Bayport ya Ngara ni wezi

Bayport ya Ngara ni wezi

Jaslaws

JF-Expert Member
Joined
May 31, 2011
Posts
6,016
Reaction score
5,301
Naona kama nikiendelea kukaa kimya ntakuwa sitimizi wajibu wangu kama mwananchi.

Pale Bayport Ngara kuna vijana wameajiliwa pale wanawachezea wananchi mchezo mbaya sana, wao wanacho kifanya ni mtu akienda kukopa wanakuandikia mkataba lakini sehemu ya hela unayokopa hawajazi kiwango.

Sasa wanachokifanya kwa mfano mtu kakopa millioni mbili, wao wanaandika millioni tano, ile pesa millioni tano ikiwa released watachukua zile milion zako mbili watakupatia na kiwango kilichobaki wanagawana wao.

Kwenye makato utaendelea kukatwa mpaka hiyo million tano itakapo kwisha.

Hii nimeishuhudia live na kuna case mahakamani ya namna hiyo.

Kwenye mahakama ya Wilaya, hao vijana wanatumia advantage ya umasikini wa wananchi na elimu ndogo kuwaibia hawa vijana hawwapi mkataba ama kopi ya mikataba baada ya makubaliano.

Hii inafanywa kwa lengo ili hata ukienda kudai mahakamani hautakuwa na kidhibiti kwenye madai yako.(as far as breach of contract is concerned)

Maombi yangu ni kwa uongozi wa juu wa bayport waingilie kati, wawasaidie hawa wananchi wananyanyasika sana, vipato vyao vyenyewe ni vidogo sana inapotokea mtu akawanyang'anya na hicho kidogo inakuwa sio.
 
Hii taasisi sasa imekua janga la kitaifa!! kila kona ya nchi ni wao na kesi zote ni za kuwatapeli na kuwabambikia riba za kutisha!! mshukuru mpo kwenye nchi yenye mapungufu makubwa ya utawala bora! mlitakiwa mfilisiwe kitambo sana.
 
Taasisi zote zina reporting lines....kulalamika mtandaoni bila ya kutafuta high levels za iyo organization haivutii sana. Hata ivo poleni!!
 
Taasisi zote zina reporting lines....kulalamika mtandaoni bila ya kutafuta high levels za iyo organization haivutii sana. Hata ivo poleni!!
Mkuu mimi sio muhanga wa haya matukio ila najaribu tu kuwasemea wanyonge..kumbuka pia uku kwenye mitandao wanapita watu wa aina tofauti..
 
Hao wanaoenda kukopa wapewe elimu. Wewe utasainije karatasi ya pesa ambayo haijaanfikwa kuwa umechukua kiasi gani?
Waache waibiwe tu. Mambo mengine ni uzembe wao.
 
yaani nilijua ni hii wilaya yangu ya kahama tu kumbe ni kila eneo!!serikali iko wapi kwa hawa wezi au kisa ni ya first lady???
 
Mimi Bayport niliistukia 2006 wKIW Raha towers. Nikafikiri wamefunga hii biashara ya wizi, kumbe mpaka leo bado wanaliza watu ?

Ushauri wangu mdogo tu. USIKOPE BAYPORT UTALIA MACHOZI YA DAMU.
 
Back
Top Bottom