Biashara ya Viungo (Spices)

Biashara ya Viungo (Spices)

Governor of Bettors-GB

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2013
Posts
10,734
Reaction score
9,913
Jamani Habari Zenu.
Nilikuwa nataka kupanua wigo wa Biashaya ya Viungo(Spices). Nina duka dogo Zanzibar ila nataka niongeze wigo wa biashara.

Kwanza ninamalizia website yetu,ambayo itakuwa na maelezo yote. Natarajia kupost kwenye baadhi ya Local Magazine pia.

Nilikuwa nataka Mawazo yenu kwa mikoa ya hapa Tanzania ambayo biashara hizi au viungo hivi vinasoko zuri. Hata kama nchi za Jirani pia sio mbaya maana sina Ideas kwa nje ya Znz

Viungo(Spices) ni kama zifuatazo:-
Cinnamon (Mdalasini)
Cumin (Uzile)
Ginger (Tangawizi)
Black pepper(Pilipili Manga)
Cardamon (Hiliki)
Lemons Grass (Mchaichai)
Cloves (Karafuu)
Vanilla (Vanila)
Nutmeg (Kungu Manga)
Turmeric (Bizari)
Coriander(Giligilani)
Fenugreek (uwatu)
Thyme(zahatari)

Spice Combination(Masala):-
Tea Masala
Fish/Meat Masala

Spices Gift Packs
-Oils Extracts
-Herbal Soaps

Na Je kuna Mikoa ambayo inalimazao lolote hapo juu kwa wingi.Na Idea ya kilo moja ni kiasu gani (Hii itanisaidia kama nitapata order kubwa,kujua wapi pa kuchukua)

Mbarikiwe
Naomba kuwasilisha,​
 
Mkuu samahan! Kwa kwa sasa hizo bidhaa unajumua kutoka wap?
Nakutakia kazi njema..ahsante!!
 
Wanajamvi naomba msaada,

Nahitaji kuanzisha biashara ya kuuza viungo vya chakula kama vya pilau, mboga na chai nk, kiukweli vitu hivyo sina ufahamu navyo sana though najua viko vingi so naomba kujua wapi tavipata kwa bei ya jumla.

Asanteni.
 
Kariakoo soko dogo kuna kila aina ya viungo kwa bei ya jumla au uvifuate mashambani mf mdalasini unapatikana Morogoro au Tanga maana ndo unakolimwa.

Pia inategemeana unataka kuuza na kupack kwa style gani maana wengine wanauza vikiwa vizima vizima na wengine wanauza unga wake ukiwa kwenye pakti au mkopo aka masala.
Unapatikana wapi?

Mi nipo Kigamboni na ndo biashara yangu na ukipenda tunaweza kushirikiana pia.

Uliza chochote kuhusu viungo ntakusaidia. 0784800989
 
Habari zenu wana Jf, napenda sana kufanya biashara ya viungo vya chai na vya chakula kama vile iliki, tangawizi, mdarasini nk ila changamoto nilionayo mpaka sana ni kujua ni maeneo gani vinalimwa kwa wingi ili niweze kwenda kufungasha moja kwa moja toka kwa wakulima .

Pia nakaribisha mtu atakae hitaji tushirikiane katika biashara hii.
 
Mkuu wa kazi kwema,

Kiukweli sina uzoefu na hizi habari ila wacha nikupe mchangi wangu,

Kwa sababu una nia na hiyo biashara yako nenda sokoni tafuta wanaofanya biashara hiyo na waulize wanapata wapi wao,

Fanya survey ya kutosha naamin utafanikiwa

Kila la kheri mkuu
 
Habari zenu wapendwa,naitwa howllaht,nnaishi Dar es salam nimeanza kujishughulisha mwenyewe kwa kuuza baadhi ya viungo kama-;
Majani ya chai
Hiriki
Karafuu
Tangawizi
Mdalasini
Bidhali
Pilipili manga Nk ila bado mchanga sijawa na wateja wengi..nifanye nini ili niweze kuongeza wateja?Naombeni mawazo yenu tafadhali
Ahsanten
 
Tengeneza mtandao wa wateja kwa kupita ktk maduka yanayouza bidhaa hizo, hakikisha unatembea na sample iliyo ktk kifungashio kizuri! Kila unaekutana nae chukua na namba yake ya simu Hata kama haitaji mzigo kwa muda huo, zoezi hili lifanye kikamilifu kwa angalau wiki mbili, kitaalam hiyo inaitwa business platform, kupitia zile namba za simu ulizokusanya utaanza kurusha msg taratibu ila hapa ni kama upo mawindoni hakikisha unaweka bei ya chini kabisa kafaida kawe kadogo sana ili kumteka mteja! Namba zingine utakuta zina what's up hapo jichekelee maana utaweza kutuma bei zako pamoja na picha mbali mbali za bidhaa zako! Zingatia sana ubora na bei!
 
Fanya ivi,Tumia chance ya kukopesha,baada ya wiki mteja ndo analipa,naimani hao watakaokopa ndiyo watakuwa wateja wako wa permanent
 
Nauza viungo vya pilau gram 100 kwenye package nzuri
Viungo ni fresh nasaga mwenyewe kabsa ni mchanganyiko wa hiliKi, mdalasini, binzari nyembamba, na giligilan
IMG_1812.JPG
 
Kuhusu vanilla tuwasiliane mi ni mkulima wa vanilla nipo mkoani kagera utapata kiadi chochote unachotaka tuwasiliane kwa namba 0622 296251.
Jamani Habari Zenu.
Nilikuwa nataka kupanua wigo wa Biashaya ya Viungo(Spices). Nina duka dogo Zanzibar ila nataka niongeze wigo wa biashara.

Kwanza ninamalizia website yetu,ambayo itakuwa na maelezo yote. Natarajia kupost kwenye baadhi ya Local Magazine pia.

Nilikuwa nataka Mawazo yenu kwa mikoa ya hapa Tanzania ambayo biashara hizi au viungo hivi vinasoko zuri. Hata kama nchi za Jirani pia sio mbaya maana sina Ideas kwa nje ya Znz

Viungo(Spices) ni kama zifuatazo:-
Cinnamon (Mdalasini)
Cumin (Uzile)
Ginger (Tangawizi)
Black pepper(Pilipili Manga)
Cardamon (Hiliki)
Lemons Grass (Mchaichai)
Cloves (Karafuu)
Vanilla (Vanila)
Nutmeg (Kungu Manga)
Turmeric (Bizari)
Coriander(Giligilani)
Fenugreek (uwatu)
Thyme(zahatari)

Spice Combination(Masala):-
Tea Masala
Fish/Meat Masala

Spices Gift Packs
-Oils Extracts
-Herbal Soaps

Na Je kuna Mikoa ambayo inalimazao lolote hapo juu kwa wingi.Na Idea ya kilo moja ni kiasu gani (Hii itanisaidia kama nitapata order kubwa,kujua wapi pa kuchukua)

Mbarikiwe
Naomba kuwasilisha,​
 
Back
Top Bottom