Preta
JF-Expert Member
- Nov 28, 2009
- 24,323
- 18,793
ZAKARIA EXPRESS basi linalotoka jijini Mza kwenda Musoma limegonga daladala ndogo aina ya NOAH na kuua watu wanane hapohapo. Majeruhi wengine hali zao ni mbaya na wamekimbizwa hospt kwa matibabu zaidi. PETER ZAKARIA ni mmiliki wa mabasi hayo. tar 20 . 2 . 2012 nilipanda basi la zakaria (bahati mbaya tiketi haijaandikwa na. za gari) ila ina VAT NO 18-004785-H, nilikua natokea musoma kwenda mza, lilikua likikimbia kwa mwendo wa kasi sana huku likiwa linayumba. Tulipofika mbele ya Ramadi kwenye break point ya polisi walianza kushusha magunia 8 niliyoyadadisi ilikua ni MIRUNGI, polisi waliyapokea na kumkabidhi pesa dereva. Nilipojaribu kuuliza nikaambiwa haya mabasi huvunja sheria za barabara na polisi wa usalama hawana ubabe wa kuyazuia. PETER ZAKARIA ni mfanyabiashara maarufu wa magendo ukanda wa ziwa. Ni mweusi, mnene wa wastani. Anasifika kwa ubabe kwani alishamwagia tindikali dereva wa Bunda basi, alishamtishia bastola padri kwenye mazishi kwa mahubiri yaliyomgusa, bingwa wa kuuza mafuta ya magendo kutoka kenya, inasemekana huteka meli za mafuta kutoka Kisumu kenya. Kuanzia RPC, RPO na TRA mkoa wa mwanza na Mara mwisho wa mwezi hupelekewa bahasha kuwapooza. Ni kada na mfadhili wa CHAMA CHA MAPINDUZI! swahiba wake mkuu ni Mwita Gachuma mjumbe wa NEC taifa. Inasemekana pia ana jeshi lake binafsi na selo za kuwaadhibu maadui zake! Naomba jeshi la polisi nchini kuingilia kati na kudhibiti vyombo vyake vya usafiri.
nasikia alishawahi kuingiza basi zima la watu 60 kwenye yard ya ofisini kwake na kuwacharaza viboko......bahati mbaya kulikuwa na ofisa fulanifulani kati ya abiria......kidogo ilimcost....