Beyond Ufipa, Lumumba Political Discourses

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
Kwanini Tusiamue kufanya itikadi ya Trump kuwa "Wrong" Kwa kujiongeza na kufikiri zaidi ya kujibizana wewe wa lumumba wewe! wewe wa ufipa!!

Ndugu watanzania wenzangu, tunatakiwa tufahamu kuwa dunia haitusubiri na muda tulio nao duniani ni mfupi mno. Sasa tukiamua kujifungia kwenye kaduara kadogo mno ka kufikiri wakati wenzetu wanatanua wigo wa kufikiri na kufanya maamuzi yenye impact za ajabu duniani na kuyatekeleza kwa kasi ndani na nje ya nchi zao ili kutimiza dhima ya maisha yao; huo utakuwa ni mzigo wetu wenyewe kama watanzania. Tutakuwa tumeamua kuwa mfano wa sisimizi aliyeingia kwenye kifuu chenye maji akadhani anaogelea kwenye bahari, kumbe yuko kwenye dunia ya peke yake!.

Dunia ni pana sana na ina vitu vingi sana ila kwa bahati mbaya Watanzania wengi (si wote) tunafikiri Dunia ni Ufipa na Lumumba, Chadema na CCM, kisha tushamaliza kila kitu, kinachofuata udaku wa kiongozi gani kamjibu nani au nani kamjibu kiongozi gani.

Ni lazima sasa Watanzania tuelewe kuwa ili kuweza kupata mabadiliko na maendeleo tunayoyataka na nchi yetu iwe bora kuliko hapo kabla, ni lazima sisi wenyewe kwanza kubadilika kwanza, na hayo yote huanzia kwenye fikra zetu.

Ndugu watanzania wenzangu; tusipoamua kubadilika hakuna kitakachobadilika juu yetu. Hiyo ni kanuni ya kimaumbile. Tusichoke kujifunza na tunayojifunza tuyafanyie kazi.Tusione aibu kubadilika kwani ndio njia pekee itakayotuwezesha kwenda mbele kwa kasi. Si nchi,si vyama vya siasa au kitu chochote kitakachokuwa bora ikiwa hatutabadilisha fikra zetu .

Tunasema eti karne ya 15, Afrika na Ulaya zilikuwa na maendeleo yanayokaribia kulingana lakini hatutafakari kwa kina kwamba kwa nini tupo hivi leo, tunafanya nini na wengine wanafanya nini na kwa nini. Tunapenda sana simple things, decisions & conclusions kwenye mambo nyeti.Tunasema Waafrika hatupendani kisha tunaishia hapo. Tunasema ukosefu wa ajira kwa vijana nchini ni bomu linalosubiri kulipuka kisha tunaishia hapo.Tunasema uzalendo umepotea Tanzania lakini hatupigi hatua mbele kujiuliza kwa nini na tufanye nini. Tunasema watanzania hatupendi kusoma vitabu halafu tunaishia hapo.Tunasema watanzania hatupendi kujadili mada za maana na kutoa hoja zenye manufaa kwetu na kwa watanzania wenzetu kisha tunaishia hapo then tunasubiria tukio la siku! n.k.

Kama mtu hajui aendako hawezi kupotea. Popote alipo au atakapokuwa itakuwa ni sawa. Kama mtu hajui au hana uhakika wa nini atakacho, chochote apatacho ni sawa.Kokote atakapoanzia, kokote atakapopita na atakapoishia ni sawa tu. Upepo ukiende kushoto, ataenda ukirudi kulia atarudi na ukiisha atatulia alipo.

Ni lazima wanadamu tuishi maisha yenye dhima "live with purpose" Tujue kwa nini tunaishi? tunataka nini? na tujiwekee misingi ya kufikia kile anachokitaka. Watanzania wengi hili bado hatujalielewa na athari yake ni kwamba tukiamka asubuhi tunaangalia nini kinatokea; tuanaenda nacho hadi jioni, tukiamka siku ya pili tunaangalia tena nini kinatokea tunaenda nacho na cha jana yake tushakisahau hivyo hivyo hadi kila mmoja wetu muda wake wa kuondoka duniani unafika, anaondoka naye anasahaulika.

