b191
JF-Expert Member
- Jul 24, 2016
- 742
- 1,032
S.L.P ........
NYUMBANI
...../..../.....
Baba Shikamo!...
Mimi ni mzima bukheri wa afya na hofu yangu ni wewe uliye mbali na upeo wa macho yangu.
Dhumuni la barua yangu Baba ni kukutahadharisha juu ya mambo machache ambayo yanafanya siku hadi siku watu wazidi kukuchukia katika kijiji chetu ambacho wewe unakiongoza.
Mambo haya Baba ni;
1. VIWANDA.
Baba watu hawaoni kama kuna matumaini ya kujenga viwanda. Japo nasikia kuna kiwanda kimoja kimeanza kufanya kazi baada ya maagizo yako. Kiwanda hiki nasikia ni kile cha KUONGEZA BINADAMU KUZALIANA.
2. UONGO
Baba wanakijiji wanalalamika sana maana wanaona udanganyifu wako katika mambo mbalimbali. Naomba nikupe mfano,
a. Baba ulidanganya eti sisi kwenye kijiji chetu hatuhitaji msaada. Watu wamepiga hesabu,
BAJETI YA KIJIJI = Trilioni 29
MAKUSANYO YETU = Trilioni 19
UKITOA INABAKI = Trilio 11
Baba waambie wanakijiji Trilion 11 utazitoa wapi?
b. Hata zile njiwa mbili ulizonunua Baba nasikia bei yake ni kubwa sana ukilinganisha na ubora wake. Wanakijiji wanadai umewadanganya kwenye bei na hata takwimu zake pia.
c. Baba nasikia hata zile pesa walizochanga watu kwenda kwa wale waathirika hazijawafikia walengwa. Nasikia umetumia kwa mambo mengine.
d. Wanachuo wa kijiji chetu baba wanalalamika kuwa wengi wao hawajapata mikopo na wengine wamefaulu lakini wamekosa vyuo wakati wewe uliwaahidi mikopo na vyuo wote wenye sifa.
3. WASAIDIZI WABOVU
Baba nasikia umechagua wasaidizi wabovu ndiyo maana wanakijiji hawaoni kama wana msaada kwako. Japo nasikia wakati unachagua ulijitapa kuwa upo makini. Nasikia wakati unachagua uliangalia zaidi wale waliogombea vyeo katika chama chako na wakashindwa na hukuangalia sifa. Nasikia eti wengine,
a. Wanawadekisha walimu madarasa mbele ya wanafunzi
b. Wanawatishia walinzi wa kijiji
c. Wanaleta siasa hata kwenye mambo muhimu ya maendeleo
d. Wamefoji vyeti
e. Wamenunua majina ya watu na wanayatumia
f. Waliwahi kuiba mitihani na wakafutiwa matokeo.
4. UZUSHI
Baba nasikia siku hizi umekuwa unafuatilia sana maisha ya watu. Nasikia upo bize sana kujua mtu ana wake na watoto wangapi kuliko kujua matatizo ya wanakijiji.
NB: Baba wanakijiji nao wanamaswali mawili ya kizushi,
1. Eti ni kweli siku hizi Baba unatoka na umeshikwa masikio na yule Dada anayeshughulika na karo zetu. Eti ni kweli chochote anachokuambia lazima ufuate?
2. Eti kweli Baba huwa unaenda kwa Bibi kuosha nyota?
Baba natumaini utaisoma barua yangu.
Wako mwanao mpendwa.
NYUMBANI
...../..../.....
Baba Shikamo!...
Mimi ni mzima bukheri wa afya na hofu yangu ni wewe uliye mbali na upeo wa macho yangu.
Dhumuni la barua yangu Baba ni kukutahadharisha juu ya mambo machache ambayo yanafanya siku hadi siku watu wazidi kukuchukia katika kijiji chetu ambacho wewe unakiongoza.
Mambo haya Baba ni;
1. VIWANDA.
Baba watu hawaoni kama kuna matumaini ya kujenga viwanda. Japo nasikia kuna kiwanda kimoja kimeanza kufanya kazi baada ya maagizo yako. Kiwanda hiki nasikia ni kile cha KUONGEZA BINADAMU KUZALIANA.
2. UONGO
Baba wanakijiji wanalalamika sana maana wanaona udanganyifu wako katika mambo mbalimbali. Naomba nikupe mfano,
a. Baba ulidanganya eti sisi kwenye kijiji chetu hatuhitaji msaada. Watu wamepiga hesabu,
BAJETI YA KIJIJI = Trilioni 29
MAKUSANYO YETU = Trilioni 19
UKITOA INABAKI = Trilio 11
Baba waambie wanakijiji Trilion 11 utazitoa wapi?
b. Hata zile njiwa mbili ulizonunua Baba nasikia bei yake ni kubwa sana ukilinganisha na ubora wake. Wanakijiji wanadai umewadanganya kwenye bei na hata takwimu zake pia.
c. Baba nasikia hata zile pesa walizochanga watu kwenda kwa wale waathirika hazijawafikia walengwa. Nasikia umetumia kwa mambo mengine.
d. Wanachuo wa kijiji chetu baba wanalalamika kuwa wengi wao hawajapata mikopo na wengine wamefaulu lakini wamekosa vyuo wakati wewe uliwaahidi mikopo na vyuo wote wenye sifa.
3. WASAIDIZI WABOVU
Baba nasikia umechagua wasaidizi wabovu ndiyo maana wanakijiji hawaoni kama wana msaada kwako. Japo nasikia wakati unachagua ulijitapa kuwa upo makini. Nasikia wakati unachagua uliangalia zaidi wale waliogombea vyeo katika chama chako na wakashindwa na hukuangalia sifa. Nasikia eti wengine,
a. Wanawadekisha walimu madarasa mbele ya wanafunzi
b. Wanawatishia walinzi wa kijiji
c. Wanaleta siasa hata kwenye mambo muhimu ya maendeleo
d. Wamefoji vyeti
e. Wamenunua majina ya watu na wanayatumia
f. Waliwahi kuiba mitihani na wakafutiwa matokeo.
4. UZUSHI
Baba nasikia siku hizi umekuwa unafuatilia sana maisha ya watu. Nasikia upo bize sana kujua mtu ana wake na watoto wangapi kuliko kujua matatizo ya wanakijiji.
NB: Baba wanakijiji nao wanamaswali mawili ya kizushi,
1. Eti ni kweli siku hizi Baba unatoka na umeshikwa masikio na yule Dada anayeshughulika na karo zetu. Eti ni kweli chochote anachokuambia lazima ufuate?
2. Eti kweli Baba huwa unaenda kwa Bibi kuosha nyota?
Baba natumaini utaisoma barua yangu.
Wako mwanao mpendwa.