Biashara gani Mwanachuo anaweza kufanya akiwa Chuoni?

Wakusolve

Senior Member
Jul 30, 2020
191
138
Wakuu habari zenu,

Natumaini ni wazima wa afya, poleni na majukumu ya kulijenga taifa. Lengo la bandiko hili ni kusaidia vijana walioko chuo na wanaotarajia kwenda chuo. Hoja ni kitu gani au biashara gani ambayo anaweza kufanya akiwa chuoni.

Asante, karibuni kwa maoni yenu.
 
Sambaza ubuyu wa Babu issa, hakika utapiga pesa.......weka kibanda cha kuuza ubuyu,andika ubuyu wa Babu issa,uza kuanzia robo na kuendelea....hakika mademu wote utawashika,pia kwa wanaume pesa zao utazipata kupitia mademu..... hahaaaha nakutania ndugu si unajua napenda utani.
 
Kwa upande wa vijana wa kiume nakumbuka nikiwa chuoni nlikuwa na laptop yenye game ya fifa, wengine walikuwa na laptop ila zilikuw ahazina uwezo mkubwa kama yangu.

Basi chumbani kwangu kila mda kulikuwa kumejaa watu wanacheza fifa.

Nlimaliza chuo na sikuwahi kunufaika nilidhani hii ni kufurahishana tu.

majuzi nimecheki channel flan huko kenya naona hii imekuwa biashara, vijana wameenda mbali zaidi kuweka Play station na Tv badala ya laptop.

Niliona mwenye kile chumba ni mwanachuo wenzake wakija kucheza inabidi walipe, Mechi moja sikujua anachaji sh ngap ila unaweza kuchaji mia tano kwa mechi moja ya dakika kumi, hapa kwa saa zinaweza kuwa mechi nne ukapata buku 2.

Laiti ningeyapata hayo mawazo nikiwa cguo basi ningetekeleza.

 
You still m
Kwa upande wa vijana wa kiume nakumbuka nikiwa chuoni nlikuwa na laptop yenye game ya fifa, wengine walikuwa na laptop ila zilikuw ahazina uwezo mkubwa kama yangu.

Basi chumbani kwangu kila mda kulikuwa kumejaa watu wanacheza fifa.

Nlimaliza chuo na sikuwahi kunufaika nilidhani hii ni kufurahishana tu.

majuzi nimecheki channel flan huko kenya naona hii imekuwa biashara, vijana wameenda mbali zaidi kuweka Play station na Tv badala ya laptop.

Niliona mwenye kile chumba ni mwanachuo wenzake wakija kucheza inabidi walipe, Mechi moja sikujua anachaji sh ngap ila unaweza kuchaji mia tano kwa mechi moja ya dakika kumi, hapa kwa saa zinaweza kuwa mechi nne ukapata buku 2.

Laiti ningeyapata hayo mawazo nikiwa cguo basi ningetekeleza.
Your misses information and still miss information...umeandika as if umeshangaa kuwa kumbe PS kuna watu wanafanya Biashara nawakati PS ni Biashara toka 2003 huko.

Then uwawekee wanachuo PC wacheze game 500 hakuna utayempata.
 
Biashara nyingine ni ku print,

Hii inalipa maana stationery nyingi hufungwa saa moja jioni hivyo wewe ukiwa unatoa huduma muda wowote basi utazoeleka haraka maana muda mwengine mchana hakuna umeme hadi usiku na watu kibao wanataka ku print assignment zao.

Printer ya bei poa ni hp 315 inktank, niliona inauzwa duka la "discount kubwa" pale kariakoo kwa 290,000/= ukiinunua utaweza kuprint hadi karatasi elf 8, na wino ukiisha kuna vichupa wanauza elf 4 unajaza.

Rim ina karatasi 500 na inauzwa tuseme elfu 10 zile nzuri, ukifanikiwa ku print hio rim nzima kwa bei ya shilingi 100 kwa karatasi moja basi una elf 50 ukitoa gharama ya rim tayari faida elf 40, ikifika jioni stationery zikiwa zimefungwa unachaji hata 200 kwa page moja.

