katika wote Walter ndiye wa ukweli kuliko hata sifa anazobebeshwa Wababa. Walter anaimba ametulia na hata uchaguzi wa nyimbo zake ni kiboko lakini mtindo wa kupanga matokeo unawafanya wampigie upatu Wababa zaidi na ni katika mtindo huo huo Norman aliondolewa.
Pili Husna kaondoka lakini nakwambia alikuwa mzuri kuliko Nsami aliyeimba kizembe wimbo wa kuboa sana na matumizi yake ya steji ni zero. Husna pia alimpiga fimbo Salma (kipenzi chao anayeandaliwa kuchukuwa hiyo 50M). Ni kweli kabisa kuwa Huyu Salma ni mbovu hata Salama leo kamkataa. Ni binti anashindwa hata kutamka maneno yanavyotakiwa ana'kithembe' na anaimbia puani. Kila siku anajificha nyuma ya gitaa. Yaani akiambwia kuimba live hata top 20 hakustahili kabisa! Hamna noma mchagueni tu huyo binti wenu wa EPIC ili mgawane naye hizo 50.