Bei ya Mashine za Kukoboa na Kusaga

Bei ya Mashine za Kukoboa na Kusaga

Kiukweli sijawahi kutumia Kinu cha Mchina. Na hata ikitokea nikakinunua hua napeleka karakana za Kibongo nakifanyia modification kwa jinsi itakayonipa faida. Hizo model za Dustless na Noiseless sijaziona.
Note; Kinu kikiwa na muundo unaochelewesha feni kuhamisha unga uliosagwa kwenda kwenye pipa la Oulet ni hasara.
Kinu kikiwa na plate nyembaba/sahani zinazobeba meno/nyundo ni hasara.
Kinu kikiwa chembamba less than inch 6 ni hasara.
Ridges(mf. Kinywani mwako kwa juu kuna matuta pia yamo ndani ya kinu cha mashine) ndani ya kinu chako ndiyo silaha ya kutwanga nafaka hakikisha hizo ridges zinakua hai muda wote. Endapo zitaisha utachomea nondo ama flat bars.
Aidha, Quality ya Unga inategemea na NAMBA YA CHEKECHEO unalotumia. Endapo utatumia chekecheo lenye macho/matundu makubwa Utapata faida kubwa ila mteja atapata unga ambao unachenga nyingi. Endapo utatumia Chekecheo lenye macho madogo means Unga utakua laini sana bila chenga na mteja atafurahia huduma lkn badala ya kusaga debe 1 dkk 6 now kwa chekecheo dogo unaweza tumia dkk 2 zaid. Kikubwa ni kutafuta chekecheo la kati ambalo ni standard. Pia hakikisha kabla ya kuanza kusaga unachunguza Chekecheo ndani ya kinu, endapo lina pancha litoe uzibe kwa Kuchomelea na Gesi ama weka jingine. Pia wakati wa kuweka chekecheo hakikisha Umeikata kwa vipimo sahihi ambavyo haviachi nafasi ya kupitisha chenga, hakikisha umeifitisha kwenye Kinu bila kuachwa mwanya wowote. Zima mota mara moja endapo utasikia chuma ama kitu chochote kisicho nafaka kimeingia ndani ya kinu na kuleta mtafaruku na ufungue mfuniko wa kinu kuchunguza madhara kabla ya kuendelea na huduma.
 
20000101_053941.jpeg
20000101_054044.jpeg


Post sent using JamiiForums mobile app
 
Gharama za Kuanzisha mashine ya Umeme.
Mota 20hp 1470 rpm Tshs 1 Mil, Kinu Lak 7, Starter ya MEM genuine Lak 4.5, Main Switch Lak 5, Control Lak 4, Tanesco Mil 2-3, Cables Lak 6 nk..
Note... Unaponunua Mota uwe makini usichukue Mota Hp kuuuubwa ukaishia kuifaidisha Tanesco, zingatia vipimo ili kuokoa matumiz ya Umeme yasiyo ya lazma ili upate faida zaidi.
Chekecheo la kinu chako pia ni mbinu ya kupata faida zaidi... Ni somo lefu Karibun kwa maswali zaidi.
Naomba kuuliza, machine hizi zinaweza kufungwa kwenye kiwanda cha unga?? Kama nataka kuanzisha kiwanda cha kusaga na kupack unga, machine hizi zinafaa??

Sent from my Startimes Nova N5 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu Nyundo/The Hummer. Kinachokuongoza kuchagua Ukubwa wa Injini uitakayo kwenye biashara yako ni;
1. WINGI wa Kazi Jinsi ulivyo. Eneo ambalo wateja ni wachache sana Mf. Unasaga magunia mawili kwa siku lazima upate hata HP 16 inatosha. Lkn eneo ambalo Mzigo ni mkubwa asbh mpaka jioni mota inafanyakazi Hakika hapo HP 20 - 40 inakuhusu.
2. MTAJI, mashine ndogo bei iko chini na kubwa ni vice versa. Hivyo kama unamtaji mdogo utanunua 16 HP na kama unajiweza utanunua 20 na zaid
3. USHINDANI, Mota ya 16 hp inasaga debe moja la mahindi kwa dkk 10 na zaid wakati ile ya 20 hp ni dkk 6 na ile ya 30 hp dkk 3 kwahiyo jipime mwenyewe. Je mteja ataendelea kupanga mstari kwako wakati pembeni yako kuna mtambo wa 40 hp gunia moja ni kufumba na kufumbua anaondoka na unga wake.
4. NGUVU YA UMEME Kwenye laini yako ya TANESCO. Endapo unatumia mashine ya Umeme Ukubwa wa Mota yako unaweza kuathiriwa na Msongo wa Umeme wa TANESCO. Kama uko kwenye maeneo yenye Low Voltage 16 hp inakuhusu na kama sio ni vice versa.
5. Lengo la Kununua Mota, Endapo umelenga Mota ya Biashara means Unataka FAIDA, ili upate faida gharama za uendeshaji lazima zisizidi mapato. Hivyo Mota ya kati yaani 20 HP ni the Most Economical kwani inatumia kiwango kidogo cha Umeme na Ina mwendokasi wa kuridhisha pia. Lkn ile ya 40 hp inatafuna Unit za Umeme mpaka uone biashara ni chungu. Lkn endapo lengo la Mota ni Kutoa huduma Jamii zisizo Za kibiashara 30 to 40 hp inakuhusu kwa mantiki kwamba huitaj faida bali kuipa huduma jamii.
Hivyo basi kabla ya kununua Mota fanya Study ya eneo lako la Biashara kujua lina Demand kiasi gani, lina Ushindani upi, Umeme nguvu ikoje nk nk? Ni hayo tu wadau.
Ivi kuna uwezekano wa kutumia mota moja kwa kusaga na kukoboa?
 
