Basi la Dar Express lapata ajali Wami

Basi la Dar Express lapata ajali Wami

Tatizo ni hizi mahakama zetu dereva ameua analipishwa faini tu ingetakiwa kifungo miaka 20 tuone kma wataendesha kizembe
 
Jk piga chini mkuu wa usalama barabarani nchini.

Pia badilisha matrafic wote barabarani waje wapya hawa waende kuwa askari magereza- make ni rushwa tu ndio kazi yao.
 
"Ajali mbaya"

Mhh. Hizi shule za kufundishwa na waalimu waliofeli masomo yao ni janga.
Poleni ndugu zetu, asipoteze uhai hata mmoja, majeraha yenu yatibiwe na kupona haraka, mliopata mshituko pateni ufahamu kuwarejea kwenye viwango vyake.
 
tunaomba sheria ya mtandao ianze kazi haraka uongo mwingine hauvumiliki.
 
Hizo habari sio za kweli hakuna basi la dar express lililopata ajali siku ya leo..... Acheni kupost vitu km hivyo sio sifa au ndio nyie msiolitakia taifa hili mema
 
Tatizo ni hizi mahakama zetu dereva ameua analipishwa faini tu ingetakiwa kifungo miaka 20 tuone kma wataendesha kizembe
Tatizo si mahakama. Ni watunga sheria ambao ni bunge badala ya kuzitunga sheria au kuzirekebisha kutokana na wakati, kazi kuuza sura kwenye TV tuwaone wanavyopeana mipasho. Mahakama haiwezi toa adhabu ambayo haipo kwenye sheria. Tafakari
 
tunaomba sheria ya mtandao ianze kazi haraka uongo mwingine hauvumiliki.

Sheria ni nzuri saana,swali tunao wataalamu wa kuitekeleza......Tunazo sheria nyingi saana nzuri lakini matokeo yake balaa.Mirungi ni marufuku lakini inauzwa kama njugu na watekelezaji wa sheria wanapatia ULAJI hapo.Kutoa escort ya fuso iliyobeba mirungi kutoka namanga to Ark ni 5m ona pesa hiyo.
 
Hao majeruhi baada kuwahi vituo vya afya wakafanye check up wanakazi ya kupiga picha ili watume fesibuku....
 
Back
Top Bottom