Sasa kwa kuishi maisha ya namna hiyo, tusitegemee kupata matokeo ya maana sana wala kuwa na mchango mkubwa kwenye kuibadili nchi hii na hali ya maisha ya watu wake kwani katika mazingira hayo; chochote kitokeacho kwetu ni sawa kwa kuwa hatuna muelekeo maalum.

Mathalan, kuna mambo ambayo watanzania kila tukiamka asubuhi tunayalalamikia lakini hatuchukui hatua yoyote ya maana, au hatua tunazochukua ni zile zile na matokeo yanakuwa yale yale lakini wala hatugutuki; tunaendelea vile vile tu! tukiamini ipo siku mambo yatabadilika tu bila kujua kuwa kufanya hivyo ni kinyume kabisa na kanuni za kimaumbile ambapo ili binadamu afanikiwe ni lazima a- comply na kanuni hizo za kimaumbile.

Pamoja na maneno yakuudhi aliyotuambia Mzee Trumph; tunayo mambo ya kujifunza kutoka kwake hasa alipoeleza baadhi ya mambo yaliyoifanya Amerika na Ulaya Kuendelea na baadhi ya matatizo aliyotueleza kuwa watu weusi tunayo ikiwemo tabia ya kupenda kutafuta zilipo ndizi mbivu badala ya kuivisha za kwetu.

Kama Watanzania tukiamua kubadilika na kuachana na ushabiki huu usiotusaidia na tukajiongeza kidogo; kila kitu kinachotuhusu kitabadilika na kama tukiendelea kuwa kama tulivyo hakuna kitakachobadilika.
 
Mkuu, shida yako ni kwamba unataka kutulazimisha sisi Watanzania wapiga porojo, wambea, wapenda udaku, tusiopenda kujisomea...tufikiri kwa kina na nje ya boksi. Hilo haliwezekani kwa sababu mfumo wetu wa elimu, kijamii na hata kitamaduni haujatuandaa kuwa watu wa kuhoji na kufikiri mambo kwa undani. Kama nilivyoona hapo juu we jiandae kutukanwa tu!

Weka mada nyepesi nyepesi tujadili hapa ohoooo ‍♂️‍♂️‍♂️‍♂️‍♂️‍♂️‍♂️‍♂️‍♂️
 
Mkuu, shida yako ni kwamba unataka kutulazimisha sisi Watanzania wapiga porojo, wambea, wapenda udaku, tusiopenda kujisomea...tufikiri kwa kina na nje ya boksi. Hilo haliwezekani kwa sababu mfumo wetu wa elimu, kijamii na hata kitamaduni haujatuandaa kuwa watu wa kuhoji na kufikiri mambo kwa undani. Kama nilivyoona hapo juu we jiandae kutukanwa tu!

Weka mada nyepesi nyepesi tujadili hapa ohoooo ‍♂️‍♂️‍♂️‍♂️‍♂️‍♂️‍♂️‍♂️‍♂️
Mkuu nijambo gumu sana na linalohitaji uvumilivu mkubwa. hata hivyo tusiogope wala kusita kutumia chochote tulicho nacho ku influence positive changes. Hatutafanikiwa kwa haraka, hatutaungwa mkono na watu wengi kwa sababu ya changamoto ya uelewa, tutapata vikwazo vingi lakini ipo siku tutafanikiwa.

Hata kama umri wetu utapita kabla hatujafanikiwa, lakini hatua tutakayopiga watakuwepo wengine wa kuendelezea hapo. Hata Trumph anayeiringia Amerika, ameikuta ikiwa imefikishwa hapo ilipo na watu wengine walioishi zamani huko. Wakati fulani unapoamua kuotesha miti ya matunda, unaweza kufa kabla haijaanza kuzaa na watakao kula matunda wakawa kizazi cha tatu.
 
Kijana , adui wa kwanza wa nchi hii ni ccm , wa pili ni Shetani , katika nchi hii huwezi kupiga hatua yeyote bila kuondosha hawa watu , hebu fikiria leo hii bado tunanunua binadamu ?
Hata humu jf huwezi ukachangia kitu cha maana sababu ya CCM? Mzee Lowasa alivyo kuwa CCM alikuwa ni zaidi ya Shetani alivyokuja kwenu amekuwa zaidi ya malaika? Nyalandu akiwa CCM alikuwa fisadi amekuja kwenu amekuwa mtu mwema? Mtulya akiwa kwenu alikuwa mtu ameenda CCM amekuwa zaidi ya Shetani! Hii ni aibu kwa nchi na kwa Afrika kuwa na watu wenye akili kama zako na wenzako. Any way sio kwamba hamjui! Tatizo Unafiki! ipo siku matunda ya mnachokipanda yatapatikana kwani halimtokei mtu isipokua lile alilootesha kwa mikono yake.

Labda nikuulize swali moja dogo tu. Ndani ya chama chenu, ni kitu gani hasa mnachofanya ili kuhakikisha kuwa viongozi wa chama chenu wanakuwa upgraded na kuwa bora zaidi ya wengine? au mtu akishakuja kwenu tu tayari malaika? Upuuzi mkubwa. Sory! unafiki mkubwa.
 
Hata humu jf huwezi ukachangia kitu cha maana sababu ya CCM? Mzee Lowasa alivyo kuwa CCM alikuwa ni zaidi ya Shetani alivyokuja kwenu amekuwa zaidi ya malaika? Nyalandu akiwa CCM alikuwa fisadi amekuja kwenu amekuwa mtu mwema? Mtulya akiwa kwenu alikuwa mtu ameenda CCM amekuwa zaidi ya Shetani! Hii ni aibu kwa nchi na kwa Afrika kuwa na watu wenye akili kama zako na wenzako. Any way sio kwamba hamjui! Tatizo Unafiki! ipo siku matunda ya mnachokipanda yatapatikana kwani halimtokei mtu isipokua lile alilootesha kwa mikono yake.

Labda nikuulize swali moja dogo tu. Ndani ya chama chenu, ni kitu gani hasa mnachofanya ili kuhakikisha kuwa viongozi wa chama chenu wanakuwa upgraded na kuwa bora zaidi ya wengine? au mtu akishakuja kwenu tu tayari malaika? Upuuzi mkubwa. Sory! unafiki mkubwa.
Sasa umejidghirisha kuwa wewe ni wa lumumba. Akili kakabidhiwa think tank Bashite na mtekelezeji chakubanga. Mambo yote ni ndani ya sanduku la ufipa na lumumba hatuchomoki. Wenye akili wanasubiri wakati mwafaka kuepuka hoja za bunduki.
 
Hata humu jf huwezi ukachangia kitu cha maana sababu ya CCM? Mzee Lowasa alivyo kuwa CCM alikuwa ni zaidi ya Shetani alivyokuja kwenu amekuwa zaidi ya malaika? Nyalandu akiwa CCM alikuwa fisadi amekuja kwenu amekuwa mtu mwema? Mtulya akiwa kwenu alikuwa mtu ameenda CCM amekuwa zaidi ya Shetani! Hii ni aibu kwa nchi na kwa Afrika kuwa na watu wenye akili kama zako na wenzako. Any way sio kwamba hamjui! Tatizo Unafiki! ipo siku matunda ya mnachokipanda yatapatikana kwani halimtokei mtu isipokua lile alilootesha kwa mikono yake.

Labda nikuulize swali moja dogo tu. Ndani ya chama chenu, ni kitu gani hasa mnachofanya ili kuhakikisha kuwa viongozi wa chama chenu wanakuwa upgraded na kuwa bora zaidi ya wengine? au mtu akishakuja kwenu tu tayari malaika? Upuuzi mkubwa. Sory! unafiki mkubwa.
Nilitaka uingie kingi kama hivi ulivyojiingiza , unao upande bali ulitaka kutumia JF ili kupata uteuzi kwa hoja zako za kipuuzi za kichaka cha uzalendo .

Natangaza kukudharau katika kipindi chako chote kilichosalia hapa duniani .
 
Kwanini Tusiamue kufanya itikadi ya Trump kuwa "Wrong" Kwa kujiongeza na kufikiri zaidi ya kujibizana wewe wa lumumba wewe! wewe wa ufipa!!

Ndugu watanzania wenzangu, tunatakiwa tufahamu kuwa dunia haitusubiri na muda tulio nao duniani ni mfupi mno. Sasa tukiamua kujifungia kwenye kaduara kadogo mno ka kufikiri wakati wenzetu wanatanua wigo wa kufikiri na kufanya maamuzi yenye impact za ajabu duniani na kuyatekeleza kwa kasi ndani na nje ya nchi zao ili kutimiza dhima ya maisha yao; huo utakuwa ni mzigo wetu wenyewe kama watanzania. Tutakuwa tumeamua kuwa mfano wa sisimizi aliyeingia kwenye kifuu chenye maji akadhani anaogelea kwenye bahari, kumbe yuko kwenye dunia ya peke yake!.

Dunia ni pana sana na ina vitu vingi sana ila kwa bahati mbaya Watanzania wengi (si wote) tunafikiri Dunia ni Ufipa na Lumumba, Chadema na CCM, kisha tushamaliza kila kitu, kinachofuata udaku wa kiongozi gani kamjibu nani au nani kamjibu kiongozi gani.

Ni lazima sasa Watanzania tuelewe kuwa ili kuweza kupata mabadiliko na maendeleo tunayoyataka na nchi yetu iwe bora kuliko hapo kabla, ni lazima sisi wenyewe kwanza kubadilika kwanza, na hayo yote huanzia kwenye fikra zetu.

Ndugu watanzania wenzangu; tusipoamua kubadilika hakuna kitakachobadilika juu yetu. Hiyo ni kanuni ya kimaumbile. Tusichoke kujifunza na tunayojifunza tuyafanyie kazi.Tusione aibu kubadilika kwani ndio njia pekee itakayotuwezesha kwenda mbele kwa kasi. Si nchi,si vyama vya siasa au kitu chochote kitakachokuwa bora ikiwa hatutabadilisha fikra zetu .

Tunasema eti karne ya 15, Afrika na Ulaya zilikuwa na maendeleo yanayokaribia kulingana lakini hatutafakari kwa kina kwamba kwa nini tupo hivi leo, tunafanya nini na wengine wanafanya nini na kwa nini. Tunapenda sana simple things, decisions & conclusions kwenye mambo nyeti.Tunasema Waafrika hatupendani kisha tunaishia hapo. Tunasema ukosefu wa ajira kwa vijana nchini ni bomu linalosubiri kulipuka kisha tunaishia hapo.Tunasema uzalendo umepotea Tanzania lakini hatupigi hatua mbele kujiuliza kwa nini na tufanye nini. Tunasema watanzania hatupendi kusoma vitabu halafu tunaishia hapo.Tunasema watanzania hatupendi kujadili mada za maana na kutoa hoja zenye manufaa kwetu na kwa watanzania wenzetu kisha tunaishia hapo then tunasubiria tukio la siku! n.k.

Kama mtu hajui aendako hawezi kupotea. Popote alipo au atakapokuwa itakuwa ni sawa. Kama mtu hajui au hana uhakika wa nini atakacho, chochote apatacho ni sawa.Kokote atakapoanzia, kokote atakapopita na atakapoishia ni sawa tu. Upepo ukiende kushoto, ataenda ukirudi kulia atarudi na ukiisha atatulia alipo.

Ni lazima wanadamu tuishi maisha yenye dhima "live with purpose" Tujue kwa nini tunaishi? tunataka nini? na tujiwekee misingi ya kufikia kile anachokitaka. Watanzania wengi hili bado hatujalielewa na athari yake ni kwamba tukiamka asubuhi tunaangalia nini kinatokea; tuanaenda nacho hadi jioni, tukiamka siku ya pili tunaangalia tena nini kinatokea tunaenda nacho na cha jana yake tushakisahau hivyo hivyo hadi kila mmoja wetu muda wake wa kuondoka duniani unafika, anaondoka naye anasahaulika.

Sasa kwa kuishi maisha ya namna hiyo, tusitegemee kupata matokeo ya maana sana wala kuwa na mchango mkubwa kwenye kuibadili nchi hii na hali ya maisha ya watu wake kwani katika mazingira hayo; chochote kitokeacho kwetu ni sawa kwa kuwa hatuna muelekeo maalum.

Mathalan, kuna mambo ambayo watanzania kila tukiamka asubuhi tunayalalamikia lakini hatuchukui hatua yoyote ya maana, au hatua tunazochukua ni zile zile na matokeo yanakuwa yale yale lakini wala hatugutuki; tunaendelea vile vile tu! tukiamini ipo siku mambo yatabadilika tu bila kujua kuwa kufanya hivyo ni kinyume kabisa na kanuni za kimaumbile ambapo ili binadamu afanikiwe ni lazima a- comply na kanuni hizo za kimaumbile.

Pamoja na maneno yakuudhi aliyotuambia Mzee Trumph; tunayo mambo ya kujifunza kutoka kwake hasa alipoeleza baadhi ya mambo yaliyoifanya Amerika na Ulaya Kuendelea na baadhi ya matatizo aliyotueleza kuwa watu weusi tunayo ikiwemo tabia ya kupenda kutafuta zilipo ndizi mbivu badala ya kuivisha za kwetu.

Kama Watanzania tukiamua kubadilika na kuachana na ushabiki huu usiotusaidia na tukajiongeza kidogo; kila kitu kinachotuhusu kitabadilika na kama tukiendelea kuwa kama tulivyo hakuna kitakachobadilika.
Toa solution sasa tutafikaje tunakotaka kwenda icje ikawa ndo wale wale unatutaka tubadilike halafu we ubadiliki
 
Sasa umejidghirisha kuwa wewe ni wa lumumba. Akili kakabidhiwa think tank Bashite na mtekelezeji chakubanga. Mambo yote ni ndani ya sanduku la ufipa na lumumba hatuchomoki. Wenye akili wanasubiri wakati mwafaka kuepuka hoja za bunduki.
Huyo masikini alidhani jf ni kama uvccm , ambako mtu kama Jokate anaweza kukwaa uongozi kwa njia za panya .
 
Kwanini Tusiamue kufanya itikadi ya Trump kuwa "Wrong" Kwa kujiongeza na kufikiri zaidi ya kujibizana wewe wa lumumba wewe! wewe wa ufipa!!

Ndugu watanzania wenzangu, tunatakiwa tufahamu kuwa dunia haitusubiri na muda tulio nao duniani ni mfupi mno. Sasa tukiamua kujifungia kwenye kaduara kadogo mno ka kufikiri wakati wenzetu wanatanua wigo wa kufikiri na kufanya maamuzi yenye impact za ajabu duniani na kuyatekeleza kwa kasi ndani na nje ya nchi zao ili kutimiza dhima ya maisha yao; huo utakuwa ni mzigo wetu wenyewe kama watanzania. Tutakuwa tumeamua kuwa mfano wa sisimizi aliyeingia kwenye kifuu chenye maji akadhani anaogelea kwenye bahari, kumbe yuko kwenye dunia ya peke yake!.

Dunia ni pana sana na ina vitu vingi sana ila kwa bahati mbaya Watanzania wengi (si wote) tunafikiri Dunia ni Ufipa na Lumumba, Chadema na CCM, kisha tushamaliza kila kitu, kinachofuata udaku wa kiongozi gani kamjibu nani au nani kamjibu kiongozi gani.

Ni lazima sasa Watanzania tuelewe kuwa ili kuweza kupata mabadiliko na maendeleo tunayoyataka na nchi yetu iwe bora kuliko hapo kabla, ni lazima sisi wenyewe kwanza kubadilika kwanza, na hayo yote huanzia kwenye fikra zetu.

Ndugu watanzania wenzangu; tusipoamua kubadilika hakuna kitakachobadilika juu yetu. Hiyo ni kanuni ya kimaumbile. Tusichoke kujifunza na tunayojifunza tuyafanyie kazi.Tusione aibu kubadilika kwani ndio njia pekee itakayotuwezesha kwenda mbele kwa kasi. Si nchi,si vyama vya siasa au kitu chochote kitakachokuwa bora ikiwa hatutabadilisha fikra zetu .

Tunasema eti karne ya 15, Afrika na Ulaya zilikuwa na maendeleo yanayokaribia kulingana lakini hatutafakari kwa kina kwamba kwa nini tupo hivi leo, tunafanya nini na wengine wanafanya nini na kwa nini. Tunapenda sana simple things, decisions & conclusions kwenye mambo nyeti.Tunasema Waafrika hatupendani kisha tunaishia hapo. Tunasema ukosefu wa ajira kwa vijana nchini ni bomu linalosubiri kulipuka kisha tunaishia hapo.Tunasema uzalendo umepotea Tanzania lakini hatupigi hatua mbele kujiuliza kwa nini na tufanye nini. Tunasema watanzania hatupendi kusoma vitabu halafu tunaishia hapo.Tunasema watanzania hatupendi kujadili mada za maana na kutoa hoja zenye manufaa kwetu na kwa watanzania wenzetu kisha tunaishia hapo then tunasubiria tukio la siku! n.k.

Kama mtu hajui aendako hawezi kupotea. Popote alipo au atakapokuwa itakuwa ni sawa. Kama mtu hajui au hana uhakika wa nini atakacho, chochote apatacho ni sawa.Kokote atakapoanzia, kokote atakapopita na atakapoishia ni sawa tu. Upepo ukiende kushoto, ataenda ukirudi kulia atarudi na ukiisha atatulia alipo.

Ni lazima wanadamu tuishi maisha yenye dhima "live with purpose" Tujue kwa nini tunaishi? tunataka nini? na tujiwekee misingi ya kufikia kile anachokitaka. Watanzania wengi hili bado hatujalielewa na athari yake ni kwamba tukiamka asubuhi tunaangalia nini kinatokea; tuanaenda nacho hadi jioni, tukiamka siku ya pili tunaangalia tena nini kinatokea tunaenda nacho na cha jana yake tushakisahau hivyo hivyo hadi kila mmoja wetu muda wake wa kuondoka duniani unafika, anaondoka naye anasahaulika.

Sasa kwa kuishi maisha ya namna hiyo, tusitegemee kupata matokeo ya maana sana wala kuwa na mchango mkubwa kwenye kuibadili nchi hii na hali ya maisha ya watu wake kwani katika mazingira hayo; chochote kitokeacho kwetu ni sawa kwa kuwa hatuna muelekeo maalum.

Mathalan, kuna mambo ambayo watanzania kila tukiamka asubuhi tunayalalamikia lakini hatuchukui hatua yoyote ya maana, au hatua tunazochukua ni zile zile na matokeo yanakuwa yale yale lakini wala hatugutuki; tunaendelea vile vile tu! tukiamini ipo siku mambo yatabadilika tu bila kujua kuwa kufanya hivyo ni kinyume kabisa na kanuni za kimaumbile ambapo ili binadamu afanikiwe ni lazima a- comply na kanuni hizo za kimaumbile.

Pamoja na maneno yakuudhi aliyotuambia Mzee Trumph; tunayo mambo ya kujifunza kutoka kwake hasa alipoeleza baadhi ya mambo yaliyoifanya Amerika na Ulaya Kuendelea na baadhi ya matatizo aliyotueleza kuwa watu weusi tunayo ikiwemo tabia ya kupenda kutafuta zilipo ndizi mbivu badala ya kuivisha za kwetu.

Kama Watanzania tukiamua kubadilika na kuachana na ushabiki huu usiotusaidia na tukajiongeza kidogo; kila kitu kinachotuhusu kitabadilika na kama tukiendelea kuwa kama tulivyo hakuna kitakachobadilika.
we ndo umechelewa uko bize na mabandiko ya kipuuzi wenzio tunapiga kazi, nyie ndo mnatuwamisha katiba mpya hamkati"
 
Back
Top Bottom