Mashine ya Kusaga ama kukoboa ina sehemu mbili. INJINI na KINU.
INJINI / MOTA zinapatikana kwa ukubwa tofauti yaan Horse Power mbalimbali. Eg. HP 12, 15, 20 na kuendelea. Injini nzuri kwa kupiga mzigo na Ulaji mzuri wa Mafuta ni HP 20 bei yake ni 950,000 aina ya Jiang Dong JD, ama DF ama AMEC zote za mchina. Usinunue Lister Peter.
Ukisha nunua Injini unanunua kinu cha Kusaga na kukoboa vinapatikana Sido ama kwa mafundi wa kuchomelea kwa bei ya 500,000-700,000 kutegemea na makubaliano.
Baada ya hapo utasimika mashine yako eneo ulilochagua. Note.... Injini moja inaweza kuvuta vinu viwili katika jengo lako kinachotakiwa ni kutafuta fundi mtaalamu. Ukiwa Dsm Injini zinapatikana Mtaa wa India duka la Jumla la Injini hizo linaitwa KILIMO BORA, AU AGRO METRO. Ukiwa Mwanza duka la Injini lipo Mtaa wa Rwagasore linaitwa SHYMOND.
Endapo utasimika mashine yako kwa usahihi kabisa Kila dumu la Lita ishirini la Diesel faida yake ni Tshs. 60,000 - 80,000 kulingana na bei ya Kusagiaa.
Karibu kwenye biashara isiyo na stress Mkuu.
Nimekupata mkuu hata mimi nikipata mtaji nitajiunga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumbuka pia kuwa kutumia Engine au Motor moja kuendesha Kinu cha kusaga na kukoboa kunakulazisha kutoa mikanda endapo moja ya kinu hakitumiki wakati huo. Ni risk pia kwa kuwa mikanda huwa haiwekewi guide ya kuzuia ajali endapo inakatika ghafla. Pia inaongeza idle time kwa kuwa lazima kinu kimoja usitumie kutokana na ukweli kuwa mzunguko wa kinu cha kusaga speed yake ni tofauti na cha kukoboa, yet Motor/Engine inayotumika ni moja. Practically it is quite impossible kuendesha vinu vyote viwili simultaneously. ...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Gharama za Kuanzisha mashine ya Umeme.
Mota 20hp 1470 rpm Tshs 1 Mil, Kinu Lak 7, Starter ya MEM genuine Lak 4.5, Main Switch Lak 5, Control Lak 4, Tanesco Mil 2-3, Cables Lak 6 nk..
Note... Unaponunua Mota uwe makini usichukue Mota Hp kuuuubwa ukaishia kuifaidisha Tanesco, zingatia vipimo ili kuokoa matumiz ya Umeme yasiyo ya lazma ili upate faida zaidi.
Chekecheo la kinu chako pia ni mbinu ya kupata faida zaidi... Ni somo lefu Karibun kwa maswali zaidi.
Samahani Mkuu, vinu vya kusaga vina size tofauti. Je, ni size gani inarandana na Mota ya 20hp? Pia kwa upande wa kukoboa ni mota size gani ndio nzuri?
 
Mwaka 2015 population ilikuwa mil 45, leo 2017 population ni karibia 49. Tathmin mwenyewe mahitaji ya chakula yameongezeka au yamepungua. Biashara ya chakula haiji kudoda
my concern ni kwamba kwa hali ya sasa biashara nyingi zimedorora kutokana na mzunguko wa pesa...sasa je hii biashara haijaguswa??

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom