Mkuu, nashukuru kwa interest na maswali yako. Itakuwa vizuri kama upo serious tuwasiliane uje kwenye biashara ukagueKila kitu na upate maelezo yote. Kwa kweli hiyo m35 nimekisiakwa kujiuliza hii biashara inayo niingizia kipato cha m5 kwa mwezinikiwa nimeweka float ya m12 inafaa niiuze bei gani? basi kama utanipasababu za kutosha nitapunguza bei. Asante
Mkuu, najaribu tena nikujibu.Naona unataka gumzo yote ifanyike kwenye forum. Ok.
Kwanza nikutaarifu, biashara ni willing buyer and willing seller kwa hiyo nnaweza kutaja bei yeyote ambayo naona inafaa.
Hii m35 ni goodwill kama @weehodie alivyo sema. kama ipo juu basi nikipewa sababu ya kupunguza kidogo nipo
tayari.
Pili. Biashara ina ofisi nane. zote za kukodisha. Kwa m35 utapata na mikataba ya kodi ya mwaka mmoja.
Kila ofisi ina kaunta na viti. ofisi mbili ni kaunta zenye madirisha ya vioo ya kutolea huduma, mbili ni nondo na grill, zingine ni open kaunta lakini muhudumu anakuwa mbali na mteja. kodi zote pamoja ni 360,000 kwa mwezi.
computer ni moja, laptop yenye mtandao wa mpesa kukuwezesha kuangalia kazi zinavyo enda.
Simu za kazi ni 19 ikiwa ni pamoja na head offfice na management till ya kukuwezesha kuhamisha hela kutoka ofisi moja hadi nyingine, kupokea commission n.k
Wafanyakazi ni 11. mishahara yao wote kwa mwezi ni 820,000. wafanya kazi 9 wapo tayari kuendelea na boss mpya.
Kuna taratibu tunazo zitumia ili kuwa na uhakika kwamba kwa sehemu kubwa wanakuwa waaminifu.
Maduka mawili yapo dsm mengine yote ni mikoani. hii ni muhimu kwa sababu hutapata tatizo la float kama inavyo kuwa kwenye maduka mengi. Mikoani wanatoa hela sana na hapo unapata float. Mjini wana deposit sana hivyo una pata cash ya kuzungusha mkoani.
Biashara inauzwa as a going concern. yaani jinsi inavyo endelea, owners wanabadilika na mwingine anaingia nakuendelea au kufanya mabadiliko yanayo mpendezeni yeye.
Hatuuzi vocha, simu, betri, au makasha ya simu. Hizi ni biashara unaweza kufanya kwenye hayo maduka ukaongeza faida
kwa kiwango kizuri. Maduka manne yanafaa sana kwa kuweka pia mtandao wa internet, yote yanafaa kuweka photocopy, typing, printing n.k Kama ukiamua kuweka float m20 na zaidi na uongeze biashara ya simu na vocha nina uhakika faida kwa mwezi haita pungua m10 kwa mwezi. Hii biashara ina kuwezesha kupata mikopo mikubwa benki mfano m100 na zaidi kwa ajili ya mzunguko wake wa hela. Hivyo tusema future yake ni nzuri sana.
Mapungufu ya biashara.
Kazi ni kubwa kwa sababu lazima u balance hela kila siku ku hakikisha hamna short. Hiyo lazima uwe mtu makini kwenye
hesabu. Hata wafanya kazi wakiwa wazuri kama haupo makini unawapa nafasi kudokoa. Kila baada ya mda usio mrefu zunguka maduka yote. Hii inachosha. Unapo weka stock na kupanua biashara itabidi kuweka walinzi na kuongeza wahudumu. Ni vizuri uwe na system ya kuweka fedha kiasi kisicho kikubwa kwa wakati mmoja na pia uendelee kuboresha maduka kwa ajili ya security ya fedha jinsi kazi zinavyo endelea.
Sababu ya kuuza hii biashara. Wenyewe wanasafiri kwenda nje ya nchi. kwa mda wa mwezi mmoja watakusaidia ku-take over na kuelewa kazi.