hakika hatakosa adhabu.
Kwa kweli, "Mungu huwapinga wenye kiburi lakini huwapa wanyenyekevu neema" (1Petro 5:5, Methali 3:34).
JE, TUNASHINDAJE KIBURI
Ikiwa tunaona kiburi chetu na athari zake, na tukijua tunapambana nacho katika mawazo yetu, maneno na matendo, tunaweza kukishinda kiburi. "Mkaribieni Mungu, naye Mungu atawakaribia ninyi" (Yakobo 4:8).
Kila mmoja anajielewa tabia yake. Tunapofanya kazi na Mungu katika mawazo yetu, huleta marekebisho na hukumu. Tunaona mahali ambapo kiburi kinafanya kazi. Tunaelewa ni wapi mapenzi yetu binafsi yako hai, kwa hiyo tunaweza kujinyenyekeza kwa kuwa watiifu kwa sheria za Mungu. Ndiyo sababu imeandikwa "Jinyenyekeze mbele za Bwana…" (Yakobo 4:10). Mtu asione aibu kujinyenyekeza, kwa kufikiri kuwa ataonekana kuwa dhaifu au mnyonge. Ni kosa zaidi, kujifikiria hivyo. Badala yake, unyenyekevu ni nguvu (strength).
Kiburi siyo dhambi unayofanya kwa njia sawa na kuiba au kusema uwongo. Ni mtazamo wa moyo na njia ya kufikiria. Huwezi kuona upepo, lakini unaweza kuona athari za upepo, na ni sawa na kiburi. Huwezi kuona kiburi, lakini unaweza kuona matokeo yake. Kimsingi, kiburi ni kufikiria wewe ni bora kuliko vile ulivyo (Warumi 12:3).
Kwa kawaida katika matukio ambayo Biblia inataja majivuno, fahari, au kiburi, ni tabia au nia iliyochukiwa na Mungu. Biblia inatuambia wale wenye kiburi na wenye moyo wenye kiburi ni chukizo kwake: "Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa Bwana; Hakika, hatakosa adhabu" (Methali 16:5).
Kuna vitu sita anavyochukia Mwenyezi-Mungu; naam, vitu saba ambavyo ni chukizo kwake: (1) macho ya kiburi, (2) ulimi mdanganyifu, (3) mikono inayoua wasio na hatia, (4) moyo unaopanga mipango miovu, (5) miguu iliyo mbioni kutenda maovu, (6) shahidi wa uongo abubujikaye uongo, na (7) mtu achocheaye fitina kati ya ndugu (Methali 6:16-19).
Kati ya mambo saba Biblia inatuambia kwamba Mungu huchukia, "macho ya kiburi" ndiyo ya kwanza iliyoorodheshwa (Methali 6: 16-19).
Kwa nini kiburi ni dhambi hivyo?
1. Kiburi ni kujitukuza wenyewe na kujinutukia sifa kwa ajili ya kitu ambacho Mungu amekamilisha.
2. Kiburi ni kuchukua utukufu wa Mungu pekee na kuweka kwa wenyewe.
3. Kiburi, kimsingi ni ibada nafsia. Kitu cho chote sisi tunachokamilisha katika dunia hii hakingewezekana isingekuwa ni Mungu anatuwezesha na kututunza. "Maana ni nini anayekupambanua na mwingine? Nawe una nini usichokipokea? Lakini iwapo ulipokea, wajisifia nini kana kwamba hukupokea?" (1Wakorintho 4:7).
Hiyo ndiyo sababu sisi humpa Mungu utukufu anaostahili peke yake.
Kiburi, pia kinajulikana kama ubatili, kinachukuliwa kuwa dhambi ya asili, na mbaya zaidi, ni kati ya dhambi saba kuu za kishetani zaidi. Pia inafikiriwa kuwa chanzo cha dhambi nyingine kuu.
Kiburi ni kinyume cha unyenyekevu. Kiburi ni hali ya "mpinga-Mungu", nafasi ambayo nafsi na nafsi inapingana moja kwa moja na Mungu: "uchafu, hasira, uchoyo, ulevi na yote hayo, si kitu kwa kulinganisha: ilikuwa ni kwa kiburi kwamba Lusifa akawa mwovu: kiburi kinaongoza kwa kila hali nyingine".
Kumbuka kwamba kiburi ni nyoka mbaya zaidi aliye moyoni, msumbufu mkuu zaidi wa amani ya roho na ushirika mtamu na Kristo.