Pia utaweza kuprint hata rangi, hususani kwenye cover page za assignment ile nembo ya chuo ina rangi, wengine watapenda kutoa kopi ya rangi watie nakshi .

Pia hii printer unaweza ku scan documents kama vyeti, unaweza kuprint picha zile za passpprt size na hata zile za kuweka kwenye albamu, So ukijiongeza waweza kuitumia kwa mambo kibao.

Hii uzuri wake ni kwamba hata mwanafunzi mwenye hii printer ananufaika kujiprintia kazi lakini pia inakuwa kitega uchumi.
 
You still m

Your misses information and still miss information...umeandika as if umeshangaa kuwa kumbe PS kuna watu wanafanya Biashara nawakati PS ni Biashara toka 2003 huko.

Then uwawekee wanachuo PC wacheze game 500 hakuna utayempata.
Mkuu hata grammer tu inakuyumbisha, Umesoma chuo gani??? eti "Your misses information" 😁😁😁

Sijajua chuo ulichosoma lakini wanafunzi wanapenda sana games hasa fifa hii kitu nakumbuka kulikuwa na mashindano kabisa ya hostel flan na fulani, Pia watu wanacheza sana kwa kuwekeana hela, Ila inategemeana na chuo ulichosomea mkuu
 
Biashara nyingine ni ku print,

Hii inalipa maana stationery nyingi hufungwa saa moja jioni hivyo wewe ukiwa unatoa huduma muda wowote basi utazoeleka haraka maana muda mwengine mchana hakuna umeme hadi usiku na watu kibao wanataka ku print assignment zao.

Printer ya bei poa ni hp 315 inktank, niliona inauzwa duka la "discount kubwa" pale kariakoo kwa 290,000/= ukiinunua utaweza kuprint hadi karatasi elf 8, na wino ukiisha kuna vichupa wanauza elf 4 unajaza.

Rim ina karatasi 500 na inauzwa tuseme elfu 10 zile nzuri, ukifanikiwa ku print hio rim nzima kwa bei ya shilingi 100 kwa karatasi moja basi una elf 50 ukitoa gharama ya rim tayari faida elf 40, ikifika jioni stationery zikiwa zimefungwa unachaji hata 200 kwa page moja.

Pia utaweza kuprint hata rangi, ila mtu akitaka page iwe ya rangi mchaji hata 300, Na pia hii printer unaweza kuprint picha zile za passpprt size na hata zile za kuweka kwenye albamu hapa utachaji hata jero.

Hii uzuri wake ni kwamba hata mwanafunzi mwenye hii printer ananufaika kujiprintia kazi lakini pia inakuwa kitega uchumi.
Hizo bei unamwekea mwanachuo gani mjomba? Mimi hapa naprint kwa gharama ya 100 kwa kuwa sipendi uswahili kwenye stationary.

Na mara nyingi group assignment naprint mimi hivyo cover page na mengine yapo kwenye kompyuta za stationary ile. Sharti langu ni moja, huwa nataka niachiwe nifanye kazi mwenyewe kisha nilipe.

Tofauti na hapo, kuna watu wanaprint kwa 70 mpaka 50 maana ushindani ni mkubwa. Hiyo 200 hupati mtu kabisa. Kwanza tangu nianze chuo ni mara moja tu umeme ulishawahi nizuia kuprint.
 
Mkuu hata grammer tu inakuyumbisha, Umesoma chuo gani??? eti "Your misses information" 😁😁😁

Sijajua chuo ulichosoma lakini wanafunzi wanapenda sana games hasa fifa hii kitu nakumbuka kulikuwa na mashindano kabisa ya hostel flan na fulani, Pia watu wanacheza sana kwa kuwekeana hela, Ila inategemeana na chuo ulichosomea mkuu
Hizo ni Error za keyboard siombi kazi hapa, wanacheza mpaka mashindano just for fun na mpaka pesa wanawekeana ila uwezi mkodisha mtu...labda uwe uwajui wanachuo sio kukupa jero hata 100 hakupi mtu.
 
