Bei ya Mashine za Kukoboa na Kusaga

Bei ya Mashine za Kukoboa na Kusaga

Kumbuka pia kuwa ufungaji wa mashine za Diesel hasa kwa maeneo ya mjini ni tatizo kubwa sana kutokana na noise level- hutoa kelele sana wakati wa kusaga mahindi. Ni swala la mazingira pia. unaweza usipate kibali kutoka kwa mamlaka husika hasa halmashauri. Ni wazo tu hasa kama lengo lako lilikuwa ni kufunga maeneo ya mjini.
Sijawahi tumia kufanya biashara ya unga kwa mashine za Diesel. Ingekuwa za umeme ningekupa shule ya kutosha. nina uzoefu katika eneo husika.
 
Nilifika Cambodia nikakuta wanatumia injini za magari madogo especially Corolla kuendeshea hizi mashine na hata boti za uvuvi. Wataalamu hasa mmteule hebu tushaurini.
 
Last edited by a moderator:
Nilifika Cambodia nikakuta wanatumia injini za magari madogo especially Corolla kuendeshea hizi mashine na hata boti za uvuvi.


Mkuu uko Sahihi kabisa, ila kuna kifaa fulan kinaitwa Changer kinahusika na aina hii ya Mota ili iweze kutumika kwa kazi hiyo. Trekta zinatumika sana hasa maeneo ya Wilaya za Magu na Bariadi. Ingawa kwa sasa utumiaji wa Engine ulizotaja haupo kabisa kutokana na Ujio wa Injin za Kichina yaan JD, DF nk ambazo ni rahisi kununua na kuziendesha pia. Kabla ya Ujio wa Injin hizi za kichina kulikuwa na Injini za Mjeruman kama LISTER PETER, DEUTZ nk ambazo zilikua zikiuzwa Mil.. 6 - 12 hivyo hali hii iliwasukuma watu wengi kutumia Injin za Colora, Isuzu, 110 matreketa nk. Lkn kwa sasa injin za mchina hata Lak 6 unapata na unaanzisha kazi ya kusaga.
 
Wadau kumbukeni kwamba, unapomiliki Mashine ya Kusaga ya Mafuta eneo ambalo halina Umeme fursa kubwa ni UFUAJI WA UMEME. Mota yako ya Kusaga yenye Ukubwa wa HP 20 Inaweza kuzalisha umeme wa kulisha zaidi ya Nyumba/familia 100 kwa matumizi ya kuwasha taa tu. Familia 1 itakulipa Tshs. 10,000 kwa mwezi na wenye Guest watakulipa Tshs 50,000 kwa mwezi. Endapo utakua eneo zuri aina hii ya biashara faida yake kwa mwezi ni zaidi ya Mil. 1 kwa mwezi. Hasa maeneo ya kambi za wachimba madini na Uvuvi ni sehemu sahihi kabisa kuvuna kipato hiki. Lkn pia mota yako inaweza kuvuta maji kutoka ziwani, Mtoni nk na kuyajaza kwenye matenki na kuyasambaza kwa walaji kwa bei mliyokubaliana. Haya yote yanawezekana kwa Mota yako ya Mchina ya Lak 9.5 ambayo utaifanya kadri utakavyo hata kutengeneza gari ya mizigo inakubali tu ni utaalam tu unatumika. Thats why ukienda site za Ujenzi za Wachina utasikia Vigari vyao vinatoa muungurumo, na kwa sasa METL ametumia Injin hizi kutengeneza Bajaj ambazo zinasambaza bidhaa jijin Dsm.
 
Wadau kumbukeni kwamba, unapomiliki Mashine ya Kusaga ya Mafuta eneo ambalo halina Umeme fursa kubwa ni UFUAJI WA UMEME. Mota yako ya Kusaga yenye Ukubwa wa HP 20 Inaweza kuzalisha umeme wa kulisha zaidi ya Nyumba/familia 100 kwa matumizi ya kuwasha taa tu. Familia 1 itakulipa Tshs. 10,000 kwa mwezi na wenye Guest watakulipa Tshs 50,000 kwa mwezi. Endapo utakua eneo zuri aina hii ya biashara faida yake kwa mwezi ni zaidi ya Mil. 1 kwa mwezi. Hasa maeneo ya kambi za wachimba madini na Uvuvi ni sehemu sahihi kabisa kuvuna kipato hiki. Lkn pia mota yako inaweza kuvuta maji kutoka ziwani, Mtoni nk na kuyajaza kwenye matenki na kuyasambaza kwa walaji kwa bei mliyokubaliana. Haya yote yanawezekana kwa Mota yako ya Mchina ya Lak 9.5 ambayo utaifanya kadri utakavyo hata kutengeneza gari ya mizigo inakubali tu ni utaalam tu unatumika. Thats why ukienda site za Ujenzi za Wachina utasikia Vigari vyao vinatoa muungurumo, na kwa sasa METL ametumia Injin hizi kutengeneza Bajaj ambazo zinasambaza bidhaa jijin Dsm.

