Biashara ya wifi internet router mtaani

Biashara ya wifi internet router mtaani

Kataa wahuni

Member
Joined
Jul 21, 2025
Posts
16
Reaction score
20
Habari zenu wakuu kama heading inavojieleza hapo juu, Nina mpango wa kuanzisha biashara ya wifi internet mtaani kwa kupitia router na kuwalipisha wateja kwa masaa Ninaomba kuuliza je kisheria iko sawa, pia kuna changamoto gan katika hii biashara Naomba kuwasilisha
 
TCRA wanataka upate leseni, application fee ya leseni ni 150k, leseni ni kama 450k hivi kwa mwaka na kuendelea kulingana na ukubwa wa eneo unalotaka kutoa huduma. Hata kama ukipata wateja 2 wakikukamata unauza bila vibali unajumuishwa na wahujumu uchumi.

All the best.
Kuhusu leseni mamlaka husika nitazitembelea ondoa shaka
 
Utapiga ela japo matumiz utacontrol vp
Naona ni biashara nzuri!
Shinyanga, nimeona mitaani jamaa wanachaji 5,000/= kwa mwezi, na pale stand (wenyewe wanaiita Manyoni) wanatoa huduma hiyo kwa 1,000/= kwa siku. Kila saa nne asubuhi, wanabadilisha password. Kuna watu wameajiriwa, wanazunguka kila kona, kutafuta na kuunganisha wateja.
Ukiniuliza hiyo biashara inafanyika kwa kujisajiri kwa wenye mamlaka, jibu sina!
 
TCRA wanataka upate leseni, application fee ya leseni ni 150k, leseni ni kama 450k hivi kwa mwaka na kuendelea kulingana na ukubwa wa eneo unalotaka kutoa huduma. Hata kama ukipata wateja 2 wakikukamata unauza bila vibali unajumuishwa na wahujumu uchumi.

All the best.
Naomba utaratibu ukoje...nataka nitengeneze customer base yangu ya wateja hata kama 500 tu hivi inatosha

Na kwa bongo nani ni main source ya internet distributor
 
Back
Top Bottom