Benki ya Dunia yaikopesha Tanzania Tsh. Trilioni 1.2 za Miradi ya Maji na Afya

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,114
49,840
Kazi inaendelea,

Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania na Wizara ya Fedha Kupitia Waziri Mwigulu zimesaini mkopo wa Dola mil. 560 sawa na shilingi Trilioni 1.3.

Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa ni kwamba mkopo huo ni kwa ajili ya Miradi ya Maji na Afya ya mama na mtoto.

====

mwiguu.jpg
mwiguu 1.jpg


Wizara ya Fedha na Mipango, imesaini mikataba wa miwili na Benki ya Dunia (WB), yenye thamani ya Sh1.264 trilioni kwa ajili ya kuboresha huduma endelevu za maji, usafi wa mazingira vijijini pamoja na afya ya mama na mtoto.

Mkataba huo umesaini leo Jumanne Februari 28, 2023 kati ya Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba, Mkurugenzi Mkazi wa WB, Nathan Belete na Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Afya Zanzibar, Dk Amour Suleiman Mohamed.

Dk Nchemba amesema mkataba huo umekwenda sambamba na msaada wa jumla ya dola za Marekani 29.93 milioni (Sh68.78 bilioni) zitakazotekeleza miradi hiyo kwa mustakabali wa maendeleo ya Watanzania.

"Mpango endelevu wa maji na usafi wa mazingira vijijinj utapokea Sh689.51bilioni ambao ni mkopo wa masharti nafuu wa IDA, eneo la mradi wa afya ya mama na mtoto litapokea Sh574.59 bilioni," amesem Dk Nchemba.

Belete amesema WB inajisikia faraja kuisadia Tanzania katika kuboresha sekta hizo ikiwemo ya afya ili kuhakikisha Taifa hili linafikia malengo yake hasa kuwezesha huduma bora ya afya ya mama na mtoto.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Afya, Dk Godwin Mollel amesema fedha hizo zitaboresha huduma za afya mama na mtoto, pamoja na ujenzi wa vituo vya upasuaji sambamba na kuwajenga uwezo watumishi wa kada ya afya.

Naye, Dk Mohamed amesema fedha hizo zitaleta mabadiliko katika sekta ya afya Zanzibar hasa katika kukabiliana na vifo vya mama na mtoto visiwani humo vinavyotokana na changamoto za afya
 
2C705F5E-C154-495D-9C72-34DC6F5ECEEC.jpeg
Waziri wa Fedha Mwigulu akisaini mikataba miwili ya mikopo ya masharti nafuu ya USD milioni 550 (sh. trilioni 1.264) kutoka Benki ya Dunia kwa ajili ya utelekezaji miradi ya afya ya mama na mtoto na mpango wa uendelevu wa maji na usafi wa mazingira.
 
View attachment 2532600 Waziri wa Fedha Mwigulu akisaini mikataba miwili ya mikopo ya masharti nafuu kutoka Benki ya Dunia kwa ajili ya utelekezaji miradi ya afya ya mama na mtoto na mpango wa uendelevu wa maji na usafi wa mazingira.
Siyo mbaya as long as kuna transparency, accountability and monitoring kwenye matumizi ya mkopo huo
 
Kazi inaendelea,

Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania na Wizara ya Fedha Kupitia Waziri Mwigulu zimesaini mkopo wa Dola mil. 560 sawa na shilingi Trilioni 1.3.

Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa ni kwamba mkopo huo ni kwa ajili ya Miradi ya Maji na Afya ya mama na mtoto.

====

View attachment 2532628View attachment 2532629

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba na Mkurugenzi Mkazi wa Benki Kuu Tanzania Bw. Nathan
Belete wakisaini na kuonesha Mikataba miwili ya Mkopo nafuu na Msaada wa USD milioni 550 (Tsh. Trilioni 1.264) kwa ajili ya kuboresha Sekta za Maji na Afya ya mama na mtoto.
Nina Imani mpaka Samia anaondoka madarakani, huduma za afya zitakuwa zimefika Kila Kona, maji ndio usiseme, yatajaa Kila mahali kama mate mdomoni
 
Kazi inaendelea,

Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania na Wizara ya Fedha Kupitia Waziri Mwigulu zimesaini mkopo wa Dola mil. 560 sawa na shilingi Trilioni 1.3.

Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa ni kwamba mkopo huo ni kwa ajili ya Miradi ya Maji na Afya ya mama na mtoto.

====

View attachment 2532628View attachment 2532629

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba na Mkurugenzi Mkazi wa Benki Kuu Tanzania Bw. Nathan
Belete wakisaini na kuonesha Mikataba miwili ya Mkopo nafuu na Msaada wa USD milioni 550 (Tsh. Trilioni 1.264) kwa ajili ya kuboresha Sekta za Maji na Afya ya mama na mtoto.
Serikali ya mikopo chini ya uongozi wa Mama Maridhiano!!
 
Dk Nchemba amesema mkataba huo umekwenda sambamba na msaada wa jumla ya dola za Marekani 29.93 milioni (Sh68.78 bilioni) zitakazotekeleza miradi hiyo kwa mustakabali wa maendeleo ya Watanzania.
Huo mustakabhali, ndio 10%?
Je hayo ni maendeleo au 'man'-endelea?
Mpango endelevu wa maji na usafi wa mazingira vijijinj utapokea Sh689.51bilioni ambao ni mkopo wa masharti nafuu wa IDA
I read between the lines
A carrot and a stick approach.
 
Hivi hizi Pesa zinakwenda wapi? Mbona maendeleo hayaonekani? Mbona maisha bado magumu??. View attachment 2532862
Bwawa la Julius Nyerere liko asilimia 85 ujenzi, valvu ya tatu kwa ukubwa duniani kupelekwa hapo, mtambo mkubwa wa tani 79 unaitwa runner umepelekwa ktk bwawa, Daraja la Jp Kigongo Busisi spidi kali, madaraja huoni Chang'ombe, Uhasibu, Kurasini, meli ya Mv Mwanza Hapakazi chombo kiko majini.

Huduma za maji, afya na nyingine hadi vijijini. Nchi kubwa hii ndugu yangu na kila Mtanzania anataka maji, umeme, barabara, afya, elimu nk. 🙏🙏🙏
 
Back
Top Bottom