Biashara ya uji

Biashara ya uji

Tuseme za ukweli uji umekuwa common kwa sasa!....sijajua km kuna kipya!
Ningekuwa ndo mie Maathai ningeenda Katoro kuchukua vitenge vya bei chee!...kila kitenge sikosi 4000!.chukua kitenge kwa 18000uza kwa 25000

Uji sio common kijana nenda instagram mtafute mtu anaitwa habpap kaangalie biashara ya uji anavyofanya utaelewa


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Habari za majukumu wanajamvi, matumaini yangu mnachukua taadhari dhidi ya janga hili la Corona.

Niende moja kwa moja kwenye mada. Mimi ni binti miaka 25 nimemaliza chuo mwaka wa tatu sasa sijabahatika kupata ajira rasmi ila nnajishughulisha na shughuli za hapa na pale mradi mkono uende kinywani.

Ninatamani kuanzisha biashara ya kuuza uji katika sehemu zenye watu wengi. Kwa sasa naishi Iringa. Malengo yangu ni kuwa na sehemu kama 10 za kuuza uji (sio ofisi bali vijana wa kutembeza katika maeneo hayo 10) asubuhi na jioni kwa mtaji wa sh 300,000.

Naomba kwa mwenye ujuzi au uzoefu au hata mawazo bunifu au ushauri wowote juu ya biashara hii.

Asante.

d9aa857a-3583-4ac6-81c4-263f6b2487e1.jpg
c6833ec3-bfb1-4393-99c7-07ca9af99d77.jpg
47873d84-2d77-428e-ac2a-a2b4f886952d.jpg


Uji uo unauzwa elfu 5000 kwa kikombe



Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Ushauri ni kuwa biashara ni kama uhai wa kiumbe..haiitaji majaribio bali ni real performance. Ukifanya kitu bora mkono uende kinywani ni bora uache mana utaharibu muda na pesa zako. Tafuta watu wanaoajiri vibarua utapata cha kupeleka mkono kinywani..ila kama unataka biashara ya uji fanya kwa ukubwa wake
 
Nikutie moyo, mimi ni muajiriwa serikalini, Mshahara wangu kwa mwezi ni Tshs 2,800,000/=...Lakini naifanya hiyo biashara ya uji kwa mwezi napata Tshs 780,000/=. Gharama za uendeshaji ni Tshs 250,000/= kwa mwezi. Faida ya uji nayobakiwa nayo ni Tshs 530,000/=. Hivyo ada za watoto wangu Private school zinalipwa na hiyo biashara ya uji.
Pambana asikurudishe mtu nyuma
 
Soni Lushoto Tanga nlikunywa uji wa mihogo umemixiwana mapilipili manga asee nlienjoy sana best lucky
 
Nikutie moyo, mimi ni muajiriwa serikalini, Mshahara wangu kwa mwezi ni Tshs 2,800,000/=...Lakini naifanya hiyo biashara ya uji kwa mwezi napata Tshs 780,000/=. Gharama za uendeshaji ni Tshs 250,000/= kwa mwezi. Faida ya uji nayobakiwa nayo ni Tshs 530,000/=. Hivyo ada za watoto wangu Private school zinalipwa na hiyo biashara ya uji.
Pambana asikurudishe mtu nyuma
Unatumia style gani kuuza huo uji?
Unauza kwa kutembeza mtaan?
Au unauza kwenye banda?
 
Back
Top Bottom