Lusungo,
Aliyeleta suala la Dr. Mwanjisi si mimi.
Soma post ya nyuma utaona hilo.
Mimi nimemjibu kuwa hapana haja ya kueleza habri zake.
Nahisi na wewe unakijua kisa cha huyu mzalendo.
Ndiyo nini hicho? nilichokuwekea nyekundu.
Hebu fata hicho ulichokinukuu uone kamjibu nani na kaulizwa nini. Wacha kudandia treni kwa mbele, utaumia.
Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
kwa jinsi ninavyo fahamu dharau za mohamed said,mabandiko yanayo anzishwa na members wengine kwa lengo la kumkosoa,huwa hashiriki hata kama ID yake umekuwa tagged in,lakni hili la prof hirji yeye mwenyewe kaelekea kibra.yupo active ku refute kila post.hakika safari hii kashikwa pabaya.
Inashangaza si kidogo.
Tukiwaomba waje na historia waijuwayo wao nasi tufaidike na elimu yao hawaji nayo, mara wanakuomba kujuwa kuhusu fulani na hiki na kile tena kwa kejeli na tashtiti za hapa na pale, ingawa hawana walijualo.
Nnakumbuka walisema siku za nyuma wataunda kikundi chao hao wajiitao Yericko Nyerere, Mzee Mwanakijiji, Nguruvi3, Mag3 na wengineo ili waje na historia kupinga historia uliyoiandika wewe. Chakushangaza! naona mpaka leo umoja huo haujaja na chochote, sana sana niliona wakati fulani ajiitae Mzee Mwanakijiji akiokotea yale yale yako (plagiarism) na kuyatoa kwenye gazeti kama vile ni yake. Nikaona tena ajiitae Yericko Nyerere akiokotea yale yale yako (plagiarism) akileta humu humu JF kama vile yake.
Leo pumba za Professor Hirji walionakama zimehuisha uhai wao lakini afanaalek, Mau Mau kapiganana Mjerumani? data za kufikirika na kupika (kakiri mwenyewe, wala si yangu hayo). Kuwaonesha hayo mawili tu, hawana cha kujibu, mara oooh picha, mara oooh matusi. Wakaulizwa kifungo cha "report abuse" hawakioni? Kimyaaaaaaa.
Sasa wanataka kujuwa kuhusu Dr. Mwanjisi.
Nilisema humu, paper ya Hirji ni knocked out na sasa tutaendeleza mnakasha kwa faida ya wengi wetu kupata darsa, lakini si kwa kumjibu Hirji, hivi mtu ukae unajibu "hypothetically...data..." (data za kufikirika)?
Tupe darsa Al Alama Mohamed Said, hao wanaosema ngano ndiyo wanajazana humu kuchota ilmu, lakini kwa uhasid wao tu, hawataki kukubali, unafikiri wangekuwa hawafaidiki wangejazana humu?
Baniani mbaya kiatu chake dawa.
Wanasikitisha sana.
Si imeeleweka shida yako nini?
Ritz, naona ama umenogewa na ngano za Mohamed Said hadi zinaanza kutia kichefu chefu au wewe ni moja katika wanaomeza simulizi za barazani bila kuhoji. Kwako hadithi haina tofauti na ukweli.Pata darsa kiduchu hapa chini.
Huu ni uongo ambao kama tu ungekuwa na kumbukumbu kidogo hungethubutu kuuandika humu JF kwani uliwahi kuletwa awali lakini ikagundulika ni simulizi tu kama za mgahawani. Mwalimu alikuwa ni Kiongozi wa TAA mkoani Tabora miaka mingi tu kabla ya huo mwaka 1952.Mwalimu Nyerere alipofika Dar es Salaam kwa mara ya kwanza mwaka wa 1952 kama mwalimu wa shule ya St. Francis' College, Pugu hakuna mtu aliyekuwa anamjua au kupata kusikia habari zake katika ulingo wa siasa.
Kama kuna mtu Dar es Salaam alikuwa hamjui Mwalimu, basi huyo mtu hakujua harakati zozote zilizokuwa zikifanyika nchini Tanganyika nje ya Dar es Salaam. Katika mkutano wa kitaifa uliofanyika kabla jimboni Tabora uliohudhuriwa na viongozi wa kitaifa wa TAA Mwalimu alikutana na wawakilishi kutoka sehemu mbali mbali nchini na Dar akiwamo Dossa Aziz na wengineo. Abdulwahid Sykes wakati huo labda alikuwa akijulikana tu kama mtoto wa baba, Klyst Sykes, na hakuwa na wadhifa wowote ndani ya TAA.Kassela Bantu ambaye alikuwa akijuana na Nyerere kwa siku nyingi alimchukua Nyerere kwa Abdulwahid Sykes kumtambulisha.
Hii ilikuwa baada ya mapinduzi ya vijana kuutwaa uongozi wa TAA na Dr. Vedasto Kyaruzi kuchaguliwa kuwa Raisi wake wa kwanza na Abdulwahid Sykes katibu. Abdulwahid Sykes hakuwahi kuchaguliwa hata mara moja kuwa Raisi wa TAA, alikuja kukaimu tu kwa muda hiyo nafasi baada ya Raisi wake, Dr. Kyaruzi kuhamishiwa mikoani na wakoloni.Wakati ule Abdulwahid alikuwa Rais wa TAA.
Ni wajumbe na viongozi wa TAA Dar es Salaam waliomuomba Mwalimu kujiunga na baraza hilo kwa sababu hakuwepo mtu aliyekuwa na ujasiri, elimu, uwezo na sifa ambaye angeweza kuiongoza TAA katika mabadiliko ya kuigeuza chama cha siasa.Nyerere mara moja akajiunga na baraza la siasa lililokuwa likifanyika Mtaa wa Mbaruku nyumbani kwa Dossa.
Mwalimu alikuwa akifuatwa huko Pugu na kuna baadhi ya mikutano iliyofanyika huko huko wakimshawishi akubali kuwa kiongozi wao.Ikawa kila Jumapili Nyerere anakuja kutoka Pugu kuja kumtembelea Dossa.
Hapana, wanasiasa wengi alishakutana nao kabla ya kwenda masomoni Uingereza, Dossa Aziz akiwa mojawao. Labda useme alikutana na viongozi wakazi wa mji ambao hawakuwahi kutoka nje ya Dar es Salaam kwa sababu mbali mbali; hapo itaeleweka.Ilikuwa katika baraza hii ndipo Nyerere alipokutana na wanasiasa wengi wa wakati ule kama Ramadhani Mashado Plantan aliyekuwa anamiliki gazeti lililokuwa likijulikana kama Zuhra, John Rupia, Dunstan Omari, Zuberi Mtemvu na wanasiasa wengine.
Mwalimu alileta changamoto na fikra mpya ndani ya TAA na hapo ndipo sauti za kudai uhuru zikaanza kusikika kupitia magazeti kama Zuhura na kadhalika.Fikra za Nyerere za kudai uhuru zilisikika kwa mara ya kwanza kupitia kalamu ya Mashado Plantan na gazeti lake la Zuhra lililokuwa likitoka kila siku ya Ijumaa.
Miezi sita tu toka ajiunge na TAA Dar es Salaam alichaguliwa kuwa kiongozi wake mkuu akimbwaga Abdulwahid Sykes aliyekuwa akikaimu nafasi hiyo naye kujitosa kugombea.Fikra za Nyerere ziliingiza msisimko mpya katika baraza lile na haukuchukua muda mwaka 1953 uongozi wa ndani ukampendekeza agombee urais wa TAA.
Labda wengine wameelewa, mimi sijaelewa ndiyo maana nikauliza ningekuwa nimeelewa nisingeuliza.
FF,
Nina umri karibia miaka 10 hivi.
Niko Kinondoni kwa bibi yangu Mwantum biti Rajab Mwinyimgeni.
Allah amrehemu.
Ni usiku tumetandika mkeka nje ya kibanda chake cha "full suit."
Wajukuu tuko pale anatuhadithia khabari za Hayati Bwana siku za likizo
shule zimefungwa wakati wa kwenda kwa bibi kula pepeta na
bwimbwi.
Huyu ni babu yangu Sheikh Mohamed Mvamila.
Bibi yangu anampamba marehemu mumewe anasema,"Basi Hayati Bwana
kashika kitabu anasomesha na watu wamemzunguka wanamsikiliza... tumehama
Mkamba tumekwenda Musoma huko kaanzisha zawia babu yenu anasomesha huko..."
Hii ilikuwa baada ya Vita Kuu ya Kwanza.
Nikisikia maneno yale mwili ulikuwa ukinisisimka kwani huyu ni babu yangu
Maalim Mohamed Mvamila anasifiwa kwa ilm...na mimi nimepewa jina lake.
Ahsante dada yangu FF umenipeleka mbali sana.
Mwenyezi Mungu awakunjulie makaburi yao wazee wetu walituwekea misingi
ya kuupenda Uislam na ayajaze nuru.
Ritz, naona ama umenogewa na ngano za Mohamed Said hadi zinaanza kutia kichefu chefu au wewe ni moja katika wanaomeza simulizi za barazani bila kuhoji. Kwako hadithi haina tofauti na ukweli.
Huu ni uongo ambao kama tu ungekuwa na kumbukumbu kidogo hungethubutu kuuandika humu JF kwani uliwahi kuletwa awali lakini ikagundulika ni simulizi tu kama za mgahawani. Mwalimu alikuwa ni Kiongozi wa TAA mkoani Tabora miaka mingi tu kabla ya huo mwaka 1952.
Kama kuna mtu Dar es Salaam alikuwa hamjui Mwalimu, basi huyo mtu hakujua harakati zozote zilizokuwa zikifanyika nchini Tanganyika nje ya Dar es Salaam. Katika mkutano wa kitaifa uliofanyika kabla jimboni Tabora uliohudhuriwa na viongozi wa kitaifa wa TAA Mwalimu alikutana na wawakilishi kutoka sehemu mbali mbali nchini na Dar akiwamo Dossa Aziz na wengineo. Abdulwahid Sykes wakati huo labda alikuwa akijulikana tu kama mtoto wa baba, Klyst Sykes, na hakuwa na wadhifa wowote ndani ya TAA.
Hii ilikuwa baada ya mapinduzi ya vijana kuutwaa uongozi wa TAA na Dr. Vedasto Kyaruzi kuchaguliwa kuwa Raisi wake wa kwanza na Abdulwahid Sykes katibu. Abdulwahid Sykes hakuwahi kuchaguliwa hata mara moja kuwa Raisi wa TAA, alikuja kukaimu tu kwa muda hiyo nafasi baada ya Raisi wake, Dr. Kyaruzi kuhamishiwa mikoani na wakoloni.
Ni wajumbe na viongozi wa TAA Dar es Salaam waliomuomba Mwalimu kujiunga na baraza hilo kwa sababu hakuwepo mtu aliyekuwa na ujasiri, elimu, uwezo na sifa ambaye angeweza kuiongoza TAA katika mabadiliko ya kuigeuza chama cha siasa.
Mwalimu alikuwa akifuatwa huko Pugu na kuna baadhi ya mikutano iliyofanyika huko huko wakimshawishi akubali kuwa kiongozi wao.
Hapana, wanasiasa wengi alishakutana nao kabla ya kwenda masomoni Uingereza, Dossa Aziz akiwa mojawao. Labda useme alikutana na viongozi wakazi wa mji ambao hawakuwahi kutoka nje ya Dar es Salaam kwa sababu mbali mbali; hapo itaeleweka.
Mwalimu alileta changamoto na fikra mpya ndani ya TAA na hapo ndipo sauti za kudai uhuru zikaanza kusikika kupitia magazeti kama Zuhura na kadhalika.
Miezi sita tu toka ajiunge na TAA Dar es Salaam alichaguliwa kuwa kiongozi wake mkuu akimbwaga Abdulwahid Sykes aliyekuwa akikaimu nafasi hiyo naye kujitosa kugombea.
Ritz, unapoambiwa jambo na wewe jipe fikra kidogo siyo unameza tu, hebu jiulize; huyu mtu ambaye hakuna aliyemfahamu anasafiri hadi Dar, anasema katoka Pugu, anakuta watu wamejipanga wanakiendesha TAA wakiwa na mipango lukuki, anatambulishwa na mtu moja na baada ya muda mfupi wanamkabidhi chama chao cha TAA walichokianzisha akiongoze! Ningekuwa wewe ningejiuliza, je hii iliwezekanaje?
Lusongo,Mkuu sio kwa hoja hiyo tu laa....
Muda mrefu Sana umekuwa ukijaribu kuchimbua haya mambo kwa undani na kujaribu kuifuta historia adhimu ya Nyerere ktk ukombozi Wa nchi hii dhumuni ni nini?
Unaamsha Sana hisia za udini kitu ambacho kwa MTU aliyestaarabika si vizuri kupigia upatu.
Unajua huyu muhindi Prof F Hirji, ni mfia Nyerere miaka yote anajulika ni shemeji yake na Prof Shivji wote hawa na wenzake ndiyo wale kigoda cha Mwalimu Nyerere.
Hawa ndiyo walikuwa wanashangilia historia ya Kivukoni iliyoanzia kwenye Nyerere na kuishia kwa Nyerere.
Hawa kina Hirji na jamaa zao kina Hassan Hirji wametajirika wakati wa Nyerere walikuwa karibu mno na serikali ya Nyerere unategemea wamseme vibaya Nyerere.
Mimi namjua huyu Hirji mfia Nyerere toka miaka ya 1980 alikuwepo pale NIT Mabibo na wafia Nyerere wenzake kina Mwaipopo, Kaimukilwa, Dr. Chijumba, na wakomunisti wengine.
Naona umejongea tartibu kwenye darsa kufyonza ilm.kwa jinsi ninavyo fahamu dharau za mohamed said,mabandiko yanayo anzishwa na members wengine kwa lengo la kumkosoa,huwa hashiriki hata kama ID yake umekuwa tagged in,lakni hili la prof hirji yeye mwenyewe kaelekea kibra.yupo active ku refute kila post.hakika safari hii kashikwa pabaya.
Kama hukuelewa uliweza vipi tambua nilichomjibu mpaka ukasaidia kumjibia kuwa alikua akijibu hoja?
Ulijuaje nadandia treni kwa mbele ikiwa hukuelewa?
Matumbo,
Unakusudia "muasisi" umeandika "muhasisi."
Hayo unayosema ndiyo ulikuwa msimamo wa miaka mingi hadi nilipoandika
kitabu cha Abdul Sykes.
Iwe itakavyokuwa hakuna sababu ya mimi na wewe tukabishana kuhusu hili.
Ukweli sasa uko wazi watu wamesoma kitabu changu na wana uhuru wa kuamini
kile wanachoona kina ukweli.
Mimi nakuomba kitu kimoja tu.
Andika kwa adabu.
Naona staha kidogo inakutoka umehamaki na kuita TAA "kijiwe."
Hapana AA (1929) na TAA na vyama vingine walivyoanzisha wazee wetu
kama Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (1933), TANU (1954) na Tanganyika
Railway African Union (1955) (TRAU) havikupata kuwa "kijiwe.''
Babu yangu Salum Abdallah ndiye alikuwa rais muasisi wa TRAU katibu akiwa
Kassanga Tumbo.
Uongozi wa TANU wa mwanzo pamoja na wanachama wake walitoka Al Jamiatul
Islamiyya.
TRAU ilipigana bega kwa bega na TANU dhidi ya Waingereza.
Yako mengi lakini na tuishie hapa.
average minds discuss events,small minds discuss people....nakushauri tu ubaki kuwa muimba mapambio ya kumshabikia mohamed said.
Mzee Mohammed niwie radhi kwa kuiita TAA kijiwe cha soga, nilikosa neno mbadala nikidhamiria 'social club'.
Lakini yote hiyo haiondoi ukweli kwamba TANU muasisi wake ni Mwl Nyerere aliyeibadilisha TAA kuwa chama cha siasa TANU, mpaka akatuletea uhuru.
Nafikiri sasa ni wakati wa kujibu hoja za Prof maana tumekuwa na subira lakini umeonekana ukikwepa au kama imeshindikana au umekosa majibu unakuwa muungwana tu ili si jambo la mashindano.
Naona vijana wako nao wameamua kurusha matusi na maneno ya kibaguzi mpaka kumuita Prof 'mshia' na kutuita wengine 'mapagani' waonye haya si maneno ya watu wenye adabu naimani ata watu wa umri wako walishayaacha pale Maggoti.
Naomba nisaidie hili swali langu dogo; Mau Mau walipigana na Wajerumani?
Lusongo,
Kuchimbua kwa undani ni kweli.
Kitabu changu kimebadili kabisa historia ya uhuru wa Tanganyika.
Kuifuta historia ya Nyerere hilo haliwezekani kabisa.
Huwezi kufuta historia ni kazi kubwa sana.
Hili nalijua kwa kuwa nina uzoefunalo.
Historia ya wazee wangu ilifutwa kwa takriban nusu karne.
Leo tuko hapa tunaizungumza.
Ikiwa unaona kuwa kwa mimi kuandika habari za wazee wangu naamsha hisia
za udini hiyo ni bahati mbaya sana kwako.
Siwezi kuacha kuwarehemu wazee wangu.
Nikiacha historia hiyo mimi nitabakia na nini katika nchi hii?
Nitakuwa muflis.
average minds discuss events,small minds discuss people....nakushauri tu ubaki kuwa muimba mapambio ya kumshabikia mohamed said.
Ritz, naona ama umenogewa na ngano za Mohamed Said hadi zinaanza kutia kichefu chefu au wewe ni moja katika wanaomeza simulizi za barazani bila kuhoji. Kwako hadithi haina tofauti na ukweli.
Huu ni uongo ambao kama tu ungekuwa na kumbukumbu kidogo hungethubutu kuuandika humu JF kwani uliwahi kuletwa awali lakini ikagundulika ni simulizi tu kama za mgahawani. Mwalimu alikuwa ni Kiongozi wa TAA mkoani Tabora miaka mingi tu kabla ya huo mwaka 1952.
Kama kuna mtu Dar es Salaam alikuwa hamjui Mwalimu, basi huyo mtu hakujua harakati zozote zilizokuwa zikifanyika nchini Tanganyika nje ya Dar es Salaam. Katika mkutano wa kitaifa uliofanyika kabla jimboni Tabora uliohudhuriwa na viongozi wa kitaifa wa TAA Mwalimu alikutana na wawakilishi kutoka sehemu mbali mbali nchini na Dar akiwamo Dossa Aziz na wengineo. Abdulwahid Sykes wakati huo labda alikuwa akijulikana tu kama mtoto wa baba, Klyst Sykes, na hakuwa na wadhifa wowote ndani ya TAA.
Hii ilikuwa baada ya mapinduzi ya vijana kuutwaa uongozi wa TAA na Dr. Vedasto Kyaruzi kuchaguliwa kuwa Raisi wake wa kwanza na Abdulwahid Sykes katibu. Abdulwahid Sykes hakuwahi kuchaguliwa hata mara moja kuwa Raisi wa TAA, alikuja kukaimu tu kwa muda hiyo nafasi baada ya Raisi wake, Dr. Kyaruzi kuhamishiwa mikoani na wakoloni.
Ni wajumbe na viongozi wa TAA Dar es Salaam waliomuomba Mwalimu kujiunga na baraza hilo kwa sababu hakuwepo mtu aliyekuwa na ujasiri, elimu, uwezo na sifa ambaye angeweza kuiongoza TAA katika mabadiliko ya kuigeuza chama cha siasa.
Mwalimu alikuwa akifuatwa huko Pugu na kuna baadhi ya mikutano iliyofanyika huko huko wakimshawishi akubali kuwa kiongozi wao.
Hapana, wanasiasa wengi alishakutana nao kabla ya kwenda masomoni Uingereza, Dossa Aziz akiwa mojawao. Labda useme alikutana na viongozi wakazi wa mji ambao hawakuwahi kutoka nje ya Dar es Salaam kwa sababu mbali mbali; hapo itaeleweka.
Mwalimu alileta changamoto na fikra mpya ndani ya TAA na hapo ndipo sauti za kudai uhuru zikaanza kusikika kupitia magazeti kama Zuhura na kadhalika.
Miezi sita tu toka ajiunge na TAA Dar es Salaam alichaguliwa kuwa kiongozi wake mkuu akimbwaga Abdulwahid Sykes aliyekuwa akikaimu nafasi hiyo naye kujitosa kugombea.
Ritz, unapoambiwa jambo na wewe jipe fikra kidogo siyo unameza tu, hebu jiulize; huyu mtu ambaye hakuna aliyemfahamu anasafiri hadi Dar, anasema katoka Pugu, anakuta watu wamejipanga wanakiendesha TAA wakiwa na mipango lukuki, anatambulishwa na mtu moja na baada ya muda mfupi wanamkabidhi chama chao cha TAA walichokianzisha akiongoze! Ningekuwa wewe ningejiuliza, je hii iliwezekanaje?