Nisipobadili CHAP CHAP Account kwenda Personal Account, NMB wanaweza kuibadili bila ridhaa yangu?

Dx and Rx

JF-Expert Member
Jul 16, 2017
1,303
3,085
Nilitaka kutoa pesa dirishani kwenye tawi moja la Bank ya NMB hapa kwenye huu mji wenye Elnino.

Nilipofika dirishani nikamkuta mhudumu nikampa ile karatasi(bank slip) niliyojaza ili nitoe hela.

Mhudumu akaingiza details na kuthibitisha taarifa then akakata hiyo slip kwenye maandishi ya kwa red pen na akaniambia nenda dirisha fulani.

Nilipofika kwenye hilo Dirisha nikampa huyo mhudumu niliyemkuta pale ile slip niliyotoka nayo dirisha la kwanza.

Baada ya kuiona na kuangalia details kwenye mfumo akaniambia nenda pale mapokezi ukapewe fomu ujaze(mimi nilikuwa sijui ni fomu ya aina gani)

Nilipofika mapokezi nikamwambia nimetoka kwenye dirisha fulani nilikuwa nataka kutoa hela ila nikaambiwa nije hapa, mhudumu wa mapokezi baada ya kunisikia hivyo akanipa fomu akaniambia jaza. Nikaisoma fomu nikagundua ni fomu ya kubadili status ya Bank Account.

Baada ya hapo nikarudi nikamwambia mimi nilitaka kutoa hela na wala sikutaka kubadili status, akanipa maelezo ambayo hata sikuyaelewa huku akisisitiza nijaze ile fomu ndipo nikapate huduma.

Nikasema ngoja nimuulize kwanza jamaa yangu ambaye alikuwa ananisubiri sehemu ili twende kusaka maokoto. Nikamtext jamaa fast na kumueleza scenario akaniambia "kimbia haraka, hao watakuumiza kwa makato", akaendelea kunisisitiza "ondoka fast jifanye unaongea na simu toka katoe ATM halafu uje twende"

Nikaamua kufuata ushauri wa jamaa yangu, nikaondoka.

Sasa nilitaka kutoa tena hela dirishani ila kwenye Tawi la hiyo Bank mkoa mwingine(maana nilisafiri kusaka maokoto)

Wakati naenda kwenye hili tawi la mkoa mwingine nilikuwa najua huenda wakanizingua tena na ikawa hivyo kweli.

Kwenye hili tawi mhudumu alipoangalia details baada ya kumpa slip, aliniuliza "umeangalia salio"? nikamwambia hapana(ila nilikuwa najua salio maana huwa nachukua risiti kila nikitoa hela ATM)

Akaniambia Account inasoma, nikamwambia inasoma nini, akaanza kutabasamu. Akasema salio lipo ila halioni kwenye computer, nikamwambia kwa hiyo haiwezekani kutoa, akasema ndio.

Nikamwambia mbona ATM natoa kama kawaida, akasema hapa dirishani haiwezekani. Halafu akaniambia nenda pale mapokezi wakakuangalizie Account na wakusaidie ili uweze kutoa.

Nikajisemea hawa mbona wananiwinda hivi, nikasepa nikaenda kutoa ATM kidogo kidogo ingawa huku napo nilipigwa limit sikuweza kutoa kiasi nilichotaka baada ya kuambiwa na system kuwa nimefikia kikomo cha kutoa kwa siku ATM.

Kabla ya kuandika huu uzi nimepitia nyuzi humu zinazohusu CHAP CHAP Account ya NMB, nimegundua kuwa haina makato mengi kama PERSONAL Account. Kubwa zaidi nimeona makato ya kila mwezi na ya minimum balance to maintain account. Naona lengo la kuwindwa ni kutaka niingizwe kwenye hayo makato na mengineo ambayo wanayajua wao.

Sasa sitaki niibadili kwanza kama wanavyonitaka, je, wanaweza kuibadili bila ridhaa yangu maana nimeona lazima nijazishwe ile fomu ambayo nitaweka details zangu kama NIN, Picha, Anwani n.k
 
Chap chap account mwisho million 5 ...

Ukitaka kuweka pesa nyingi Zaidi ndio huwa wanabadili account kutoka chap chap mpaka personal account.....

Sasa Ni pesa gani uliyonayo kwenye chap chap mpaka kutoa inakuwa ngumu hivo ....Nina iman haizid million 5 ,sasa hio Ni pesa ya kukuzuia kuchukua
 
Chap chap account mwisho million 5 ...

Ukitaka kuweka pesa nyingi Zaidi ndio huwa wanabadili account kutoka chap chap mpaka personal account..
Hahahaaa, sasa wanaweza kubadili bila mimi kuridhia maana wananitaka nijaze fomu ili waweze kuibadili.

Natumia chap chap mkuu na salio lishazidi hiyo 5M kitambo, sasa kikwanzo ndio nikitaka kutoa zaidi ya 1M na nikienda dirishani ndio wananitaka nibadili kwanza kwa kunijazisha zile fomu ndipo nipate huduma.

ATM natoa bila shida yeyote ila nimeona wananilimit kutoa kiasi kwa siku
 
Hahahaaa, sasa wanaweza kubadili bila mimi kuridhia maana wananitaka nijaze fomu ili waweze kuibadili.

Natumia chap chap mkuu na salio lishazidi hiyo 5M kitambo, sasa kikwanzo ndio nikitaka kutoa zaidi ya 1M na nikienda dirishani ndio wananitaka nibadili kwanza kwa kunijazisha zile fomu ndipo nipate huduma.

ATM natoa bila shida yeyote ila nimeona wananilimit kutoa kiasi kwa siku
Nenda katoe kwa wakala wa Bank husika, problem solved.
 
Sasa hio ndio njia pekee utatoa hela bila kero. Kama unaona makato makubwa kasajili Personal Saving Account uanze kulimwa charges. Hio Chap Chap ni ya wanafunzi na wanachuo kupokelea boom
Ni sahihi mkuu, nilijiunga miaka mingi nyuma kipindi naanza chuo, baada ya kumaliza nikaendelea nayo hadi sasa. Hawa walaji nao wanaanza kumezea mate vijisenti vilivyopo mle kwa kutaka makato mengi.

Ngoja niendelee kutoa kwa Wakala na ATM ila kuna muda lazima watanikandamiza tu hadi nibadili. Mfano Kadi inaisha muda wa matumizi mwakani, nikija kutaka kuibadili wanaweza kunikazia nibadili na account
 
Ni sahihi mkuu, nilijiunga miaka mingi nyuma kipindi naanza chuo, baada ya kumaliza nikaendelea nayo hadi sasa. Hawa walaji nao wanaanza kumezea mate vinisenti vilivyopo mle kwa kutaka makato mengi.

Ngoja niendelee kutoa kwa Wakala na ATM ila kuna muda lazima watanikandamiza tu hadi nibadili. Mfano Kadi inaisha muda wa matumizi mwakani, nikija kutaka kuibadili wanaweza kunikazia nibadili na account
Hahahahahah hapo imeisha hio!!! Lazma mkae meza ya usuluhishi
 
Hahahahahah hapo imeisha hio!!! Lazma mkae meza ya usuluhishi
Hahahaa Dah, basi ngoja nikomae kibishi hadi mwakani endapo sitapata dharura ya kunilazimu kufikia kuibadili kwa lazima.

Halafu hawa NMB wameanza kunishobokea kwa sms zao sijui mkopo, mara Jamii Bond kisa wamejua kuna maokoto ya hapa na pale yanayoingia kwenye account. Kibindi maokoto hamna hawakuwa wananitumia hizi sms.
 
Hahahaa Dah, basi ngoja nikomae kibishi hadi mwakani endapo sitapata dharura ya kunilazimu kufikia kuibadili kwa lazima.

Halafu hawa NMB wameanza kunishobokea kwa sms zao sijui mkopo, mara Jamii Bond kisa wamejua kuna maokoto ya hapa na pale yanayoingia kwenye account. Kibindi maokoto hamna hawakuwa wananitumia hizi sms.
Tuelekezane basi mazingira vipi
 
Hahahahahah mi pia niko mjini ntolee password basi maana hio card yangu ina kutu. Hela zinaishia Mpesa tu
Hahahaaaa, miaka haifanani mkuu tunaumaliza jwa Elnino huu, miaka ya nyuma haikuwepo. Mwakani huenda kuna neema ya aina yake na kutu hutoiona
 
Hapo watakuvutaaa vutaaaa baadae atm card wataipiga pin. Ukitaka kwenda kupata nyingine hapoa ndipo unapigwa na kitu kizito.
Niliwahi milik chal chap nilidunda nayo sanaaa. Ila nikapoteza atm card mhudumu mmoja wakat naenda chukua nyingine akaniuliza niibadil account. Nkamwqmbia hapana pia akanambia sawa maana si inaingia stahiki za kibarua tuu nikamjibu ndio. Basi akanipa atm card mpya pasipo kubadil account status. Siku nyingne wakafunga atm card yangu nadhan hii ilikumba chap chap zoteeee maana siku naenda badili nilikuta chap chap weng ndo wanatoa taarifa zao zile za nida ili twendelee kupata maisha.

Sasa siku nyingne nikaenda pale nmb flan pale karibu na kisutu na kachap chap kangu dada mmoja akanipa form ya kujaza nikaisoma nikamwambia mm sitaki kubadil status ya account yeye akakazana siibadili inakuwa hivyo hivyo tuuu nikaangaliaaaa nkaona huyu mwanamke ananionajee yan vitu viko waz kimaandish ila anasema habadiliii.

Nikakasirika nikajisemea ngoja tu nijaze maana sina uwezo wa kutumia atm sasa nafanyajeee wakati ndo anakazania na mm sijui cha ziada. Baada ya kumaliza nikamwona mama mmoja ambae yupo hapo na aliwahi nihudumi nikamwambia akasikitika ila akanambia ndo basi labda wakati mwingine ukija ku renew atm card tunaweza irudisha hiyo account yako kwenye chap chap tena maana haiwekwi akiba zaid vile unakingia hela ya chakula na kutoa


Bahati nzuri au mbaya huyo mama ndo kashastaafu kazi
Na huyo mama ndo alinifunua kuhusu chap chap na namna watu wanavyo badilishiwa hadhi za account zao pasipo kujua na pasipo kutaka.

Yote kwa yote wao wanashawish watu kuwa na chap chap ila hawataki ziishi muda mrefu ili waweze kupata hela nying hasa kutoka kwenye makato ya mwez na huduma nyingine.

Huo ni uhun flan ambao wanafanya ambao hata si mzuri. Bora wangesema chap chap inaishi miaka kadhaa ila si huu uhuni wa kutaka kumbadilishia mtu account status kijanja kijanza.
 
Hapo watakuvutaaa vutaaaa baadae atm card wataipiga pin. Ukitaka kwenda kupata nyingine hapoa ndipo unapigwa na kitu kizito.
Niliwahi milik chal chap nilidunda nayo sanaaa. Ila nikapoteza atm card mhudumu mmoja wakat naenda chukua nyingine akaniuliza niibadil account. Nkamwqmbia hapana pia akanambia sawa maana si inaingia stahiki za kibarua tuu nikamjibu ndio. Basi akanipa atm card mpya pasipo kubadil account status. Siku nyingne wakafunga atm card yangu nadhan hii ilikumba chap chap zoteeee maana siku naenda badili nilikuta chap chap weng ndo wanatoa taarifa zao zile za nida ili twendelee kupata maisha.

Sasa siku nyingne nikaenda pale nmb flan pale karibu na kisutu na kachap chap kangu dada mmoja akanipa form ya kujaza nikaisoma nikamwambia mm sitaki kubadil status ya account yeye akakazana siibadili inakuwa hivyo hivyo tuuu nikaangaliaaaa nkaona huyu mwanamke ananionajee yan vitu viko waz kimaandish ila anasema habadiliii.

Nikakasirika nikajisemea ngoja tu nijaze maana sina uwezo wa kutumia atm sasa nafanyajeee wakati ndo anakazania na mm sijui cha ziada. Baada ya kumaliza nikamwona mama mmoja ambae yupo hapo na aliwahi nihudumi nikamwambia akasikitika ila akanambia ndo basi labda wakati mwingine ukija ku renew atm card tunaweza irudisha hiyo account yako kwenye chap chap tena maana haiwekwi akiba zaid vile unakingia hela ya chakula na kutoa


Bahati nzuri au mbaya huyo mama ndo kashastaafu kazi
Na huyo mama ndo alinifunua kuhusu chap chap na namna watu wanavyo badilishiwa hadhi za account zao pasipo kujua na pasipo kutaka.

Yote kwa yote wao wanashawish watu kuwa na chap chap ila hawataki ziishi muda mrefu ili waweze kupata hela nying hasa kutoka kwenye makato ya mwez na huduma nyingine.

Huo ni uhun flan ambao wanafanya ambao hata si mzuri. Bora wangesema chap chap inaishi miaka kadhaa ila si huu uhuni wa kutaka kumbadilishia mtu account status kijanja kijanza.
Mkuu ahsante sana umenifungua sana kuhusu hizo mbinu zao. Nimekwepa attemp mbili hadi sasa kutoka matawi tofauti.

Nilikuwa nawakimbia mawakala kutolea hela kwao, sasa itanibidi niwe mteja muhimu wa mawakala pindi nikitaka kutoa hela zaidi ya 1M.

Hela ndogo ndogo za mboga nitakomaana ATM. Kadi inaexpire mwakani hapo nitashikwa, bora waje kunishika hivyo ila sio sasa. Hawa watu sio kabisa, wakiona kasalio kidogo wanakatolea mate, kama yule mdada wa pili kwenye tawi la pili alikuwa anatabasamu tu bila kuniambia ukweli huku akisema huwezi kutoa hela, nenda pale mapokezi ukasaidiwe.
 
Back
Top Bottom