Barikiwa sana mkuu!!,yaani umenipa maujanja ya kutosha.
 
mmteule vp mashine za kujibia mpunga gharama zake
 
Last edited by a moderator:
um
Wadau kwa Uzoefu wangu wa Kufanya biashara nimegundua Kuwa Biashara ambayo ni non mobile yaan iliyotulia sehemu maalum au isiyohamishika ina changamoto chache mno ukilinganisha na ile ya kuhamahama. Kwa biashara ya Mashine changamoto kubwa ni VIPURI FEKI, MGAO WA UMEME na Ubabaishaji wa Wafanyakazi. Zingatia unaponunua Vifaa vya Mashine yako ununue VIFAA GENUINE INGAWA VITAKUA BEI AGHALI LKN UTAFAIDI ZAIDI. mf. Switch ya kuwasha Mashine FEKI INAUZWA LAK 2 Kkoo, Lkn ukienda kwa Dealer wa Vifaa vya MEM ya Uingereza vifaa ambavyo utapewa Grantii ya Miaka 20 hiyo Starter wanauza Lak 4.5
ukijiloga ukanunua starter feki ya lak 2 kwa mwaka itaungua zaidi ya Mara 6 au zaidi so wewe utakua daily ni kwenda kununua spea. Tujitahidi kutafuta vifaa imara. Wenzetu wanasema CHEAP IS EXPENSIVE
umetuelimisha vya kutosha Thank u
 
Bei kwa Injini ya 20 HP ni Ths. 950,000 zinapatikana kwa Wingi mtaa wa India duka la KILIMO BORA.
Kaka MTEULE MUNGU AKIPE KILALAKHERI KATIKA MAISHA YAKO. samahani naomba unifanyie outline ya kila kitu na bei yake katika mradi huu, kuna jamaa anataka kuanzisha sasa naona kama anataka kunipiga za uso.

Nakuomba uorodheshe vifaa vinavyotakiwa ikiwa ni pamoja na vya umeme na gharama za installation za umeme. Nitashukuru sana.
 
Mashine ya Kusaga ama kukoboa ina sehemu mbili. INJINI na KINU.
INJINI / MOTA zinapatikana kwa ukubwa tofauti yaan Horse Power mbalimbali. Eg. HP 12, 15, 20 na kuendelea. Injini nzuri kwa kupiga mzigo na Ulaji mzuri wa Mafuta ni HP 20 bei yake ni 950,000 aina ya Jiang Dong JD, ama DF ama AMEC zote za mchina. Usinunue Lister Peter.
Ukisha nunua Injini unanunua kinu cha Kusaga na kukoboa vinapatikana Sido ama kwa mafundi wa kuchomelea kwa bei ya 500,000-700,000 kutegemea na makubaliano.
Baada ya hapo utasimika mashine yako eneo ulilochagua. Note.... Injini moja inaweza kuvuta vinu viwili katika jengo lako kinachotakiwa ni kutafuta fundi mtaalamu. Ukiwa Dsm Injini zinapatikana Mtaa wa India duka la Jumla la Injini hizo linaitwa KILIMO BORA, AU AGRO METRO. Ukiwa Mwanza duka la Injini lipo Mtaa wa Rwagasore linaitwa SHYMOND.
Endapo utasimika mashine yako kwa usahihi kabisa Kila dumu la Lita ishirini la Diesel faida yake ni Tshs. 60,000 - 80,000 kulingana na bei ya Kusagiaa.
Karibu kwenye biashara isiyo na stress Mkuu.
Ni jambo gani la kuzingatia wakati wa kuchagua huo ukubwa wa hp mf kama ninunue hp 12 au hp 20.

Vipi kuna hizi mashine za mchina mabazo nafikiri kwa muundo ninavyouona naona kama motor na kinu ni in-built,je mashine za mchina (vinu)sio nzuri? maana nipo inpressed nazo sana kwakuwa ni dustless,noiseless,ulaji wa umeme wanasema ni mdogo sana,quality ya unga nayo wanaandika kuwa ni wa kiwango cha juu sana.Je,ubora wa hizo mashine hasa motor na kinu ni mzuri?
 
Wadau naona kuna Maswali ya Tangu Nov. 2015 bado hayana majibu yaan nilikua sijapitia post za wadau. Huu uzi ni darasa tosha lkn nashangaa Mods wanauficha sana huu Uzi. Kuna maswali ya Mashine za Kukoboa Mpunga, Mashine za Kusaga kuorodhesha mahitaji yoote ntayatolea majibu. Tujikite sana hii biashara haiumiz Kichwa. Tulioko Mbarali, Mpanda, Sumbawanga, Ifakara wekezeni Kujenga Magodown yenye Mashine za kukoboa Mpunga nimefika huko pesa ziko nje nje sana.
 
