Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 18,305
- 33,924
Kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa ni marufuku kwa vyama vya siasa kutumia majengo ya Umma na serikali kuendeshea shughuli zao za kisiasa. Lakini CCM pamoja na kupora majengo kadhaa ya umma na kuyageuza ya kwao, bado wanatumia IKULU yetu kufanyia vikao vyao.
Mbali ya hayo kwenye kikao cha CCM wameweka Bendera ya Rais kwenye kikao hicho. Hawa watu wanapenda sana kudharau mambo ya umma kwa kuyachanganya na chama chao.
Samia hapo haongozi hicho Kikao kama Rais wa watanzania bali kama Mwenyekiti wa chama chake CCM.