Bibi Harusi mtarajiwa aingia mitini baada ya kupelekwa saluni

Bibi Harusi mtarajiwa aingia mitini baada ya kupelekwa saluni

wadzelino

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2019
Posts
231
Reaction score
391
Dunia imebeba mengi sana na Ukistaajabu ya Musa Hujayaona ya Firauni.

Hii imetokea Kijijini kwetu huku. Baada ya Utambulisho na maridhiano ya pande mbili. Mahari ikatolewa, Mil 2.5 hivi, na mipango ya harusi ikaanza.

Ee bwana ee siku zimesonga, hatimaye siku ya harusi ikawadia, mapema kabisa bibi Harusi akapelekwa saluni ili apambwe, kumbe alikuwa na yake, ni kwamba watu walisubiri bibi harusi hakurejea, almost wiki, taharuki imetanda.

Wazazi wa pande zote hawaelewi, wale wa binti ndo kabisa, kwa kuwa fedha walopokea kama Mahari ilishatumika, na Hawana kipato cha kuweza kurejesha, baada ya wiki.

Binti kaja kuonekana, akapangwa fasta baada ya manung'uniko ya Wazazi hapa na pale akakubali kukaa nao chini kuwaeleza ukweli, heee. Hawakuamini walichosikia!

Nanukuu "Kwa kweli mimi wakati nakutana na huyu (bwana aliyetaka kufunga ndoa) nilikuwa na bwana mwingine ninaempenda sana, ila huyu nilimpendea fedha tu, alikuwa akinihudumia, sasa ukweli ni kwamba Sikuwa tayari animiliki moja kwa moja, ndiyo maana nilifanya vile"

Mama yake alianguka ghafla.

Itaendelea...
 
kama sio kusini mwa Tz bwanawewe nawasi wasi 😃🙌
 
Huyo mwamba si juzi tu alileta uzi huu wa malalamiko ya namna ya kurudishiwa mahali baada ya binti kumkataa
 
Karma is real uyu demu atokuja kuolewa tena uyo anaempend nae anawake anampenda
 
Nimechumbia kwa binti fulani mama amesema ni binti anatabia nzuri

Wa hivi huwa wanagongewa sana
 
[emoji445][emoji445][emoji445][emoji445][emoji445] unapunguza utamu[emoji445][emoji445][emoji445][emoji445][emoji445][emoji448][emoji448][emoji448][emoji448][emoji448] unapinguza utamuuuuu....endeleeni na verse
 
Back
Top Bottom