Ben Saanane anastahili Tuzo CHADEMA

Ben Saanane anastahili Tuzo CHADEMA

Greenwhich

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
1,337
Reaction score
968
Ni takribani miezi miwili tangu mwanachama wa Chadema Ben Saanane aibuke katika vyombo vya habari hususan mitandao mbalimbali ya kijamii na kile kinachoitwa kundi la Masalia ndani ya Chadema ambalo lilikuwa linatumiwa na CCM kuhujumu chama na ambalo lilikuwa pia na malengo ya kutukana na kukashifu viongozi wakuu wa chama kupitia mitandao ya kijamii.

Kati ya waliotajwa kuasisi na kuunda kundi hilo ni Mtela Mwampamba aliyegombea ubunge jimbo la Mbozi na Juliana Shonza
aliyekuwa Makamu Mwenyekiti BAVICHA.Ben alitoa ushahidi mbalimbali ambao kwa kiasi kikubwa ulisaidia BAVICHA kuwafukuza uanachama Mtela Mwampamba na Juliana Shonza.


Hata hivyo wako watu wachache waliolaumu na kupinga uamuzi huo na kusema vijana hao wameonewa.Hata hivyo leo yametimia baada ya vijana hao kurudi CCM na kuporomosha kila aina ya kashfa kwa chama cha Chadema na viongozi wake.

Ni ukweli ulio wazi kwamba aliyosema Ben Saanane leo yametimia pale aliposema vijana hao walikuwa wamepanga kuleta madhara makubwa ndani ya chama na hatimaye kutimkia CCM.Kutokana na ushirikiano wa Ben Saanane hatimaye vijana hawa walifukuzwa kwa hiyo hawakukamilisha mpango waliopanga kuhujumu chama.

Kuna wengine walipinga kitendo cha Ben Saanane kumhusisha Zitto Kabwe na vijana hawa mapandikizi hata hivyo vyovyote iwavyo Zitto Kabwe amebadilika sana tokea tuhuma dhidi yake zitolewe na yuko pamoja na chama katika shughuli za kukijenga tofauti na siku za nyuma.Ilikuwa ni nadra sana Zitto kushiriki maandamano ya Chadema kama alivyoungana na viongozi wenzie Jumapili ya kumlaani Spika wa bunge Zitto alishangiliwa sana Temeke Mwisho Jumapili pale alipomkaribisha Dr Slaa na kusema’’ huyu ni Rais wa watu ambaye hakutangazwa mshindi’’ Ni wazi mwenendo wa Zitto umebadilishwa na ujasiri wa Ben Saanane.

Bila unafiki wala upendeleo Chadema wanapaswa kumpongeza Ben Saanane kwa kazi kubwa aliyofanya kuwatifua Mapandikizi ya CCM na kuleta umoja na mshikamano ndani ya Chadema.
 
Last edited by a moderator:
anastahili tuzo au Nishani? Alafu Mabadiriko ya Zitto hasa ni yepi? kumuita Dr Slaa Rais au nini hasa?
 
mi mawazo yangu ni haya ZITO ni mtu ambae siasa zake zimeshindwa kutabirika na hazieleweki sio CHADEMA tu hata CCM
inavyoonekana inaonekana ZITO aliwatega CCM wamuone kama ni wao washirikiane nae ili a win simpathy kutoka ccm ili KUIVURUGA cdm KUMBE zito halikua lengo lake hilo na ushahidi ni huuu zito hajawai hata siku moja kumsema kikwete na kikwete wakati wa kampeni alitembea majimbo yote tanzani kasoro jimbo la kigoma kaskazini na viongozi wengi wa ccm waliona zito ndo sehemu ya kukimbilia kuivuruga CDM wapo vijana ambao walikua kwenye huo mkumbo bila kujijua...

kilichofata.....baada ya CCM kuona kwamba zito haelekei na wale madogo walivyotoswa bila hata zito kutoa tamko wakastuka na ikumbukwe hata huo uenyekiti wa POAC zito alipewa na kikwete kwa kuamrisha wabunge wake wampigie kura na ndio maana baada ya jaribio lao kushindwa wakaona wamkomoe kwa kufuta kamati yake sababu cheo walimpa wao na wanamuona kama mtu ambae hatabiriki nini hasa anachokitaka kwa maoni yangu hayo ndo yamejificha chini ya kapeti...ila wale madogo imekula kwao ndo mana habibu machange hajui afanyeje mpaka sasa kwenda ccm anashindwa kuomba msamaha chadema anashindwa hata chagulani wa MWANZA nae yupo kwenye mkumbo huo huo ni kama ameshapotea mwenzake matata keshajitambulisha kama yeye ni CCM SASA chagulani hajui afanyeje alitumika bila kujua linalofata kama wenzie kina habibu machange
 
kazi sana, nchi hii kila mtu njaa tupu. Hadi mi naona wenye uchungu na nchi walikwisha tangulia mbele ya haki. Wamebaki wababaishaji tupu. TUJIPANGE SANA.
 
Naunga mkono hoja kwa 100%, uliyosema yote ni ukweli mtupu bila Ben Saanane kuonyesha ujasiri wa kuweka mambo hadharani, isingekuwa rahsi hawa pandikizi wa CCM kufukuzwa ndani ya CDM, na mbele ya safari wangeleta madhara makubwa naamini hata wale ambao bado wapo CDM wamepata somo zuri la aidha kujiondoa kwy chama au kubadilika.
Kudos Ben Saanane!
 
mi mawazo yangu ni haya ZITO ni mtu ambae siasa zake zimeshindwa kutabirika na hazieleweki sio CHADEMA tu hata CCM
inavyoonekana inaonekana ZITO aliwatega CCM wamuone kama ni wao washirikiane nae ili a win simpathy kutoka ccm ili KUIVURUGA cdm KUMBE zito halikua lengo lake hilo na ushahidi ni huuu zito hajawai hata siku moja kumsema kikwete na kikwete wakati wa kampeni alitembea majimbo yote tanzani kasoro jimbo la kigoma kaskazini na viongozi wengi wa ccm waliona zito ndo sehemu ya kukimbilia kuivuruga CDM wapo vijana ambao walikua kwenye huo mkumbo bila kujijua...

kilichofata.....baada ya CCM kuona kwamba zito haelekei na wale madogo walivyotoswa bila hata zito kutoa tamko wakastuka na ikumbukwe hata huo uenyekiti wa POAC zito alipewa na kikwete kwa kuamrisha wabunge wake wampigie kura na ndio maana baada ya jaribio lao kushindwa wakaona wamkomoe kwa kufuta kamati yake sababu cheo walimpa wao na wanamuona kama mtu ambae hatabiriki nini hasa anachokitaka kwa maoni yangu hayo ndo yamejificha chini ya kapeti...ila wale madogo imekula kwao ndo mana habibu machange hajui afanyeje mpaka sasa kwenda ccm anashindwa kuomba msamaha chadema anashindwa hata chagulani wa MWANZA nae yupo kwenye mkumbo huo huo ni kama ameshapotea mwenzake matata keshajitambulisha kama yeye ni CCM SASA chagulani hajui afanyeje alitumika bila kujua linalofata kama wenzie kina habibu machange

Nakugongea 'LIKE' kubwa sana , maana umemaliza yote niliyotaka kuandika , kwa Zito kurudi kwenye Msitari CDM ndiyo kulikomgharimu POAC .
 
Back
Top Bottom