Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,810
- 11,981
Kwa mara ya kwanza katika kupindi cha miaka 22, mkutano unafanyika mwezi Mei badala ya mwezi Machi. Hii ni kutokana na serikali kujikitiza kwenye juhudi za kupambana na virusi vya Corona, na kuhakikisha usalama wa afya ya wabunge. Mkutano umefanyika sasa kwa kuwa kuna uhakika wabunge wote watakuwa salama.
Kwa mara ya kwanza Serikali ya China haijaweka makadirio ya ongezeko la uchumi (GDP) kwa mwaka huu kutokana na sintofahamu ya mwelekeo wa hali ya uchumi wa dunia.Kutokana na hali ya isiyokadiriwa ya maambukizi ya COVID-19 na hali ya kiuchumi na kibiashara duniani, maendeleo ya China yanakabiliwa na sintofahamu nyingi.
Kutokana na hali hii serikali ya China haijaweka malengo maalum la ongezeko la uchumi kwa mwaka huu.Ripoti pia imesisitiza kuwa China itaendelea nahatua ya kuzuia na kudhibiti virusi vya Corona katika kipindi kijacho, na kushughulikia vizurimaendeleo ya kiuchumi na kijamii.
======
Mkutano wa Bunge la Umma la China umefunguliwa leo mjini Beijing, baada ya kuahirishwa kwa miezi miwili kutokana a virusi vya Corona. Rais Xi Jinping na viongozi wengine wa Chama cha Kikomunisti cha China na wa serikali, pamoja na wajumbe 2,897 wa Bunge la Umma la China wamehudhuria ufunguzi wa mkutano huo. Hii ni mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 22 kwa mkutano huu kuahirishwa kutoka mwezi Machi hadi mwezi Mei kutokana na COVID-19.
Kubwa lililofanyika kwenye ufunguzi wa mkutano, ni Waziri Mkuu wa China Bw. Li Keqiang kutoa ripoti ya utendaji wa serikali katika mwaka uliopita, na ripoti ya mpango ya kazi za serikali kwa mwaka unaokuja.
Alitaja baadhi ya mambo yak
1. Mwaka jana pato la taifa la China liliongezeka kwa asilimia 6.1 na kufikia dola trilioni 13.9 za kimarekani, nafasi milioni 13.52 za ajira ziliongezeka, na idadi ya watu wenye hali duni sana kiuchumi vijijini ikipungua kwa watu milioni 11.09.
2. Mwaka huu serikali itahakikisha inawaondoa watu wote kutoka kwenye umasikini na kutokomeza umaskini, kuongeza juhudi za kusaidia vijiji maskini vilivyobaki.
3. China mwaka huu itaendelea kutekeleza sera chochezi za kifedha na sera tulivu za sarafu. China itadumisha kiwango chake cha ubadilishanaji wa fedha kuwa tulivu.
4. Serikali inapanga kuendeleza kupunguza mzigo wa kodi na gharama za uzalishaji, na kuzisaidia kampuni ndogondogo na wafanyabiashara binafsi kukabiliana na matatizo kwenye shughuli zao.
5. Serikali itahimiza uzalishaji viwandani na maendeleo ya shughuli mpya zinazojitokeza. Na itaendeleza zaidi mtandao wa Internet na kuhimiza teknolojia ya akili bandia, kwa kimombo “Artificial Intelligence (AI)”.
6. Serikali itaweka mkazo katika kuunga mkono ujenzi wa miundo mbinu ya aina mpya, kupanua matumizi ya teknolojia ya 5G.
7. Serikali itaweka kipaumbele kuleta utulivu wasoko la ajira na kulinda maisha ya watu, kushinda vita dhidi ya umasikini na kujitahidi kufikia lengo la kukamilisha kazi ya ujenzi wa jamii yenye maisha bora kwa pande zote mwaka huu.
8. Serikali itapunguza ukiritimba kwenye sekta zilizozuiliwa kwa uwekezaji kutoka nje kuingia kwenye soko la China, kuweka orodha ya sekta zinazozuiliwa kwa huduma na biashara nje ya nchi, na kuyapatia maeneo ya majaribio ya biashara huria haki zaidi ya kujiamulia juu ya mageuzi na kufungua mlango.
9. Serikali itaimarisha utaratibu wa afya ya umma, kwa kutoa msisitizo kwenye kujali maisha, kufanya mageuzi ya mfumo wa kukinga na kudhibiti magonjwa, kuboresha mfumo wa utoaji wa tahadhari na taarifa kuhusu magonjwa ya kuambukiza, kuendelea kutoa habari kwa uwazi kuhusu maambukizi.
10. Serikali itaunga mkono maendeleo ya uchumi wa Hong Kong na Macau, kuboresha maisha ya umma, kuunganisha maendeleo ya maeneo hayo katika mpango wa ujumla wa maendeleo ya taifa.
Kwa mara ya kwanza Serikali ya China haijaweka makadirio ya ongezeko la uchumi (GDP) kwa mwaka huu kutokana na sintofahamu ya mwelekeo wa hali ya uchumi wa dunia.Kutokana na hali ya isiyokadiriwa ya maambukizi ya COVID-19 na hali ya kiuchumi na kibiashara duniani, maendeleo ya China yanakabiliwa na sintofahamu nyingi.
Kutokana na hali hii serikali ya China haijaweka malengo maalum la ongezeko la uchumi kwa mwaka huu.Ripoti pia imesisitiza kuwa China itaendelea nahatua ya kuzuia na kudhibiti virusi vya Corona katika kipindi kijacho, na kushughulikia vizurimaendeleo ya kiuchumi na kijamii.
======
Mkutano wa Bunge la Umma la China umefunguliwa leo mjini Beijing, baada ya kuahirishwa kwa miezi miwili kutokana a virusi vya Corona. Rais Xi Jinping na viongozi wengine wa Chama cha Kikomunisti cha China na wa serikali, pamoja na wajumbe 2,897 wa Bunge la Umma la China wamehudhuria ufunguzi wa mkutano huo. Hii ni mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 22 kwa mkutano huu kuahirishwa kutoka mwezi Machi hadi mwezi Mei kutokana na COVID-19.
Kubwa lililofanyika kwenye ufunguzi wa mkutano, ni Waziri Mkuu wa China Bw. Li Keqiang kutoa ripoti ya utendaji wa serikali katika mwaka uliopita, na ripoti ya mpango ya kazi za serikali kwa mwaka unaokuja.
Alitaja baadhi ya mambo yak
1. Mwaka jana pato la taifa la China liliongezeka kwa asilimia 6.1 na kufikia dola trilioni 13.9 za kimarekani, nafasi milioni 13.52 za ajira ziliongezeka, na idadi ya watu wenye hali duni sana kiuchumi vijijini ikipungua kwa watu milioni 11.09.
2. Mwaka huu serikali itahakikisha inawaondoa watu wote kutoka kwenye umasikini na kutokomeza umaskini, kuongeza juhudi za kusaidia vijiji maskini vilivyobaki.
3. China mwaka huu itaendelea kutekeleza sera chochezi za kifedha na sera tulivu za sarafu. China itadumisha kiwango chake cha ubadilishanaji wa fedha kuwa tulivu.
4. Serikali inapanga kuendeleza kupunguza mzigo wa kodi na gharama za uzalishaji, na kuzisaidia kampuni ndogondogo na wafanyabiashara binafsi kukabiliana na matatizo kwenye shughuli zao.
5. Serikali itahimiza uzalishaji viwandani na maendeleo ya shughuli mpya zinazojitokeza. Na itaendeleza zaidi mtandao wa Internet na kuhimiza teknolojia ya akili bandia, kwa kimombo “Artificial Intelligence (AI)”.
6. Serikali itaweka mkazo katika kuunga mkono ujenzi wa miundo mbinu ya aina mpya, kupanua matumizi ya teknolojia ya 5G.
7. Serikali itaweka kipaumbele kuleta utulivu wasoko la ajira na kulinda maisha ya watu, kushinda vita dhidi ya umasikini na kujitahidi kufikia lengo la kukamilisha kazi ya ujenzi wa jamii yenye maisha bora kwa pande zote mwaka huu.
8. Serikali itapunguza ukiritimba kwenye sekta zilizozuiliwa kwa uwekezaji kutoka nje kuingia kwenye soko la China, kuweka orodha ya sekta zinazozuiliwa kwa huduma na biashara nje ya nchi, na kuyapatia maeneo ya majaribio ya biashara huria haki zaidi ya kujiamulia juu ya mageuzi na kufungua mlango.
9. Serikali itaimarisha utaratibu wa afya ya umma, kwa kutoa msisitizo kwenye kujali maisha, kufanya mageuzi ya mfumo wa kukinga na kudhibiti magonjwa, kuboresha mfumo wa utoaji wa tahadhari na taarifa kuhusu magonjwa ya kuambukiza, kuendelea kutoa habari kwa uwazi kuhusu maambukizi.
10. Serikali itaunga mkono maendeleo ya uchumi wa Hong Kong na Macau, kuboresha maisha ya umma, kuunganisha maendeleo ya maeneo hayo katika mpango wa ujumla wa maendeleo ya taifa.