Benki ya NMB wamenifanya ombaomba baada ya kuibiwa pesa zangu nilizolimbikiza kwa miaka kadhaa

Status
Not open for further replies.
Nimewahi kufanya kazi NMB,ninachojua ni kwamba pesa haiwezi kutoka akaunti moja kwenda nyingine bila idhini ya mteja,kuna kitu kinaitwa "standing order" yaani unajaza fomu ya makubaliano baina yako mteja na benki ili ikifika tarehe fulani pesa kiasi fulani kitoke kwenye akaunti yako na kiingie kwenye akaunti nyingine,mfano akaunti ya mtoto bila wewe kwenda benki kujaza fomu(Automatic debited and credited).Hilo la kwanza!

La pili(na hili ndilo linawakumba wengi), ni utapeli!Hapa kuna ushirikiano "mchafu" kati ya watumishi wa benki na wa kampuni za simu(baadhi wasio waaminifu) na hawa matapeli kwa kuvujisha taarifa za mteja.Hapa kidogo tuwe makini maana katika hili benki kama taasisi haihusiki na wala usijisumbue kudai haki yako maana moja kwa moja unaingia katika kundi la watu/wateja ambao hawakufuata masharti ya benki na hivyo kuitwa ulikuwa "mzembe".

Kinachofanyika ni kwamba kuna hao matapeli wanakupigia simu na kujitambulisha kuwa wao ni staff wa benki fulani,wanachofanya ni kucheza na saikolojia tu,kwanza watakutaja jina lako kabla hata hujawatajia,watataja namba yako ya akaunti,watakutajia kiasi kilichoingia, kilichotoka karibuni,nk.Baada ya hapo watajifanya kama wapo bize ofisini wanapokea simu nyingine watakuweka hewani kidogo huku kwa mbali ukisikia sauti za watu kama vile ofisini panavyokuwa bize(kumbuka hii ni katika kukuteka wewe akili ukiamini kwamba kweli hao jamaa wapo benki).Kisha baadae watakwambia kuna taarifa zako zinaonekana hazijaboreshwa kwa hiyo wanatka kuziboresha.Watakuuliza ulijaza fomu za kuboresha akaunti, utasema ndio;baadae baada ya kukuzungusha na maswali meengi na wewe kuamini ni watu wa benki watakuuliza,hivi namba yako ya SIRI ulitumia ile ile ya mwanzo ambayo ni.....(watataja no ya uongo mfano 1234), wewe haraka haraka utasema hapana natumia 1980.Ndugu yangu, UMEKWISHA!

Baada ya muda wa dakika kama mbili au tatu kama ulijiunga na huduma za kibenki kwa simu, wanai-swap line yako hutoweza ku-access huduma za kibenki kwa njia ya simu kuanzia muda huo,watahamisha kiasi cha pesa kilichomo kwenye akaunti yako kwenda kwenye no "fake" za simu zao na baada ya sekunde kadhaa hizo pesa zilizohamishwa kwenye hizo no zao zinahamishwa tena kwenda kusikojulikana na zile line zao pia wanazi-swap.Yaani ni wizi unaotumia akili sana hata jeshi letu la polisi nadhani kwa kutokuwa na wataalamu(sina hakika), wanashindwa kabisa kusaidia kutokomeza wezi hawa.

Kama huna utaratibu wa kwenda benki kuangalia salio ndugu yangu baada ya siku kadhaa hata ungekuwa na milioni 50 zinalambwa zote.Hawana ujanja wa kuhamisha kiasi kikubwa kwa siku moja ndio maana wanakuondolea access ya kuweza kuangalia hata salio kwa simu yako ili wao wapate nafasi ya kuendelea kuzihamisha.So ni vizuri kila wakati jaribu kuingia kwenye akaunti yako kama umejiunga na huduma za kibenki kupitia mitandao ya simu,ukiona huwezi kuona kitu usijiridhishe kusema tu kuwa ni tatizo la kimtandao, chukua hatua mbele zaidi.

