Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Mgombea ubunge wa Karagwe, Innocent Bashungwa amesema kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) ndicho chama pekee chenye uwezo wa kuendelea kuongoza Serikali bila nchi kuingia kwenye machafuko.
Bashungwa ameyasema hayo jana Oktoba 10, 2025 katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika katika Kijiji cha Nyakayanja, Kata ya Nyaishozi, ambapo ametumia nafasi hiyo kuwataka wananchi kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu kwa kujitokeza kupiga kura za ndiyo kwa wagombea wa CCM ifikapo Oktoba 29.
“Zamu hii kina mama ni zamu yenu. Huyu ni mama mwenzenu (Samia Suluhu Hassan), naomba mumpende, tumpe ushirikiano na kura zote za kina mama ni mtaji namba moja,” amesema Bashungwa akimuombea kura mgombea urais wa CCM, Samia Suluhu Hassan.
Mbali na hilo, Bashungwa pia ametumia nafasi hiyo kuomba kura kwa ajili yake kugombea ubunge wa Karagwe pamoja na mgombea udiwani wa Kata ya Nyaishozi, Wallace Mashanda.
Ameahidi kuendelea kuboresha huduma za kijamii, ikiwemo kuboresha miundombinu ya barabara zinazounganisha vijiji mbalimbali katika jimbo hilo ili kurahisisha usafiri na shughuli za kiuchumi.
Bashungwa ameyasema hayo jana Oktoba 10, 2025 katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika katika Kijiji cha Nyakayanja, Kata ya Nyaishozi, ambapo ametumia nafasi hiyo kuwataka wananchi kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu kwa kujitokeza kupiga kura za ndiyo kwa wagombea wa CCM ifikapo Oktoba 29.
“Zamu hii kina mama ni zamu yenu. Huyu ni mama mwenzenu (Samia Suluhu Hassan), naomba mumpende, tumpe ushirikiano na kura zote za kina mama ni mtaji namba moja,” amesema Bashungwa akimuombea kura mgombea urais wa CCM, Samia Suluhu Hassan.
Mbali na hilo, Bashungwa pia ametumia nafasi hiyo kuomba kura kwa ajili yake kugombea ubunge wa Karagwe pamoja na mgombea udiwani wa Kata ya Nyaishozi, Wallace Mashanda.
Ameahidi kuendelea kuboresha huduma za kijamii, ikiwemo kuboresha miundombinu ya barabara zinazounganisha vijiji mbalimbali katika jimbo hilo ili kurahisisha usafiri na shughuli za kiuchumi.