Mwanakili90
JF-Expert Member
- Nov 24, 2010
- 1,568
- 246
17 Oktoba 2011 12:49
Rais wa Liberia Ellen Johnson-Sirleaf amesema
ameridhia kukabiliana na duru ya pili ya
uchaguzi dhidi ya aliyekuwa mwanadiplomasia
wa umoja wa mataifa Winston Tubman. Huku takriban kura zote zikiwa
zimeshahesabiwa, Bi Sirleaf alipata kura nyingi
zaidi lakini alishindwa kuvuka asilimia 50
inayotakiwa kupata ushindi. Bw Tubman alisema atagombea tena katika duru
hiyo baada ya chama chake kudai kuwepo
udanganyifu na kudai kujitoa. Huu ni uchaguzi wa pili Liberia tangu kumalizika
kwa miaka 14 ya vita vya wenyewe kwa
wenyewe mwaka 2003. Bi Sirleaf, ambaye alipewa tuzo ya amani ya
Nobel wiki iliyopita, alishinda uchaguzi wa
mwaka 2005 na kuwa mwanamke wa kwanza
Mwafrika kuchaguliwa kuwa rais. Alimshinda aliyekuwa mcheza soka George
Weah, ambaye kwa sasa ni mgombea mwenza
wa Bw Tubman. Bi Sirleaf alisema yuko tayari kwa ushindani
lakini pia alikuwa ana uhakika wa kushinda. Ikiwa aslimia 96 ya kura zote zikiwa
zimehesabiwa, yeye ana asilimia 44 dhidi ya 32
za Bw Tubman, tume ya uchaguzi imetangaza.
Waliojitokeza kupiga kura ni asilimia 74. "Duru ya pili ni karibu sana," alisema James
Fromayah kutoka tume ya taifa ya uchaguzi
(NEC). Imepangwa kufanyika Novemba 8.
Source:BBC
Rais wa Liberia Ellen Johnson-Sirleaf amesema
ameridhia kukabiliana na duru ya pili ya
uchaguzi dhidi ya aliyekuwa mwanadiplomasia
wa umoja wa mataifa Winston Tubman. Huku takriban kura zote zikiwa
zimeshahesabiwa, Bi Sirleaf alipata kura nyingi
zaidi lakini alishindwa kuvuka asilimia 50
inayotakiwa kupata ushindi. Bw Tubman alisema atagombea tena katika duru
hiyo baada ya chama chake kudai kuwepo
udanganyifu na kudai kujitoa. Huu ni uchaguzi wa pili Liberia tangu kumalizika
kwa miaka 14 ya vita vya wenyewe kwa
wenyewe mwaka 2003. Bi Sirleaf, ambaye alipewa tuzo ya amani ya
Nobel wiki iliyopita, alishinda uchaguzi wa
mwaka 2005 na kuwa mwanamke wa kwanza
Mwafrika kuchaguliwa kuwa rais. Alimshinda aliyekuwa mcheza soka George
Weah, ambaye kwa sasa ni mgombea mwenza
wa Bw Tubman. Bi Sirleaf alisema yuko tayari kwa ushindani
lakini pia alikuwa ana uhakika wa kushinda. Ikiwa aslimia 96 ya kura zote zikiwa
zimehesabiwa, yeye ana asilimia 44 dhidi ya 32
za Bw Tubman, tume ya uchaguzi imetangaza.
Waliojitokeza kupiga kura ni asilimia 74. "Duru ya pili ni karibu sana," alisema James
Fromayah kutoka tume ya taifa ya uchaguzi
(NEC). Imepangwa kufanyika Novemba 8.
Source:BBC