BAVICHA yatangaza bingo kubuni nembo

BAVICHA yatangaza bingo kubuni nembo

Wala msihangaike. Mpeni Deus Malya, atawatengenezea nembo nzuri sana.
 
Hongera BAVICHA.Vijana wabunifu na wachoraji laki5 hizo siyo zakulazia damu onyesheni ujuzi wenu
 
BARAZA la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA) linafanya mchakato wa kutafuta nembo yake ambayo itakuwa kielelezo cha vijana ndani ya chama hicho.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Katibu Mkuu wa BAVICHA, Deogratias Munishi, ilieleza kuwa nembo hiyo itakuwa alama ya utambulisho na inatarajiwa kutumika katika shughuli na mambo mbalimbali ya vijana ndani wa chama hicho.

Munishi aliwataka vijana wa CHADEMA na wapenda mabadiliko kubuni nembo kwa ajili ya alama ya baraza hilo.
“Ili kutoa fursa kwa vijana wabunifu kutumia vipaji vyao kutoa mchango wao kwa chama na baraza lao, tumeandaa shindano maalumu la ubunifu wa nembo na atakayeshinda atazawadiwa,” alisema.
Munishi alisema wale wote wenye kipaji cha ubunifu na wangependa kushiriki shindano hilo, watapaswa kuzingatia vigezo muhimu ambavyo ni pamoja na rangi kuu za CHADEMA.
Alisema watakaokamilisha kazi zao, waziwasilishe makao makuu ya chama hicho yaliyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam kabla ya Machi 26.

Munishi alisema baada ya wadau mbalimbali kuwasilisha nembo walizozibuni, sekretaiati ya BAVICHA itazichambua na hatimaye kupata tatu bora ambazo zitawekewa utaratibu wa kushindanishwa kwa kuingizwa kwenye vyombo vya kimaamuzi, ili kupata nembo moja.
Alisema atakayeshinda atapatiwa sh 500,000 kama zawadi na cheti maalumu cha kutambua mchango wake kwa BAVICHA.

source:Tanzania Daima

mbona ni rahisi tuu waweke picha ya fisi akila mzoga chini ya mzoga waandike bavicha
 
good move although the reward is not that much attractive .... they need to add more motivation e.g award of computer and or automatic qualification to a winner to do all BAVICHA designing contracts

Nafikiri recognition ya kushinda design ya taasisi mashuhuri kama ya CHADEMA ni zaidi ya kupata fedha, it will give you an enormous publicity! Kwahiyo wasishindanie fedha, washindanie kutambuliwa! Vijana designers wako wengi na wengine huwa wanafanya bure kwa mapenzi yao kwa chama tu!
 
Nafikiri recognition ya kushinda design ya taasisi mashuhuri kama ya CHADEMA ni zaidi ya kupata fedha, it will give you an enormous publicity! Kwahiyo wasishindanie fedha, washindanie kutambuliwa! Vijana designers wako wengi na wengine huwa wanafanya bure kwa mapenzi yao kwa chama tu!

Umenena vema sana.
 
mbona ni rahisi tuu waweke picha ya fisi akila mzoga chini ya mzoga waandike bavicha

product za mlugo hizi FFFFFFF mpaka uso wako ni Fffff Meno yako Fffff,ila sio makosa yako nitaendelea kuilaani ccm ndio inafyetua mitambo sambo yako
 
Nafikiri recognition ya kushinda design ya taasisi mashuhuri kama ya CHADEMA ni zaidi ya kupata fedha, it will give you an enormous publicity! Kwahiyo wasishindanie fedha, washindanie kutambuliwa! Vijana designers wako wengi na wengine huwa wanafanya bure kwa mapenzi yao kwa chama tu!

Naungana na wewe. Hapa suala si pesa, suala ni kujenga heshima ya kutoa mchango wa ujenzi wa taasisi kubwa ya vijana kama BAVICHA. Kutambulika ndio jambo muhimu na BAVICHA wameamua kuwapa fursa vijana wao ili watumie ujuzi wao na ujulikane. Wangeweza kwenda hata china kutafuta hiyo nembo lakini ni watu wanaojali vipaji miongoni mwao na miongoni mwa Watanzania. Bravooo BAVICHA
 
Naungana na wewe. Hapa suala si pesa, suala ni kujenga heshima ya kutoa mchango wa ujenzi wa taasisi kubwa ya vijana kama BAVICHA. Kutambulika ndio jambo muhimu na BAVICHA wameamua kuwapa fursa vijana wao ili watumie ujuzi wao na ujulikane. Wangeweza kwenda hata china kutafuta hiyo nembo lakini ni watu wanaojali vipaji miongoni mwao na miongoni mwa Watanzania. Bravooo BAVICHA

You are correct!
 
good move although the reward is not that much attractive .... they need to add more motivation e.g award of computer and or automatic qualification to a winner to do all BAVICHA designing contracts

The great motivation here is that sense of belonging and Recognition by this distinguished institution brother! Apart from that, this will be a call for business.
 
Mimi nshatuma ubunifu wangu BAVICHA. Naamini nitashinda. Sijui wengine wenye vipaji vipi wajameni!
 
Aliyekupa wewe ndo kawanyima wenzio,hiyo kwako ni ndogo sana ila kuna wanaosotea elfu 1 tu wanaikosa,omba sana uendelee kuchezea hela la sivo mabo yakiwa kinyume nakuonea huruma lazima ulie
Dau la laki tano ndogo sana.
 
Back
Top Bottom