Kwa upande wa vijana wa kiume nakumbuka nikiwa chuoni nlikuwa na laptop yenye game ya fifa, wengine walikuwa na laptop ila zilikuw ahazina uwezo mkubwa kama yangu.

Basi chumbani kwangu kila mda kulikuwa kumejaa watu wanacheza fifa.

Nlimaliza chuo na sikuwahi kunufaika nilidhani hii ni kufurahishana tu.

majuzi nimecheki channel flan huko kenya naona hii imekuwa biashara, vijana wameenda mbali zaidi kuweka Play station na Tv badala ya laptop.

Niliona mwenye kile chumba ni mwanachuo wenzake wakija kucheza inabidi walipe, Mechi moja sikujua anachaji sh ngap ila unaweza kuchaji mia tano kwa mechi moja ya dakika kumi, hapa kwa saa zinaweza kuwa mechi nne ukapata buku 2.

Laiti ningeyapata hayo mawazo nikiwa cguo basi ningetekeleza.
Kwa sasa wapenda game wanamiliki laptop zenye graphics ya >2GB. Hakuna mtu atakuja kukodisha laptop ili acheze game, ukitaka kupata hela miliki PS 4 na sasa wenye pesa ndefu wataenda PS 5.
 
Hizo bei unamwekea mwanachuo gani mjomba? Mimi hapa naprint kwa gharama ya 100 kwa kuwa sipendi uswahili kwenye stationary. Na mara nyingi group assignment naprint mimi hivyo cover page na mengine yapo kwenye kompyuta za stationary ile. Sharti langu ni moja, huwa nataka niachiwe nifanye kazi mwenyewe kisha nilipe.
Tofauti na hapo, kuna watu wanaprint kwa 70 mpaka 50 maana ushindani ni mkubwa. Hiyo 200 hupati mtu kabisa. Kwanza tangu nianze chuo ni mara moja tu umeme ulishawahi nizuia kuprint.
Mkuu binafsi nimeshauri owe hio shilingi 100 kwa sababu hii ndio bei nayoiona stationery nyingi, Ila labda kama upo dar huko kuna ushindani mkubwa, Kwa hapa nilipo na nilikosomea chuo bei ni hio niliyopendekeza (100/=)

Hiyo 200 nimeweka wazi kabisa inabidi uichaji katika mazingira ambayo hakuna mbadala na hata kama upo basi una gharama zaidi, Nimetoa mfano kwmba mida ya jioni stationery zikifungwa kuna watu bado wanahitaji kuprint na hapo umaweza kuchaji 200, ila pia umeme ukizingua na ukawa wa kirudi usiku basi na hapo hutapata ushindani n utaweza kuamua bei iwe 200

Sio kila mwanachuo anasomea mazingira uliyopp wewe ambayo umeme upo kwa uhakika, saizi moja haiwezi kutosha kote, Kuna vyuo umeme ni tatizo.
 
Hizo ni Error za keyboard siombi kazi hapa, wanacheza mpaka mashindano just for fun na mpaka pesa wanawekeana ila uwezi mkodisha mtu...labda uwe uwajui wanachuo sio kukupa jero hata 100 hakupi mtu.
Mkuu naomba ujisemeage moyoni "sina hela" badala ya kufungua kinywa mbele ya watu kuropoka "hatuna hela",
 
Kwa sasa wapenda game wanamiliki laptop zenye graphics ya <2GB. Hakuna mtu atakuja kukodisha laptop ili acheze game, ukitaka kupata hela miliki PS 4 na sasa wenye pesa ndefu wataenda PS 5.
Hivi wa wapi wewe, unajua hata unachoandika 🙄🙄

Naona umekaa sana negatively

Hivi kwa akili yako umeoma mtu anaependa game na yupo serious eti anunue laptop yenye graphocs chini ya gb 2,

Ni vyema ukakaa kimya tu mkuu kuliko kufungua kinywa na kuuacha uchi ujinga wako ambao huenda ukikaa kimya utafichika.

Unakuta hata hio sign uliyoweka ya less than hata hujui maana yake.
 
Mkuu naomba ujisemeage moyoni "sina hela" badala ya kufungua kinywa mbele ya watu kuropoka "hatuna hela",
Wapi nimesema hawalipi kwasababu hawana pesa hata wapokee ma Boom ya Million leo hakuna utaye mkodisha.
1)Uwana..most ya hao wanaocheza ni washkaji/marafiki.
2)PC ni nyingi...Access ya kupata PC kubwa how come watoe pesa.
3)Team..katika Gamer wanne mmoja kati yao anayo PC how come wakodi kwako.

Nk nk nk
 
Wapi nimesema hawalipi kwasababu hawana pesa hata wapokee ma Boom ya Million leo hakuna utaye mkodisha.
1)Uwana..most ya hao wanaocheza ni washkaji/marafiki.
2)PC ni nyingi...Access ya kupata PC kubwa how come watoe pesa.
3)Team..katika Gamer wanne mmoja kati yao anayo PC how come wakodi kwako.

Nk nk nk

Haya mkuu umeshinda 🙄🙄 naona kubishana na mshamba ni kumuongezea kiburi cha kuwa mjinga hata akiujua ukweli.

Sema kuwa inspired, dont hate

 
Mkuu binafsi nimeshauri owe hio shilingi 100 kwa sababu hii ndio bei nayoiona stationery nyingi, Ila labda kama upo dar huko kuna ushindani mkubwa, Kwa hapa nilipo na nilikosomea chuo bei ni hio niliyopendekeza (100/=)

Hiyo 200 nimeweka wazi kabisa inabidi uichaji katika mazingira ambayo hakuna mbadala na hata kama upo basi una gharama zaidi, Nimetoa mfano kwmba mida ya jioni stationery zikifungwa kuna watu bado wanahitaji kuprint na hapo umaweza kuchaji 200, ila pia umeme ukizingua na ukawa wa kirudi usiku basi na hapo hutapata ushindani n utaweza kuamua bei iwe 200

Sio kila mwanachuo anasomea mazingira uliyopp wewe ambayo umeme upo kwa uhakika, saizi moja haiwezi kutosha kote, Kuna vyuo umeme ni tatizo.
Wakati unasema hukutaja ni sehemu gani, wakati najibu sikutaja niko sehemu gani. Kila mtu kajibu kwa upande wake na atakuwa kapatia. Anayesoma asipozingatia location ambayo haijatajwa anaweza jikuta anafungua stationary Dar na atoze 200.
 
Hivi wa wapi wewe, unajua hata unachoandika

Naona umekaa sana negatively

Hivi kwa akili yako umeoma mtu anaependa game na yupo serious eti anunue laptop yenye graphocs chini ya gb 2,

Ni vyema ukakaa kimya tu mkuu kuliko kufungua kinywa na kuuacha uchi ujinga wako ambao huenda ukikaa kimya utafichika.

Unakuta hata hio sign uliyoweka ya less than hata hujui maana yake.
Tatizo lako unataka ligi kwenye vitu ambavyo hata hakuna ulazima. Hayo matusi naweza sana lakini inategemea, hapa sioni sababu ya kukujibu kwa matusi.

Kingine, kama unahisi sina akili kisa typing errors kwenye hii reply yako umekosea mara tatu. Je, niseme wewe ni kichwa maji kisa umekosea typing?
 
  • Thanks
Reactions: amu
Wakuu habari zenu,

Natumaini ni wazima wa afya, poleni na majukumu ya kulijenga taifa. Lengo la bandiko hili ni kusaidia vijana walioko chuo na wanaotarajia kwenda chuo. Hoja ni kitu gani au biashara gani ambayo anaweza kufanya akiwa chuoni.

