Me naifanya japo nimeanza na mtaji mdogo lakini nashukuru unasogea.
uzuri wa vitu hivyo ni rahisi kusafirisha as unakuta mzigo wa milioni moja lakini haujafika kilo mbili.
Kwa ushauri inategemea na mtaji utakaoanza nao, kama una mtaji mkubwa tafuta fremu eneo lililochangamka uwe unauza rejareja kwa kumuweka mtu pia itakua store yako, wewe utakua na begi lako unazunguka kutafuta wateja wa hapa hapa dar na wa mikoani unaanza nao kwa kutengeneza nao connection kidogo kidogo.
Changamoto kubwa ni kuwa ukiwa una supply bila kuwa na ofisi/fremu permanent watu wanaogopa as anaweza kununua mzigo ukawa mbovu alafu hajui pa kukupata.
hivyo vitu ulivyotaja ukaongezea makava ya simu, earphones, mouse, mp 3 na mp 4, pads za play station, power bank n.k