Bei ya mafuta yashuka-upuuzi mwingine wa ewura

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,150
Bei ya mafuta yashuka


na Betty Kangonga


amka2.gif

BEI ya mafuta ya petroli na dizeli nchini imeshuka baada ya kutokea mabadiliko katika soko la dunia na kupanda kwa thamani ya shilingi ikilinganishwa na dola ya Marekani.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), Haruna Masebu, inaeleza kwamba bei za rejareja kwa aina zote za mafuta imeshuka ikilinganishwa na toleo la mwezi uliopita.
“Taarifa hiyo inaeleza kwamba petroli imeshuka kwa asilimia 3.7), dizel asilimia 4.92 na mafuta ya taa asilimia 6.86; na wafanyabiashara wanatakiwa kuelewa kwamba ni kosa kwa kituo kuuza mafuta bila kuweka mabango ya bei inayoonekana vizuri kwa wateja,” ilieleza taarifa hiyo.
Aidha, kwa mujibu wa sheria ya mafuta ya mwaka 2008, bei ya bidhaa hizo itaendelea kupangwa na soko. Hivyo mamlaka husika itaendelea kuhamasisha ushindani kwa kutoa taarifa za bei elekezi pamoja na bei ya kikomo. Taarifa hiyo inaeleza zaidi kuwa kampuni za mafuta zipo huru kuuza bidhaa hiyo kwa bei ya ushindani ili mradi ziwe chini ya bei ya kikomo ambayo ni asilimia 7.5 ya bei elekezi. Pia inaelekeza mnunuzi kuhakikisha anapata stakabadhi ya malipo inayoonyesha jina la kituo, tarehe na aina ya mafuta aliyonunua na bei kwa lita kwani ndiyo kidhibiti endapo yanajitokeza malalamiko ya ama kuuziwa kwa bei ya juu kuliko ya kikomo au kuuziwa mafuta yasiyokuwa na kiwango.


h.sep3.gif


wakati wakisema haya

PETROL 1500-1585

DIESEL 1300-1425

HUU UPUUZI WAO SIJUI WATAUCHA LINI..NAHISI KUNA WATU WANA MAKAMPUNI YA MAFUTA NDIO MAANA MGONGANO WA MASLAHI INAKUWA SHIDA KUPUNGUZA...
 
Bei ya mafuta yashuka


na Betty Kangonga


amka2.gif

BEI ya mafuta ya petroli na dizeli nchini imeshuka baada ya kutokea mabadiliko katika soko la dunia na kupanda kwa thamani ya shilingi ikilinganishwa na dola ya Marekani.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), Haruna Masebu, inaeleza kwamba bei za rejareja kwa aina zote za mafuta imeshuka ikilinganishwa na toleo la mwezi uliopita.
“Taarifa hiyo inaeleza kwamba petroli imeshuka kwa asilimia 3.7), dizel asilimia 4.92 na mafuta ya taa asilimia 6.86; na wafanyabiashara wanatakiwa kuelewa kwamba ni kosa kwa kituo kuuza mafuta bila kuweka mabango ya bei inayoonekana vizuri kwa wateja,” ilieleza taarifa hiyo.
Aidha, kwa mujibu wa sheria ya mafuta ya mwaka 2008, bei ya bidhaa hizo itaendelea kupangwa na soko. Hivyo mamlaka husika itaendelea kuhamasisha ushindani kwa kutoa taarifa za bei elekezi pamoja na bei ya kikomo. Taarifa hiyo inaeleza zaidi kuwa kampuni za mafuta zipo huru kuuza bidhaa hiyo kwa bei ya ushindani ili mradi ziwe chini ya bei ya kikomo ambayo ni asilimia 7.5 ya bei elekezi. Pia inaelekeza mnunuzi kuhakikisha anapata stakabadhi ya malipo inayoonyesha jina la kituo, tarehe na aina ya mafuta aliyonunua na bei kwa lita kwani ndiyo kidhibiti endapo yanajitokeza malalamiko ya ama kuuziwa kwa bei ya juu kuliko ya kikomo au kuuziwa mafuta yasiyokuwa na kiwango.


h.sep3.gif


wakati wakisema haya

PETROL 1500-1585

DIESEL 1300-1425

HUU UPUUZI WAO SIJUI WATAUCHA LINI..NAHISI KUNA WATU WANA MAKAMPUNI YA MAFUTA NDIO MAANA MGONGANO WA MASLAHI INAKUWA SHIDA KUPUNGUZA...
Ama kweli huu ni upuuzi mwingine kama ulivyosema. Hakuna mtu asiyejua kuwa huwezi kupata Petrol mahali popote bila na kuwa na 1440 - 1550.

Shame on you EWURA
 
EWURA wana mitindio ya ubongo kama siyo vichaa jumla. nafikiri wapandishe bei maana siku zote wanatutishia
 
mpaka sasa sijaona kazi au jukumu la EWURA bora tu ifutwe, ili tuende wenyewe
 
hivi JojiPoji hiyo kwenye avatar yako ni nini..au macho yangu hayaoni vizuri?
 
EWURA ilianzishwa kwa nia na madhumuni ya kusimamia mtumiaji (consumer) asiumizwe na syndicate za walafi wasioridhika na faida kiasi, matokeo; EWURA imekuwa inahalalisha upandishaji ovyo wa bei za mafuta! Kama alivyosema Chaka, shame on you EWURA.
 
Back
Top Bottom