Benjamin William Mkapa nimjuaye...

Hata mimi Binafsi sijafurahishwi na Jk hata kidogo, amekuwa anaficha sana uhalisi wake na pia hata utendaji wake tofauti sana na BEN, Ben alikuwa makini japo madudu yake. Jk is freaking with his ambitions. \sijui akipewa miaka mitano mingine itakuaje??
 
...pombe alikuwa obedient kwa mkapa ...na kwa maana hiyo mgombea yeyote ambaye alikuwa obedient kwa mkapa angepata urais ...lillikuwa chaguo la mkapa kwa uwaziri mkuu...

pinda...alikwa low profile kama nidhamu ya kikazi inavyompasa kuwa mtiifu kwa dola ..always yeye ni nationalist....[taifa kwanza]...NI WAZI HAKUWA KWA KIKWETE ..na kikwete hakumtaka....

...kikwete alitakiwa kumuweka pinda uwaziri mkuuu kama compromise kati ya watu wa mkapa, nationalists [wataifa].... kama angesaidia kuondoa hisia za umtandao....kikwete alikataa...lakini mwisho wa siku alikwama..akarudi kwa wazee ...na kumuweka pinda...

hata mkiangalia uteendaji wa pinda sio mwanasiaasa hata kidoho...lakini pia sio charismatic..yeye ni mtawala zaidi.... angepata rais mwenye msimamo thabiti... angefanikiwa sana kusimamia kazi...,tatizo kubwa ni kuwa rais wetu hana kauli dhabiti....za kimamlaka!!! aliyekuwa akimsaidia kwa kauli za namna hiyo ni lowassa....na ndio kusema pamoja na uzuri wa pinda anashindwa jambo moja na lowasa ...charsima!!!

Pinda sio tishio sana kwa nafasi ya urais ..kwa wanamkakati wa mwaka 2015...haoneshi tamaa ya madaraka!!!..he is a goob PM with poor president!!
 
Mkapa ni kweli alikuwa kiongozi mwenye agenda ya kueleweka kuhusu nchi yetu iende vipi, na kuna mambo mengi aliyofanya yanayoonekana, mfano TRA, ujenzi wa barabara, etc. Nisicho elewa ni kwanini utawala wake ukaruhusu corruption za kiwango kikubwa kama tulizoziona? Ilikuwaje wawekezaji aliwaona kama ndo warithi halali wa mali za TZ kuliko watz wenyewe? Sikazi yangu kuhukumu ila nafasi ipo ya yeye kutuambia yoote kuhusu hizi tuhuma zinazomkabili. Nafikiri anayochance ya kufanya hivyo. J
K bwana...duuh, story zimekuwa story!!!Yaani, we acha tu!!
 
Kwa maoni yangu, Mkapa aliona jinsi hali ya uchumi wa nchi ilivyokuwa isingewezekana kupata nguvu ya ndani ya kuiokoa kwa haraka. Nadhani ndio maana aliweka juhudi kubwa kutoka kwa wawekezaji wa nje. Ninaweza kukubaliana nae kwenye hilo. Kumbuka inflation ya 48% alipokuwa akichukua nchi.

Kumbuka wingi wa wataalam walivyoamua kuacha kazi na kukaa Salamander kwakuwa walipata nafuu ya maisha pale kuliko ofisini. Nchi ilikuwa haikopesheki wala haiaminiki hata kidogo. Mtu yeyote angeweza kutegeka kutafuta nguvu kubwa kutoka nje katika hali kama hiyo. Nadhani imani hiyo pia ilichangiwa na mifano ya nchi ambazo zimekuwa zikitafuta uwekezaji wa nje na kufanikiwa kwa kiasi kikubwa. Hali yetu ilikuwa mbaya sana wakati ule.

Tatizo ni kwamba, baada ya hali kuanza kuwa bora, alitakiwa aanze taratibu kuwezesha waTanzania kumiliki sehemu ya uchumi wa nchi badala ya kuachia wawekezaji wa nje kwenye kila sekta.
 
Ni kweli kabisa na pia Pinda is more Nationalist, ila napata sana wasiswasi na Jk maana sijaelewa sana itikadi yake..!! Hana sana tamaa ya madaraka sana Pinda labda aje kubadilika baadae sana.
 
Give me a break. Magufuli waziri mkuu!!! Hivi hatuna vipimo vya kujua ni nani anaweza kuwa kiongozi bora!? Wana-JF mnaanza kumshabikia mvunjaji sheria mkubwa Bw Magufuli, au kwa vile hamkujua aliyoyafanya kwenye mabarabara kuwavunjia watu nyumba bila ya kujali haki zao za msingi, tena kwa kukataa kuheshimu sheria ambayo ilikuwa wazi! Alishauriwa kuhusu haki za wananchi kule Kigoma na Shinyanga ambao barabara iliwafuata na sio wao waliingilia kingo za barabara, akakataa kata kata, matokeo wananchi wakavunjiwa bila fidia na Mungu anajua kilichowapata wale walala hoi. ALipojaribu kufanya hivyo hivyo kule Rombo, fisadi Mramba akazuia kwa nguvu zote, na wananchi wa Rombo walilipwa na wanaendelea kulipwa fidia. WAROMBO walikuwa na msemaji, hao wengine hawakuwa na msemaji. Tena hata pale Rombo Magufuli alilkuwa akifanya vikao vya kuwakemea wananchi licha ya Mbunge wao kutafasiri sheria na kuwahakikishia haki itatendeka. Huyu ukimpa madaraka makubwa si atajeuza sheria zote ziwe kwake.

Jamani mnasahau hata ile barabara aliyoilazimisha kule jimboni kwake, yaani kuifikia barabara ya lami ya Magufuli unapita kwenye mashimo makubwa mno....kiongozi anayevuta kamba kwake, jamani jamani halafu mje mlaani tena kama mnavyomlaani kijana mtanashati mwenye sura na akili za kuvutia JK......SIONI cha kumuenzi Mkapa kwani kama raisi alitimiza wajibu wake na tukamlipa na tunazidi kumlipa, lakini hilo la kuiba na mashemeji, wakwe na wattoto wake ni lazima alilipie
 
Ben Mkapa
Lakini watanzania sisi ni watu wa ajabu sana, kwa sababu sheria zipo na tunazifanyia marekebisho mara kwa mara tunapo hisi mapungufu, kiongozi yeyote anaongozwa na sheria zilizopo na kamwe hawezi kuwa juu ya sheria, tunaona wenzetu zambia na malawi wanvyofanya ukivurunda sheria itakuvurunda pia, Mkapa sio Mungu, ana kesi nyingi sana za kujibu na kuna watu wana ushahidi naye sasa kwa nini asishtakiwe? kama kujitetea mahakama ipo akajitetee huko ndiko haki na ukweli utapatikana, tatizo letu sisi watanzania ni waoga sana wa kutekeleza mambo, ni mabingwa wa kutoa hoja tu.
 
Kama kuna sheria mbona hajashitakiwa pamoja na madudu yote??
 
aliyekuwa anaongea kwa vitisho na kukemea waandishi wa habari lakini sasa anaishi kama nguchiro kwa kujificha...lol
 
Ni kweli kabisa na pia Pinda is more Nationalist, ila napata sana wasiswasi na Jk maana sijaelewa sana itikadi yake..!! Hana sana tamaa ya madaraka sana Pinda labda aje kubadilika baadae sana.



Saana Saana Tu! Duh!😀
He's very coal minded(sic) Hic!! tena sana😀
 



Mawazo yenu please objectively and for the better future of our country ,lovely Tanzania.


Huyu ndiye Kaniki kabokaaaa tehehehe😀
 
Pamoja na mengi lakini kubwa kuliko yote ni kuwa mjasiriamali akiwa ikulu. Yaani kufungua kampuni na kujipa mgodi wa kiwira wakati akiwa pale ikulu.
 
nadhani kuna vitu ambavyo labda tunashindwa kuvielewa au ni matatizo ya ufahamu wetu,
kwa Ben Mkapa kufanya mambo mema sio kujitahidi, huo ni wajibu wake na alikuwa hapo madarakani kwa sababu hiyo, kwa hiyo kama aliunyanyua uchumi, alipunguza mfumuko, ilikuwa ni wajibu wake na ndilo tulilolitegemea kutoka kwake, ni kama katika soka, uwezi kusema leo kipa kajitahidi kudaka, kawekwa golini kwa sababu hiyo,
kwa hiyo basi kwasababu Mkapa kafanya mambo ambayo yapo kinyume na matarajio yetu hapo ni lazima tumlaumu sana kwa sababu kafanya makusudi, hatukumweka hapo afanye ufisadi, kwa hiyo kwa kufanya huo ufisadi damu na vilio vya WaTanzania viko juu yake, na hayo yote aliyoyafanya kwa ufanisi yamefutwa na mabaya yote aliyoyafanya hata kama ni machache
 
Thread tamu hii, naona kabisa wana JF wnazungumza kweli ya moyoni mwao.

Tumeburuzwa wee vya kutosha, uongozi wa JK na nvyombo vyao vya hbari wametulazimisha tumseme mkapa kwa muda wa miaka minne-JUST IMAGINE 4 YRS WATU WANAMSEMA MKAPA, 4 YEARS HAKUNA REMARKABLE CHANGES ZA UONGOZI WA SASA , 4YRS JK hana kitu

BMW alikuwa ametulia, nasema , narudia tena , wenye chuk mchukueni, ila tunaompenda tupo, semeni msemavyo,

Mkapa hoyeee!
JK ziiii!!!!!!

Benjamin Mkapa quote


“Derision, cynicism, prejudice, stereotyping and hunger for stories of failure than of success will be the undoing of democratic progress on the continent.” Benjamin Mkapa quote
http://thinkexist.com/user/suggest/...cynicism-prejudice-stereotyping-and&id=727941http://thinkexist.com/common/email/...=derision-cynicism-prejudice-stereotyping-andhttp://thinkexist.com/services/book...=derision-cynicism-prejudice-stereotyping-andhttp://thinkexist.com/common/discus...=derision-cynicism-prejudice-stereotyping-and

“East Africa is an island of peace and stability surrounded by a neighborhood that is bedeviled with war, upheaval and unrest, ... We can only feel secure in our development efforts when the neighborhood is peaceful and stable.” Benjamin Mkapa quote

But the majority of people chose peace.” Benjamin Mkapa quote
 
Usijichanganye, tulia! Mie nilikuwa narudia- sana sana tu!😉
Hujanipa nini, Ideology?
Sasa mzee wangu upo wapi?? Mimi naona bora watangaze kura za Maoni kama kweli wanataka kumsafisha Mkapa!! yeye mwenyewe aliwahi kusema kuwa akiondoka watu wataanza kumshambulia sana kwa ajili ya mambo yeke alikuwa sahihi kabisa. Kama amekosea akiwa madarakani adhibiwe kama mwanadamu mwingine na pia ndio raha ya ofisi ya umma, lakini pamoja na yote haya Mkapa is better than Jk kwa utendaji na ni mkweli sana kuliko Jk, hata kama kuna watu wanakataa hivyo. then sijajua Jk huwa ana washauri wazuri kama Jk
 
Sidhani kuwa Mkapa ana kesi za kujibu. Bali ana shutuma nyingi ambazo wanaomshutumu hawajaweza hadi leo kuzifikisha mahakamni ili azijibu. Hivyo hana kesi yoyote.
 
Shuhuda zipo mimi naona Mkapa alijitahidi sana kuiwekea nchi heshima ya juu haswa katika kukuza pato la taifa na kuzima mfumuko wa bei,maisha ya mtanzania ni ya kawaida sana kwa hiyo raisi anapoweza kumuwezesha kila mtanzania angalau kula mlo mmoja bila maumivu makubwa tunasema aliweza.

Aliikuta nchi iko pabaya sana alikuwa na ziada yakutufanyia watanzania tuwe na mwelekeo wa kiuchumi ili kuwa kazi ya taabu sana kwa hiyo panapostahili tumpe sifa.

Jk makundi yanamchanganya sana anapigana vita tatu wanompinga serikalini,wanompinga katika chama chake,na wananchi na wapinzani wote wamemkalia koo,yeye mwenyewe alikosea sana kuingia kwa njia ya mtandao na kutumia vyombo vya habari kumkandia,ndio maana yamemrudia na anapoteza umaarufu kwa haraka sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…