Huwezi kujua kwamba unabaguliwa kama nawe siyo mbaguzi.
Tofauti na unavyosema. Anayebaguliwa ndie anae jua kuwa anabaguliwa pamoja na machungu yake. Mbaguzi anaona kila kitu kiko sawa.
Watu wanaanzisha movement baadae wanaikana wenyewe ati walikuwa wanatikisa kiberiti?
Nyerere aliwahi kusema kuwa ataondoka CCM kama akiona kuwa inaenda kusiko. Alisema CCM sio mama yake. Hicho ndicho G-55 walichofanya. Hawajatikisa kiberiti, wamefanya kweli. Ni kazi ya waliobaki kuwathibitishia kuwathibitishia kwa vitendo kuwa walikosea kuondoka Chadema.
Ni upotoshaji kusema kuwa kuenguliwa kwao katika nafasi za uongozi ndio sababu ya baadhi ya G-55 kuondoka Chadema. Sababu walitoa ni:
1. Maoni yao kuto sikilizwa. Ingawa wenye chama wanaaema waliitwa kwenye mkutano wa watia nia ili wakatoe duku duku zao lakini mwenye akili aliona kuwa mualiko huo ulikuwa na nia ya kuwazodoa na sio kuwasikiliza. Wakati wa mkutano waliohudhuria walitakiwa kunyoosha mikono kama hawaungi mkono NRNE. Bwana mmoja alinyoosha mikono lakini reception aliyopata ilibidi aseme hakuelewa swali. Haya sio mazingira ya mjadala wa haki na uwazi.
2. Hamna mkakati wa kutekeleza NE. Kila wakiiliza walikuwa wanapigwa chenga.
3. Waliona mkakati wa kususia uchaguzi hautafanikiwa pamoja na kuwa utawanyima wanachama wa Chadema haki yao ya kikatiba ya kupiga na kupigiwa kura.
4. Matusi na lugha za kejeli dhidi yao.
5. Kutengwa na wenzao.
Nadhani haujui historia ya Nyerere na TANU. Nyerere aliacha kazi ili ajilite zaidi kwenye shughuli za chama. Kama vile alivyojiuzuru kwenye nafasi ya uongozi wa serikali ili akijenge chama chake.
Amandla...