Kiburi ni dhambi ya kwanza kuwahi kuwako na iko chini kabisa katika msingi wa jengo zima la Lusifa, na ndiyo iliyong'olewa kwa shida zaidi, na ndiyo iliyofichwa zaidi ya siri na ulaghai katika kila aina ya siri na udanganyifu.
Matumizi ya kisasa ya kiburi yanaweza kujumlishwa katika methali ya kibiblia: "kiburi hutangulia uharibifu; roho yenye majivuno hutangulia anguko". Kwa kifupi, "kiburi hutangulia anguko" (Mithali 16:18).
"Kiburi kinachopofusha", husababisha vitendo vya kipumbavu dhidi ya akili ya kawaida. Kwa mfao, katika uchanganuzi wa kisiasa, "kiburi" mara nyingi hutumiwa kuelezea jinsi viongozi walio na mamlaka makubwa kwa miaka mingi wanavyozidi kujiamini na kudharau ushauri, na kuwaongoza kutenda kwa msukumo.
Badala ya majivuno, Biblia inatufundisha kinyume chake. 1Wakorintho 13:4 inasema, "Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni".
Wakristo wanaitwa ili kuonyesha upendo; kiburi ni kinyume na upendo huo. Warumi 12:3 inasema, "Kwa hiyo nawaarifu ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu." Hatuwezi kuwa na majivuno huku tukiwa na unyenyekevu wa kiungu.
Kuwa na mtazamo wa majivuno kuwa "Mimi ni bora zaidi kukuliko" huwa unatishia na kuharibu mahusiano yetu na wengine. Hata hivyo, Yesu alitufundisha kuweka wengine mbele ya nafsi zao: "Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu anayetaka kuwa mkubwa kwenu, atakuwa mtumishi wenu, na mtu anayetaka kuwa wa kwanza wenu, atakuwa mtumwa wa wote. Kwa maana Mwana wa Adamu naye hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi" (Marko 10:43-45).
Ikiwa mtazamo wetu ni wa kiburi, hatuwezi kutumikia wengine vizuri
Mtume Paulo alielezea mawazo hayo katika barua yake kwa kanisa la Filipi: "Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake" (Wafilipi 2:3).
Hii ni tofauti sana kutokana na hali ya ushindani ya dunia yetu hii leo, na kutuacha bila nafasi yo yote sisi kuwa na kiburi. Ambapo dunia inatusukuma kujitahidi kufikia ngazi ya juu bila kujali gharama, na kuwa wenye kiburi.
Wakati sisi hufanya hivyo, Yesu ametuagiza kuwa tofauti: "Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa" (Luka 14:11; Yakobo 4:6).
Kuhusu mtazamo wetu kwa Mungu na wanadamu wenzetu, Mungu anatupa ahadi mbili: Kwanza, wapumbavu wataadhibiwa (Methali 16:5; Isaya 13:11).
Pili, "Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao" (Mathayo 5:3).
Methali 21:24 inasema “Mwenye kiburi na kutakabari, jina lake ni mbishi; Hutenda mambo katika majivuno ya kiburi chake”. Na, Methali 16:5 inasema “Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa Bwana; Hakika hatakosa adhabu.
Kwa kweli, "Mungu huwapinga wenye kiburi lakini huwapa wanyenyekevu neema" (1Petro 5:5, Methali 3:34).
JE, TUNASHINDAJE KIBURI
Ikiwa tunaona kiburi chetu na athari zake, na tukijua tunapambana nacho katika mawazo yetu, maneno na matendo, tunaweza kukishinda kiburi. "Mkaribieni Mungu, naye Mungu atawakaribia ninyi" (Yakobo 4:8).
Kila mmoja anajielewa tabia yake. Tunapofanya kazi na Mungu katika mawazo yetu, huleta marekebisho na hukumu. Tunaona mahali ambapo kiburi kinafanya kazi. Tunaelewa ni wapi mapenzi yetu binafsi yako hai, kwa hiyo tunaweza kujinyenyekeza kwa kuwa watiifu kwa sheria za Mungu. Ndiyo sababu imeandikwa "Jinyenyekeze mbele za Bwana…" (Yakobo 4:10). Mtu asione aibu kujinyenyekeza, kwa kufikiri kuwa ataonekana kuwa dhaifu au mnyonge. Ni kosa zaidi, kujifikiria hivyo. Badala yake, unyenyekevu ni nguvu (strength).