Asante, karibuni kwa maoni yenu.
Mwnachuo anaweza akawaza biashara yeyote kulingana na uwezo wake wa kushika vitu viwili kwa wakati mmoja
 
Kama ni wa Kiume Kama utakuwa na interest na hii biashara ya kupaka Rangi kucha wadada wa chuo basi hautojuta kuifanya ukiwa mazingira ya chuoni mana utakuwa unafanya mobile service yaani unawafata katika hostel zao humo humo unatoa huduma,kwa hela hizi za kula kwako na za kufanyia mambo mengine zitakuwa hazikusumbui

Kitu cha kwanza kama hauna ujuzi wowote wa kupaka rangi kucha unaweza ukamtafuta mtu mpaka rangi eneo ulilopo ukamwomba akufundishe,wengine wanaweza kukufundisha bure au ukalipia mafunzo inategemea na mtu utakae kutana nae.

Kama utakuwa na kichwa ya haraka kushika mambo basi ndani ya mwezi mmoja/miwili unaweza ukawa ushajua kila kitu about basics za upakaji rangi kucha na ukajua mahitaji yapi yanatakiwa katika hii biashara ya kuanza nayo.Na ukawa tayari kwa kuanza rasmi shughuli zako hapo chuoni.Pia
YouTube toturial zipo nyingi ya kitu kwa beginners.

NOTE: Biashara hii ukiifanya kwenye misingi sahihi kama biashara zingine pesa utaiona,ila kama utaamua ufanye hii biashara upate totozi uwale kweli utawapata tu. Mana ina changamoto nyingi ni wewe tu kusimama kwenye misingi yako ya biashara..

Changamoto nyingine ipo kwenye ku manage muda wa masomo chuoni na kufanya hii inshu mana inataka moyo wa kuweza ku manage muda wa masomo na hii harakati,

Unaweza mwenyewe ukatenga muda wako wa kupiga kazi kwamba kila ijumaa, jumamosi na jumapili unaenda kwenye hostels za kike unapiga kazi zako au katikati ya week pale kama hakuna kipindi class unaenda kupiga hii harakati hapo itategemea na time table yako 30000 au zaidi kwa week hukosi kupata.

NOTE: Kama ndo unaenda kuanza first year yasome kwanza mazingira ya hapo chuoni kwenu yapoje kisha ujitathimini mwenyewe mana unaweza ukawekeza nguvu sana kuitafuta pesa ukanogewa na pesa afu nguvu ya darasani ukaipoteza.



Sijaandika kwa mpangilio mzuri ila nazani utakuwa umepata at least kitu hapo,Mana na uzoefu na hii Biashara hapa chuoni kwetu.



"Biashara yoyote ya Urembo inayomuhusu Mwanamke inalipa"
 
Biashara nyingine ni ku print,

Hii inalipa maana stationery nyingi hufungwa saa moja jioni hivyo wewe ukiwa unatoa huduma muda wowote basi utazoeleka haraka maana muda mwengine mchana hakuna umeme hadi usiku na watu kibao wanataka ku print assignment zao.

Printer ya bei poa ni hp 315 inktank, niliona inauzwa duka la "discount kubwa" pale kariakoo kwa 290,000/= ukiinunua utaweza kuprint hadi karatasi elf 8, na wino ukiisha kuna vichupa wanauza elf 4 unajaza.

Rim ina karatasi 500 na inauzwa tuseme elfu 10 zile nzuri, ukifanikiwa ku print hio rim nzima kwa bei ya shilingi 100 kwa karatasi moja basi una elf 50 ukitoa gharama ya rim tayari faida elf 40, ikifika jioni stationery zikiwa zimefungwa unachaji hata 200 kwa page moja.

Pia utaweza kuprint hata rangi, hususani kwenye cover page za assignment ile nembo ya chuo ina rangi, wengine watapenda kutoa kopi ya rangi watie nakshi .

Pia hii printer unaweza ku scan documents kama vyeti, unaweza kuprint picha zile za passpprt size na hata zile za kuweka kwenye albamu, So ukijiongeza waweza kuitumia kwa mambo kibao.

Hii uzuri wake ni kwamba hata mwanafunzi mwenye hii printer ananufaika kujiprintia kazi lakini pia inakuwa kitega uchumi.
Nimekuelewa mnooh,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom