Bei ya SUKARI mikoa mbalimbali Tanzania

Shindu Namwaka

JF-Expert Member
Sep 22, 2014
4,911
3,080
Ikiwa serikali imetoa tamko la sukari kushuka bei kufikia sh.1800 kwa gk1 bado bidhaa hiyo tunanunua sh.2200 kwa wateja wa reja reja wakati wateja wa jumla wakinunua sh.50000 hadi sh.49000 kwa kg25.

Ni wazi kuwa sukari sasa imezidi kupaa bei kila uchao, sehemu nyingi sasa bei ni elfu 3 kwa kilo, maamuzi ya Rais wetu mpendwa Magufuli naona aliya fanya haraka mno,wananchi wa chini sasa ndo wanaoumia zaidi.

Badala ya kupata unafuu ulikusudiwa sasa linaelekea kuwa janga. Najiuliza hapo ni sukari tu je angetangaza kupiga marufuku kuagiza na bidhaa zingine hali ingekuwaje? Kama sukari tu imeleta shida.
 
Kuna watu hawaamini kuwa enzi hizi na za mwalimu Nyerere ni tofauti kabisa. Hakuna namna nyingine y kushusha bei za vitu usivyozalisha wala kuuza wewe bila kupunguza kodi.

Serikali ni wakati sasa isishindane na nguvu ya soko bali iangalie namna ya kuingilia kwa mifumo stahiki. Serikali ingeweza kupunguza kodi ambayo itaakisi kupungua kwa bei.
 
Bodi ya Sukari hawakujiandaa kabla ya kutangaza bei Elekezi...


Lango lao ilikuwa ni ili waandikwe ktk Media.... Hawana lolote la Maana.
 
Demand and supply is only the reason for price of products to decline and when other factors remain constant
 
Sijui kama agizo la Rais limepuuzwa ama mheshimiwa alipotoka, tuliambiwa kuwa sukari inatakiwa kuuzwa kwa shilingi 1800 kwa kilo 1, ila bei haijashuka na bado inaendelea kupanda, bei ya sukari kwa bei ya jumla imepanda kutoka shilingi 82,000 kwa ujazo wa mfuko wa kilo 50 mpaka 98,000, ikiwa ni ongezeko la shilingi 16,000.

Mfanyabiashara huyu ili apate faida inabidi auze kwa shilingi 2,200 ambapo atapata faida ya shilingi 9,800, ni hasara kuuza kwa shilingi 1,800 kwa kilo wakati bei ya jumla sukari inauzwa 98,000 kwa kilo 50 (hasara ya shilingi 8,000 na ikumbukwe mifuko hii ya kilo 50 huwa haiwi kamili, mara nyingi ni kilo 49).

Mheshimiwa amesema, kama ni mfanyabiashara na ufanye biashara kweli kweli ili kukuza uchumi, kwa hesabu ndogo tu hapo ni biashara gani itafanyika?

HII NI BEI YA SUKARI YA JUMLA KWA DODOMA MJINI KWA SIKU YA LEO TAREHE 31/03/2016.
 
Hata jana huko Ntwara kwetu niliulizia nikaambiwa kilo moja ni 2200/= nikajisemea moyoni........hii Nchi ss maneno yanazidi kuwa mingi zaidi ya kawaida.
 
Serikali hii ya awamu ya tano ni ngumu kuielewa, walizunguka kwenye viwanda vya sukari wakasema iko tele na kupanga bei elekezi, jana mbunge anasema vitolewe vibali kuagiza sukari ya nje, eti ila waagizaji wasiagize, NYINGI sana! hajasema nyingi ni kuanzia tani ngapi, rais alisema sukari ya nje marufuku, haya rais alisema hakuna michango mashuleni tena tunaambiwa michango ni kwa vibali maalumu, kuielewa hii serikali ya WAPIGA PICHA inahitaji akili ya mwendawazimu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom