Biashara ya wifi internet router mtaani

Biashara ya wifi internet router mtaani

Naona ni biashara nzuri!
Shinyanga, nimeona mitaani jamaa wanachaji 5,000/= kwa mwezi, na pale stand (wenyewe wanaiita Manyoni) wanatoa huduma hiyo kwa 1,000/= kwa siku. Kila saa nne asubuhi, wanabadilisha password. Kuna watu wameajiriwa, wanazunguka kila kona, kutafuta na kuunganisha wateja.
Ukiniuliza hiyo biashara inafanyika kwa kujisajiri kwa wenye mamlaka, jibu sina!
Kumbe ina chakula ee
 
nipo mkoa nataka ninunue ya Airtel wadau wawe wanachangia buku buku nione kama tutaishi
Hapa changamoto iliyopo ni kwamba wanaweza waka scan hiyo barcode ya wi fi then wakawa wanatumia tuu bure kwa kuunganishana,nadhani kwanza tungejuwa namna ya kuzuia watu ku scan then tungefanya hii biashara kwa usalama zaidi
 
Utapiga ela japo matumiz utacontrol vp
Ile huwa inakuwa unlimited unalipia kwa mwezi na nadhani device moja wanaweza kutumia watu 10 hadi 15.
Sema kibongobongo ni ngumu kidogo kuiplement hii labda kama unaishi kwenye nyumba za kota au hostel inakuwa rahisi
 
Nilikuwa nina wazo kama lako lakini ni kwenye vyuo... unaingia ubia na chuo, kwasababu router zao zina-range ndogo na overloaded: unafunga routers kila angle na populated area kwenye chuo. Kwa maeneo ya mjini ISP anakuvutia Fiber. User anaingia kwa username na password, Internet plan yake iki-expire ndiyo basi.

Vitu vya kuzingatia:

1. Internet: ISP + B2B, Fiber + CPE/ONT

2. Wi-Fi setup: 3x enterprise Wi-Fi 5/6 APs, SSL certificate, Cat6 UTP, RJ45

3. User management: RADIUS server, Ubiquiti UniFi

4. Gateway: MikroTik

5. Monitoring: LibreNMS, USB/SMS modem

6. TCRA

7. Power: TANESCO + Solar+Battery backup, UPS 1 kVA, LiFePO4 12 V 50 Ah battery

Hizi ni hesabu za kwenye karatasi...

TZS 2,000... 10Mbps/24hrs

TZS 40,000... 20Mbps/30 days

Ni wazo tu sina hakika kama linaweza kufanyika vizuri kwasababu vyuo vingi tayari vina Wi-Fi zao.
 
mimi nko kondoa mjin naona 4G network ndio iiyopo kwa mitandao yote kwa iyo nikinunua airtel 5G router haitanisumbua network
IMG-20250720-WA0068(5).jpg
 
Wengi mnalichukulia juu juu. Pigeni hesabu za kiufundi pia. Hizi router zilizokuwa designed kwa matumizi ya nyumbani nyingi haziendi zaidi ya 30m. Na kama eneo lina vizuizi kama kuta au miti inaweza isifike hata 15m ukakutana na dead zone.
Pia kuna changamoto ya ukomo wa idadi ya watumiaji wanaoweza kujiunga. Vifaa vingi vya bei rahisi ni watumiaji 32. Nyengine watumiaji 64.
Zingatia hayo yote usije kuona biashara ngumu.
Kama una pesa unaweza kununua ap kuongeza umbali na kufanya meshing kwa router nyengine kuongeza ubora wa signal. Wengine wanaweka router za repeater lkn huwa zinapunguza nguvu ya mtandao.
 
Utapiga ela japo matumiz utacontrol vp
Kama ni cable internet akiweka kwenye routers kama za MikroTik unaweza ku control na kufanya unachotaka hata ukitaka kuuza kwa mfumo wa bando au vocha unaweza hamna mambo ya kuscaniana kwa QR Code hapa mianya yote inabanwa... Kuna aina ya Router za MikroTik zina hizi features ukipata mtu mtaalamu ana kuconfigia..
 
Naona ni biashara nzuri!
Shinyanga, nimeona mitaani jamaa wanachaji 5,000/= kwa mwezi, na pale stand (wenyewe wanaiita Manyoni) wanatoa huduma hiyo kwa 1,000/= kwa siku. Kila saa nne asubuhi, wanabadilisha password. Kuna watu wameajiriwa, wanazunguka kila kona, kutafuta na kuunganisha wateja.
Ukiniuliza hiyo biashara inafanyika kwa kujisajiri kwa wenye mamlaka, jibu sina!
Dah watu wanapambana sana.
 
Back
Top Bottom