Ndio maana hapo juu kuna wadau wamechangia kuwa muhanga wa tatizo hili aweke wazi mazingira ya kuibiwa ili watu wamshauri.Mi namshauri kama aliitoa no yake ya siri kwa mtu yeyote na pesa imeibiwa kupitia eidha ATM au kupitia mtandao wa simu,basi hapo benki haihusiki kwa namna yoyote maana wanashauri na kutoa matangazo kila siku, USITOE NAMBA YAKO YA SIRI KWA MTU YEYOTE.(Labda hapa kwenye neno 'yeyote' hatujapatilia maanani), yaani hata mkeo/mumeo.
Ila kama pesa imehamishwa ndani ya benki,yaani "account to account"; tafuta mwanasheria wako fungua kesi kifua mbele maana hiyo ni kesi nyepesi mno na uzuri ushahidi unao yaani benki itakulipa tu hakuna namna.

Kumradhi:
Najua kwa komenti hii naweza nikawa nimewaharibia " wapiga dili"hao lakini ni bora uokoe mamia na kupoteza makumi.
 
Pole sana boss
Sifahamu utaratibu wa sheria vizuri ila nadhani ni muda sasa na wewe uufahamu ili ikiwezekana uwafungulie kesi mahakamani.
Na ukumbuke hiyo ni bank, hivyo usije ukadai hela za kununulia maembe ya futari.
Wao wana mawakili wakugeuza ukweli kuwa uwongo, sijui kama mhanga nae ana uwezo wa kuweka wakili wa kumsaidia kufanya ukweli ubaki kuwa ukweli
Fungua kesi mahakamani utashinda asubuh mapema
 
Tana huyu meneja mpya hajari utazunguka sana. Kenyata sasa hivi ovyo bora enzi za mathias.

Pesa ya benk haipotei wewe nenda mahakamani utalipwa na usumbufu miaka yoteee
 
Nimewahi kufanya kazi NMB,ninachojua ni kwamba pesa haiwezi kutoka akaunti moja kwenda nyingine bila idhini ya mteja,kuna kitu kinaitwa "standing order" yaani unajaza fomu ya makubaliano baina yako mteja na benki ili ikifika tarehe fulani pesa kiasi fulani kitoke kwenye akaunti yako na kiingie kwenye akaunti nyingine,mfano akaunti ya mtoto bila wewe kwenda benki kujaza fomu(Automatic debited and credited).Hilo la kwanza!

La pili(na hili ndilo linawakumba wengi), ni utapeli!Hapa kuna ushirikiano "mchafu" kati ya watumishi wa benki na wa kampuni za simu(baadhi wasio waaminifu) na hawa matapeli kwa kuvujisha taarifa za mteja.Hapa kidogo tuwe makini maana katika hili benki kama taasisi haihusiki na wala usijisumbue kudai haki yako maana moja kwa moja unaingia katika kundi la watu/wateja ambao hawakufuata masharti ya benki na hivyo kuitwa ulikuwa "mzembe".

Kinachofanyika ni kwamba kuna hao matapeli wanakupigia simu na kujitambulisha kuwa wao ni staff wa benki fulani,wanachofanya ni kucheza na saikolojia tu,kwanza watakutaja jina lako kabla hata hujawatajia,watataja namba yako ya akaunti,watakutajia kiasi kilichoingia, kilichotoka karibuni,nk.Baada ya hapo watajifanya kama wapo bize ofisini wanapokea simu nyingine watakuweka hewani kidogo huku kwa mbali ukisikia sauti za watu kama vile ofisini panavyokuwa bize(kumbuka hii ni katika kukuteka wewe akili ukiamini kwamba kweli hao jamaa wapo benki).Kisha baadae watakwambia kuna taarifa zako zinaonekana hazijaboreshwa kwa hiyo wanatka kuziboresha.Watakuuliza ulijaza fomu za kuboresha akaunti, utasema ndio;baadae baada ya kukuzungusha na maswali meengi na wewe kuamini ni watu wa benki watakuuliza,hivi namba yako ya SIRI ulitumia ile ile ya mwanzo ambayo ni.....(watataja no ya uongo mfano 1234), wewe haraka haraka utasema hapana natumia 1980.Ndugu yangu, UMEKWISHA!