Wadau naona kuna Maswali ya Tangu Nov. 2015 bado hayana majibu yaan nilikua sijapitia post za wadau. Huu uzi ni darasa tosha lkn nashangaa Mods wanauficha sana huu Uzi. Kuna maswali ya Mashine za Kukoboa Mpunga, Mashine za Kusaga kuorodhesha mahitaji yoote ntayatolea majibu. Tujikite sana hii biashara haiumiz Kichwa. Tulioko Mbarali, Mpanda, Sumbawanga, Ifakara wekezeni Kujenga Magodown yenye Mashine za kukoboa Mpunga nimefika huko pesa ziko nje nje sana.
Ok,nijibu swali hapo juu.
 
Mashine ya Kusaga ama kukoboa ina sehemu mbili. INJINI na KINU.
INJINI / MOTA zinapatikana kwa ukubwa tofauti yaan Horse Power mbalimbali. Eg. HP 12, 15, 20 na kuendelea. Injini nzuri kwa kupiga mzigo na Ulaji mzuri wa Mafuta ni HP 20 bei yake ni 950,000 aina ya Jiang Dong JD, ama DF ama AMEC zote za mchina. Usinunue Lister Peter.
Ukisha nunua Injini unanunua kinu cha Kusaga na kukoboa vinapatikana Sido ama kwa mafundi wa kuchomelea kwa bei ya 500,000-700,000 kutegemea na makubaliano.
Baada ya hapo utasimika mashine yako eneo ulilochagua. Note.... Injini moja inaweza kuvuta vinu viwili katika jengo lako kinachotakiwa ni kutafuta fundi mtaalamu. Ukiwa Dsm Injini zinapatikana Mtaa wa India duka la Jumla la Injini hizo linaitwa KILIMO BORA, AU AGRO METRO. Ukiwa Mwanza duka la Injini lipo Mtaa wa Rwagasore linaitwa SHYMOND.
Endapo utasimika mashine yako kwa usahihi kabisa Kila dumu la Lita ishirini la Diesel faida yake ni Tshs. 60,000 - 80,000 kulingana na bei ya Kusagiaa.
Karibu kwenye biashara isiyo na stress Mkuu.
Mkuu kama ulikuwa kwenye akili yangu vile
 
Mkuu Nyundo/The Hummer. Kinachokuongoza kuchagua Ukubwa wa Injini uitakayo kwenye biashara yako ni;
1. WINGI wa Kazi Jinsi ulivyo. Eneo ambalo wateja ni wachache sana Mf. Unasaga magunia mawili kwa siku lazima upate hata HP 16 inatosha. Lkn eneo ambalo Mzigo ni mkubwa asbh mpaka jioni mota inafanyakazi Hakika hapo HP 20 - 40 inakuhusu.
2. MTAJI, mashine ndogo bei iko chini na kubwa ni vice versa. Hivyo kama unamtaji mdogo utanunua 16 HP na kama unajiweza utanunua 20 na zaid
3. USHINDANI, Mota ya 16 hp inasaga debe moja la mahindi kwa dkk 10 na zaid wakati ile ya 20 hp ni dkk 6 na ile ya 30 hp dkk 3 kwahiyo jipime mwenyewe. Je mteja ataendelea kupanga mstari kwako wakati pembeni yako kuna mtambo wa 40 hp gunia moja ni kufumba na kufumbua anaondoka na unga wake.
4. NGUVU YA UMEME Kwenye laini yako ya TANESCO. Endapo unatumia mashine ya Umeme Ukubwa wa Mota yako unaweza kuathiriwa na Msongo wa Umeme wa TANESCO. Kama uko kwenye maeneo yenye Low Voltage 16 hp inakuhusu na kama sio ni vice versa.
5. Lengo la Kununua Mota, Endapo umelenga Mota ya Biashara means Unataka FAIDA, ili upate faida gharama za uendeshaji lazima zisizidi mapato. Hivyo Mota ya kati yaani 20 HP ni the Most Economical kwani inatumia kiwango kidogo cha Umeme na Ina mwendokasi wa kuridhisha pia. Lkn ile ya 40 hp inatafuna Unit za Umeme mpaka uone biashara ni chungu. Lkn endapo lengo la Mota ni Kutoa huduma Jamii zisizo Za kibiashara 30 to 40 hp inakuhusu kwa mantiki kwamba huitaj faida bali kuipa huduma jamii.
Hivyo basi kabla ya kununua Mota fanya Study ya eneo lako la Biashara kujua lina Demand kiasi gani, lina Ushindani upi, Umeme nguvu ikoje nk nk? Ni hayo tu wadau.
 
Hapo mmteule nimekupata vizuri kabisa kuhusu hizo hp nilikuwa sizifahamu kabisa nilikuwa najuwa ni nguvu ya machine but how ndo nilikuwa gizani.

Vipi kuhusu vinu vya kichina,maana wanavi-promote kuwa ni dustless,noiseless(hizi mbili zinaleta shida mtu permanent wa ku-run machime),matumizi madogo ya umeme(hii inamu-affect Boss) na quality ya unga(hii ina-affect wateja).Je,unazifahamu vyema hizo machine na kati ya hizo na hizi za SIDO kila moja ina disadvantage gani hasa durability na mengineyo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom