BBC Swahili ya enzi hizo!

BBC Swahili ya enzi hizo!

Acha ujuha wewe

Tatizo umezaliwa 2000s
Kuna jamaa alikuja na uzi humu akidai kasumba ya kusema eti, "kitu fulani ilikuwa zamani bwana"
ni ujuha.
Utasikia, ndoa zamani bwana,
Mara usikie, wanawake zamani bwana.
Na wewe umekuja unasema vile vile, eti BBC ilikuwa zamani,
kwahiyo ya sasa hivi imekuwa Baba yako au!
 
BBC swahili wamezidi utoto kwenye kipindi
 
Kuna yule mama ana sauti nzito kama ya kiume.... alitoka IPP akaenda BBC. Alikuwa anasoma taarifa ya habari siku za jumamosi mechi ikiwa inatangazwa.
Yule alikuwa DW Bana siyo BBC UMMY HERI MPKA LEO YUPO
 
Toka Mkenya alipopewa ukuu wa idhaa ndio ukawa mwanzo wa kuiharibu Radio yetu pendwa. Siku hizi inatia kichefuchefu kabsa. Wamejaa wajaluo hata Kiswahili hawajui. Wamelazimisha makao makuu iwe Nairobi wakati utafiti wao wenyewe BBC unaonyesha wasikilizaji wengi wapo TZ.
kweli mkuu inaboa sana aisee na vile vimijadala vyao havieleweki kbs....
 
Inanikumbusha kila nikiamka kwenda shule nafungulia redio kwanza,12:30 kipindi kikisha ndo naenda shule.

Asubuhi imefika, jua linaanza kuchomooza, amkeni kumekucha aah aah amka na bbc.
 
Kigara eee! Amka na BBC, Kinshasha eeh! Amka na BBC kwa masafa mafupi na ....

BBC ya enzi hizo asikwambie mtu.Ilisheheni manguli wa habari. Lubunga Byaombe (DRC) Tido Mhando, Suzan Mongi, Mariam Omary, Aisha Yahaya, Chama Omary Matata, Greipo Mbea (Mtaalamu wa mashairi), Iddy Seif, Zuena Seif, Suluma Kasimu, Ali Salehe, Ali Mutasa (Mtaalamu wa uchumi), Abdalah Majura,( Michezo). Baadae wakaja akina Hasan Mhelela, Salim Kikeke, Charles Hilal. I surely miss those ancient beautiful days.
Manase Lukungu.
 
Kigara eee! Amka na BBC, Kinshasha eeh! Amka na BBC kwa masafa mafupi na ....

BBC ya enzi hizo asikwambie mtu.Ilisheheni manguli wa habari. Lubunga Byaombe (DRC) Tido Mhando, Suzan Mongi, Mariam Omary, Aisha Yahaya, Chama Omary Matata, Greipo Mbea (Mtaalamu wa mashairi), Iddy Seif, Zuena Seif, Suluma Kasimu, Ali Salehe, Ali Mutasa (Mtaalamu wa uchumi), Abdalah Majura,( Michezo). Baadae wakaja akina Hasan Mhelela, Salim Kikeke, Charles Hilal. I surely miss those ancient beautiful days.
vip sasa hivi
 
Saivi BBC wamechukua kifaa kipya kutoka DW, Caro Robi. Ana bahati sana kuunganisha radio mbili mfululizo. Ni mkenya ila namkubali sana.
 
Lubunga Byaombe sijui yuko wapi yule jamaa. Nilikuwa nasikiliza sana BBC Swahili kuanzia 2007..Tumbo risasi.
Byaombe Mara ya mwisho nilisikia ni mwandishi wa rais mstaafu wa DRC-Kabila Joseph
 
Back
Top Bottom