Baada ya muda wa dakika kama mbili au tatu kama ulijiunga na huduma za kibenki kwa simu, wanai-swap line yako hutoweza ku-access huduma za kibenki kwa njia ya simu kuanzia muda huo,watahamisha kiasi cha pesa kilichomo kwenye akaunti yako kwenda kwenye no "fake" za simu zao na baada ya sekunde kadhaa hizo pesa zilizohamishwa kwenye hizo no zao zinahamishwa tena kwenda kusikojulikana na zile line zao pia wanazi-swap.Yaani ni wizi unaotumia akili sana hata jeshi letu la polisi nadhani kwa kutokuwa na wataalamu(sina hakika), wanashindwa kabisa kusaidia kutokomeza wezi hawa.

Kama huna utaratibu wa kwenda benki kuangalia salio ndugu yangu baada ya siku kadhaa hata ungekuwa na milioni 50 zinalambwa zote.Hawana ujanja wa kuhamisha kiasi kikubwa kwa siku moja ndio maana wanakuondolea access ya kuweza kuangalia hata salio kwa simu yako ili wao wapate nafasi ya kuendelea kuzihamisha.So ni vizuri kila wakati jaribu kuingia kwenye akaunti yako kama umejiunga na huduma za kibenki kupitia mitandao ya simu,ukiona huwezi kuona kitu usijiridhishe kusema tu kuwa ni tatizo la kimtandao, chukua hatua mbele zaidi.

Ndio maana hapo juu kuna wadau wamechangia kuwa muhanga wa tatizo hili aweke wazi mazingira ya kuibiwa ili watu wamshauri.Mi namshauri kama aliitoa no yake ya siri kwa mtu yeyote na pesa imeibiwa kupitia eidha ATM au kupitia mtandao wa simu,basi hapo benki haihusiki kwa namna yoyote maana wanashauri na kutoa matangazo kila siku, USITOE NAMBA YAKO YA SIRI KWA MTU YEYOTE.(Labda hapa kwenye neno 'yeyote' hatujapatilia maanani), yaani hata mkeo/mumeo.
Ila kama pesa imehamishwa ndani ya benki,yaani "account to account"; tafuta mwanasheria wako fungua kesi kifua mbele maana hiyo ni kesi nyepesi mno na uzuri ushahidi unao yaani benki itakulipa tu hakuna namna.

Kumradhi:
Najua kwa komenti hii naweza nikawa nimewaharibia " wapiga dili"hao lakini ni bora uokoe mamia na kupoteza makumi.
Umeelezea vizuri sana nadhani umewasaidia na wengine. Huo wizi wa kuswap line nadhani wameuthibiti sasa hivi maana ukiswap line siku hizi huduma za mobile banking zinakuwa deactivated mpaka ukaunganishwe tena benki husika
 
POLE SANA MKUU ILA NACHOJIULIZA WAKINA NANI WALIKUWA WANAHAMISHA PESA ZAKO,JE ZILIKUWA ZINAKWENDA KWENYE ACCOUNT IPI NA KWA NINI WAFANYE HIVYO????
 
POLE SANA MKUU ILA NACHOJIULIZA WAKINA NANI WALIKUWA WANAHAMISHA PESA ZAKO,JE ZILIKUWA ZINAKWENDA KWENYE ACCOUNT IPI NA KWA NINI WAFANYE HIVYO????
Yaani haya mabenki ni shida sana,
Dada yangu alikua na account akiba, kuna kipindi kama cha miezi 6 hivi akawa anakuta account yake salio kubwa tofauti na ela za wateja wake walivyokua wanamtumia, akawa anazitumia maana zilikua zinakaa hadi wiki, baadae akiingiziwa ela wanakata ela yao na ilkua mara nyingine ml4 mpaka10, yaani kwa hesabu aliyopiga alizungusha kama ml 32 kwa hicho kipindi cha miezi6
 
Yaani haya mabenki ni shida sana,
Dada yangu alikua na account akiba, kuna kipindi kama cha miezi 6 hivi akawa anakuta account yake salio kubwa tofauti na ela za wateja wake walivyokua wanamtumia, akawa anazitumia maana zilikua zinakaa hadi wiki, baadae akiingiziwa ela wanakata ela yao na ilkua mara nyingine ml4 mpaka10, yaani kwa hesabu aliyopiga alizungusha kama ml 32 kwa hicho kipindi cha miezi6


Au system huwa inasumbua nini??
 
Aisee pole sana mkuu kama umesoma vizuri maelezo ya mdau aliefanya nmb hapo juu na kuyaelewa na una nyaraka zote nenda mahakamani kifua mbele!kama documents zako haziko complete nenda benki wakuprintie zote na usiwaambie lolote then toa nakala za kutosha hakikisha kama kuna sehemu zinahitaji mhuri zigongwe kila sehemu.
Halafu watafute mawakili mithili ya kina lisu haki ya Mungu wewe ni tajiri mkubwa sana tena utalipwa na fidia za kutosha.

Sent from my VFD 301 using JamiiForums mobile app
 
Kwa nini usiende Mahakamani?. Wewe chukua Wakili mpe vielelezo vyote utaona utakavyowashikisha adabu.
 
Ndugu wanaJF, Mimi ni mtanzania mzalendo na wa kipato cha chini ambaye Benki yangu ya NMB Tanzania imenifanya sasa ni wewe omba omba baada ya kuibiwa pesa zangu zote ambazo nimezilimbikiza kwa miaka kadhaa.

Nakumbuka niliamua kuweka pesa zangu benki ili ziwe salama. Nimezungushwa vya kutosha katika kujaribu kutafuta haki yangu lakini bado nimekuwa nikiwasiliana na meneja tawi la NMB Tanzania Kinyatta road bila kupata mafanikio kwa miaka kadhaa.Nimejaribu kuomba msaada NMB Tanzania makao makuu mpaka sasa sijapata msaada.

Naomba Msaada ili nirejeshewe pesa zangu kwani pesa zangu zilikuwa zikihamishwa kutoka kwenye account yangu na kuingizwa kwenye account nyingine bila idhini yangu.

Hivi punde nitaweka vielelezo vyote vya barua ya Polisi,barua ya meneja NMB Tanzania Tawi la Kinyatta jijini Mwanza na barua ya meneja makao makuu.

Nataka muone benki ya wazalendo NMB Tanzania ilivyoyafanya maisha yangu kuingia shimoni.

----------Update------------
Asante wadau, nitaweka vielelezo vyote ninavyo kwani kesi hiyo ilifika polisi.Vielelezo vyote vinavyoonesha pesa zilivyohamishwa ninavyo na account zilipokuwa zinahamishiwa ninazo pia.

Katika barua ambazo nilizituma nilipomwandikia Mkurugenzi Mkuu wa NMB Tanzania niliambatanisha na vielelezo vyote.

Niliweka
1. Barua ya kufungulia kesi
2. Niliweka bank statement inayoonyesha pesa zangu zilivyo kuwa zikihamishwa kwenda kwenye account mbili tofauti.

Nilisambaza nakala hizo kwa...
a) BoT Mwanza
b) BoT Taifa
c) Mwanasheria mkuu
d) Mwanasheria wa mkoa wa Mwanza
e) Waziri Mkuu
f) Waziri wa Katiba na Sheria
g) Mkuu wa Mkoa Mwanza
h) Meneja wa tawi la Kinyatta NMB Tanzania,
i) RCO mkoa wa Mwanza.

Kati ya hao ni Mwanasheria wa Mkoa angalau alionesha kujali kwa kuniita ofisini kwake.

Aidha nakiri kupokea barua kutoka makao makuu NMB Tanzania, lakini haikuonesha msaada zaidi ya kusema tuwasiliane.

Miaka kadhaa imepita sasa naendelea kuzunguka meneja wa Tawi NMB Tanzania Kinyatta Mwanza ameishanipa maelekezo ikiwemo kunitaka niandike barua ya kuomba nilipwe lakini hata baada ya kuandika ni miaka sasa hakuna majibu.

Naomba msaada kwa Waziri wa Fedha anisaidie kwani wale ambao pesa zangu zilihamishiwa kwenye account zao wapo na tulishakutana Polisi na wakadai account zao hazitumiki.

Sielewi na sielewi naomba msaada wa haraka.
mkuu kusena kweli unenikumbusha mbali sana., nimewahi kuibiwa hela nyingi kuputia tawi hilo ,ilikuwa mwaka 2011 ilinipa taabu sana nilianzia polisi nikafingua kesi ,baada ya kuona sipati msaada nikafunga safari ya kwenda makao makuu ya NMB na hapo nikaelekezwa kwenda kunuona RISK manager lakini naye sikuona msaada wowote.
ilinibidi nirudi polisi wakasema wanashughulikia mpka sasa sijawahi kupata mrejesho.
nikipata wasaa nitaeleza namna nilivyoibiwa.
Sina imani tena na NMB ,
 
Unaweza kutoa maelezo kuhusu mazingira ya kuibiwa kwako ili tufahamu imetokana na na uzembe wa bank au ni mwenyewe ndie umesababisha!!

Umejuaje pesa zilikuwa zinahamishwa kutoka kwenye akaunti yako na kwenda kwenye account nyingine?! Ni kwamba kuna hizo details kwenye statement; au?!
Sasa wewe unafikiri statement isipoeleza fedha zimeenda wapi itaeleza nini? Ndio maana ya statement. Hata ukinnunua.muda wa maongezi au kununua umeme toka akaunti ya NMB utakuta kila kitu kwenye statement.
 
nenda bot kuna kitengo kinachoshugurikia madai kama yako utapewa jibu, njia rahisi ni kwenda mahakamani ila tatizo la mawakili wetu ni kutaka pesa mbele pia wengi sio waaminifu hao waaminifu hela yao ni kubwa sana
 
Duh hizi bank za TZ shida sana asante mkuu umenifungua macho sasa hivi naanza mikakati ya kuzitoa fedha zangu benk zote nikafanye investment kumbe naweza azirika mjini kihivyo nilikua naziamin sana bank lakini kwa hili inabidi nijivue
 
Inasikitisha sana...
Pole sana..


Kuna wafanyakazi wa bank wasio waaminifu...Itakuwa wana take advantage kwa kuhamisha pesa kwenye account zilizokaa sana bila kutumiwa...

Sababu account Ikikaa sana bila kutumiwa, lets say 2years bank zingine wana zi freez, mpaka pale utakapohitaji kuitumia tena na hawana longo longo kuzi re activate....

Kwa NMB utaambiwa ufungue nyingine mpya... Nahisi hapo ndiyo wanapo take advantage...



Cc: mahondaw
 
Dah pole sana ...basi sasa itakua Upuuzi kuweka sasa akiba benki.hizi za kiswahili mtu unaweka hela benk unategemea ziko.salama.kumbe zinapigwa..aise umenifungua macho
 
Mkuu shaks001, (post #21 hapo juu) uliyewahi fanya Nmb, maelezo uliyotoa ni shule tosha.. Tena ingefaa ungeweka hayo maelezo kny uzi mpya, wengi wajue wafunguke. Umenitoa tongotongo kwa hili. Thnx!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom